TAARIFA YA WILAYA YA HAI KWA WAZIRI
MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA
1.0.1
ENEO LA WILAYA
Wilaya
ina ukubwa wa kilometa za mraba 1,011 sawa na Hekta 101,100.
1.0. 2
IDADI YA WATU
Kwa
mujibu wa Sensa ya Kitaifa ya Watu na Makazi ya mwaka 2002, Wilaya ilikuwa na
wakazi wapatao 167,097. Wanaume 82,053
na wanawake 85,044. Kwa maoteo ya ukuaji
wa asilimia 1.9 kwa mwaka (projection), idadi ya watu kwa mwaka 2008, inakisiwa
kuwa 183,712 kwa mgawanyo wa wanaume
90,214 na wanawake 93,498. Kwa wastani
msongamano wa watu kiwilaya katika kilometa 1 ya mraba ni kati ya watu 182
ukanda wa tambarare na hufikia hadi 700
katika Ukanda wa Juu.
1.0.3 DIRA NA MWELEKEO
Katika
miaka kumi ijayo Halmashauri ya Wilaya ya Hai ichangie juhudi za kuondo
umaskini kwa kutoa huduma bora, endelevu na shirirkishi kwa kuzingatia utawala
wa sheria na usawa wa kijinsia kwa kutumia rasilimali zilizopo na kuwajibika
kwa jamii.
LENGO KUU
Lengo
kuu ni kuwa katika kipindi cha miaka mitatu halmashauri ya Wilaya ya Hai
iboreshe huduma zitolewazo za kiuchumi na kijamii kwa wastani wa asilimia kumi.
Wilaya
imegawanyika katika Kanda Kuu tatu (3) za kijiografia ambazo ni;
i. Ukanda wa
Tambarare
Ukanda huu uko chini ya meta 900 juu ya usawa wa
bahari. Hupata mvua za wastani wa kiasi cha mm. 700 kwa mwaka. Hali ya hewa ni ya joto wakati wa kiangazi.
ii. Ukanda wa
Kati
Uko kati ya meta 900 – 1,660 juu ya usawa wa
bahari. Mvua ni za wastani wa kiasi cha
mm. 750 – 1,250 kwa mwaka. Hali ya hewa
ni ya vuguvugu wakati wa kiangazi.
iii. Ukanda wa
Juu
Uko juu ya meta 1,700 juu ya usawa wa bahari. Mvua ni za wastani wa kiasi kati ya mm. 1,250
– 1,750 kwa mwaka na muda mwingi ukanda huu ni wa baridi.
MATUMIZI YA
ARDHI
Matumizi ya ardhi ya Wilaya hii, yamegawanyika katika
sehemu kuu nne,
1.
Hekta 46,506 (46%)
zinafaa kwa kilimo
2.
Hekta 14,154 (14%) ni
eneo la misitu
3.
Hekta 13,143 (13%) ni
eneo la miamba na
Hekta
27,297 (27%) ni eneo lifaalo kwa malisho ya mifugo.
1.0.5
HALI YA UCHUMI
Wastani
wa pato la mkazi wa Wilaya hii kwa mwaka 2005/2006 kwa mujibu wa utafiti
uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu mwaka 2005, lilikadiriwa kuwa Tshs.
385,000/= kwa mwaka. Hii ikiwa ni sawa
na Tshs. 32,000/= kwa mwezi. Hali hii ilisababishwa na kufululiza kwa vipindi
vya ukame, kuanguka kwa bei na kupungua kwa ubora na wingi wa zao la kahawa
ambalo ndilo zao kuu la biashara kwa wenyeji wa Wilaya hii. Kwa mwaka 2006/2007
pato la mkazi wa Wilaya ya Hai linakadiriwa kuwa ni Shs. 450,000/= hii ni sawa
na pato la Shs. 37,500/= kwa mwezi (Chanzo: Takwimu za CSPD Januari – 2007)
UCHUMI WA HALMASHAURI
Idara
ya Fedha na Biashara ni mojawapo ya Idara nane (8) za Halmashauri ya Wilaya ya
Hai kwa mujibu wa maboresho ya serikali za Mitaa na ndiyo yenye jukumu kubwa
katika ukusanyaji wa mapato.
Idara
ya Fedha na Biashara imegawanywa katika sehemu Kuu tano (5) ili kurahisisha
utendaji na utakelezaji wa majukumu
yake.
Sehemu
hizo ni
(i)
Mapato
(ii)
Matumizi
(iii)
Mishahara
(iv)
Hesabu za Mwisho
(v)
Biashara
Majukumu
ya Idara ya Fedha na biashara ni
(i)
Kuhakikisha,
kanuni, taratibu za fedha mbalimbali
inayotolewa na Serikali inafuatwa na kutekelezwa.
(ii)
Kuandaa Bajeti
ya Mapato na Matumizi kwa kushirikiana na Wakuu wa Idara na kusimamia
utekelezaji wake.
(iii)
Kuandaa taarifa
mbalimbali za fedha kulingana na miongozo na mahitaji ya Halmashauri , Wizara
ya fedha na Wizara ya Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa.
(iv)
Kuandaa Mahesabu ya kila mwisho wa mwaka wa Fedha.
(v)
Kujibu hoja za
Mdhibiti Mkuu wa Mahesabu ya Serikali
(vi)
Kuandaa mahesabu
kwa ajili ya kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC)
Mafanikio
ya Idara ya Fedha na biashara ni
TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI KWA
KIPINDI CHA 2006/2007, 2007/2008 NA 2008/2009
Idara ya fedha na bishara katika
ukusanyaji wa mapato ya halmashauri imeweza kuongeza ukusanyaji wa mapato kwa
mwaka 2006/2007 ilikusanya asilimia 83.03 na mwaka 2007/2008 kuvuka lengo la
bajeti kw asilimia 101.22. Mafanikio yametokana na kushirikiano wa wakuu wa
idara na waheshimiwa madiwani kwa kuwashawishi wananchi juu ya umuhimu wa
kulipa kodi za serikali ka ujumla wanapokuwa katika mikutano katika kata zao.
Idara ya fedha na biashara kwa
upande wa matumizi kwa kipindi cha mwaka 2006/2007, 2007/2008 na 2008/2009
imeendelea kufanya matumizi kwa mujibu wa kanuni na tartatibu za fedha na
miongozo kutoka serikalini na kwa wahisani mbalimbali.
Yafuatayo ni majedwali yanayoonyesha
mapato na matumizi kwa vipindi vya 2006/2007, 2007/2008 na 2008/2009
Mapato
|
2006/2007 |
|
|
|
|
Maelezo |
Makisio |
Halisi |
Asilimia |
|
Mapato ya Halmashauri |
353,289,200.00 |
293,351,783.92 |
83.03 |
|
Ruzuku(GPG) |
144,000,000.00 |
119,795,563.45 |
83.19 |
|
Ruzuku Mbalimbali |
8,293,000,000.00 |
8,548,366,023.51 |
103.08 |
|
Wahisani Mbalimbali |
3,030,878,200.00 |
2,082,788,145.88 |
68.72 |
|
Jumla |
11,821,167,400.00 |
11,044,301,516.76 |
93.43 |
Matumizi
|
2006/2007 |
|
|
|
|
Maelezo |
Makisio |
Halisi |
Asilimia |
|
Mapato ya Halmashauri |
353,289,200.00 |
249,334,578.77 |
70.58 |
|
Ruzuku(GPG) |
144,000,000.00 |
133,580,371.13 |
92.76 |
|
Ruzuku Mbalimbali |
8,293,000,000.00 |
8,397,866,108.86 |
101.26 |
|
Wahisani Mbalimbali |
3,030,878,200.00 |
1,530,850,455.99 |
50.51 |
|
Jumla |
11,821,167,400.00 |
10,311,631,514.75 |
87.23 |
Mapato
|
2007/2008 |
|
|
|
|
Maelezo |
Makisio |
Halisi |
Asilimia |
|
Mapato ya Halmashauri |
315,495,817.00 |
319,342,124.55 |
101.22 |
|
Ruzuku(GPG) |
187,845,000.00 |
133,249,608.56 |
70.94 |
|
Ruzuku Mbalimbali |
11,350,969,596.11 |
10,588,324,495.91 |
93.28 |
|
Wahisani Mbalimbali |
1,542,292,632.00 |
934,079,774.47 |
60.56 |
|
Jumla |
13,396,603,045.11 |
11,974,996,003.49 |
89.39 |
Matumizi
|
2007/2008 |
|
|
|
|
Maelezo |
Makisio |
Halisi |
Asilimia |
|
Mapato ya Halmashauri |
315,495,817.00 |
300,342,124.55 |
95.20 |
|
Ruzuku(GPG) |
187,845,000.00 |
130,249,608.56 |
69.34 |
|
Ruzuku Mbalimbali |
11,350,969,596.11 |
10,646,999,393.42 |
93.80 |
|
Wahisani Mbalimbali |
1,542,292,632.00 |
994,079,774.47 |
64.45 |
|
Jumla |
13,396,603,045.11 |
12,071,670,901.00 |
90.11 |
Mapato
|
2008/2009 |
|
|
|
|
Maelezo |
Makisio |
Halisi (Hadi |
Asilimia |
|
Mapato ya Halmashauri |
342,016,157.00 |
68,624,368.74 |
20.06 |
|
Ruzuku(GPG) |
150,816,000.00 |
23,268,212.50 |
15.43 |
|
Ruzuku Mbalimbali |
8,228,083,947.00 |
1,223,915,040.67 |
91.68 |
|
Wahisani Mbalimbali |
1,334,951,880.12 |
415,142,461.00 |
4.13 |
|
Jumla |
10,055,867,984.24 |
1,730,950,082.91 |
17.21 |
Matumizi
|
2008/2009 |
|
|
|
|
Maelezo |
Makisio |
Halisi (Hadi |
Asilimia |
|
Mapato ya Halmashauri |
342,016,157.00 |
54,899,494.99 |
16.05 |
|
Ruzuku(GPG) |
150,816,000.00 |
20,941,391.25 |
13.89 |
|
Ruzuku Mbalimbali |
8,228,083,947.00 |
1,221,500,475.30 |
14.85 |
|
Wahisani Mbalimbali |
1,334,951,880.12 |
373,628,214.90 |
27.99 |
|
Jumla |
10,055,867,984.24 |
1,670,969,576.44 |
16.62 |
MAFANIKIO
Halmashauri imekuwa ikivuka Malengo
yake ya ukusanyaji wa Mapato ya kutoka vyanzo vyake iliyojiwekea kila Mwaka.
CHANGAMOTO
1. Kumekuwa
na uelewa potofu kwa walipa ushuru kuhusu kodi na shuru mbalimbali ambazo zimefutwa na
wanazostahili kuzilipa.
2. Hali ya
ukame iliyoikumba Nchi nzima hivyo kusababisha uzalishaji wa Kahawa kushuka
sambamba na ushuru wa kahawa.
3. Vyanzo muhimu vya Mapato vimepungua kutokana
na kugawanyika kwa Wilaya ya Siha.
Mwelekeo kwa mwaka 2008/2009
Katika mwaka wa fedha 2008/2009
tunatarajia kukusanya jumla ya Tshs 10,055,867,984.24 na tunatarajia kufikia
lengo katika ukusanyaji wa mapato ya halmashauri
Kwa upande wa matumizi tutaendelea
kufanya matumizi kwa kuzingatia kanuni na taratibu za fedha na miongozo
mbalimbali.
MAPATO
YA SERIKALI KUU (TRA)
Taarifa ya makusanyo ya kodi
ya Wilaya Hai/Siha kwa mwaka wa fedha 2005/2006 hadi nusu mwaka wa fedha [2007/2008
Julai – Desemba 2007]. Wilaya ya Hai kwa ujumla imekuwa ikivuka lengo la
Ukusanyaji Kodi kila Mwaka kutokana hii imetokana na sababu zifuatazo;-
o
Kupanuka kwa
wigo wa walipa Kodi [Tax Base], hili limechangiwa zaidi kutokana na kugawanywa
maeneo ya Wilaya katika Blocks (Blocks Management).
o
Elimu ambayo
imetolewa kwa Walipa Kodi kwa njia ya kuwatembelea sehemu zao za Kazi.
o
Kuanzishwa kwa
Kamati za Kodi za Wilaya [District Tax Advisory Committees] ambazo zimekuwa
chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa Wilaya ambapo Katibu wake ni Meneja wa Mamlaka ya
Mapato wa Wilaya kwa mujibu wa sheria ya Kodi ya Mapato ya Mwaka 2004 kifungu
namba 129.
o
Kukua kwa Miji
ya Bomang’ombe na Sanya Juu
Kwa ujumla Wilaya imekuwa ikivuka malengo yake Mwaka
hadi Mwaka, kwa mfano katika kipindi cha Mwaka wa Fedha 2005/2006 Makusanyo
yalikuwa Tshs 728,226,964.92 dhidi ya lengo la Tshs 518,466,454.00 hivyo kuvuka
lengo kwa asilimia 140.46%. Katika kipindi cha Mwaka 2006/2007 jumla ya Tshs
1,845,242,589.53 zilikusanywa dhidi ya lengo la Tshs 1,258,598,134.00 hivyo
kuvuka lengo kwa asilimia 146.61%. Na katika Kipindi cha 2007/2008 kuanzia
Julai – Desemba jumla ya Tshs 1,845,242,589.53 zilikusanywa dhidi ya Tshs
1,258,598,134.00 zilizolengwa na hivyo kuvuka lengo kwa asilimia 101.39
MWAKA WA FEDHA 2005/2006
|
MWEZI |
LENGO KWA
MWEZI |
MAKUSANYO
HALISI |
ASILIMIA |
|
Julai 05 |
22,037,226.00 |
25,028,938.42 |
113.58% |
|
August 05 |
19,256,874.00 |
42,832,907.13 |
222.43% |
|
Sept 05 |
52,378,362.00 |
63,361,306.06 |
120.97% |
|
Oct 05 |
25,817,529.00 |
36,557,499.93 |
141.60% |
|
Nov 05 |
34,008,239.00 |
42,078,000.86 |
123.73% |
|
Dec 05 |
55,196,597.00 |
58,758,943.81 |
106.45% |
|
Jan 06 |
38,754,581.00 |
42,429,901.05 |
109.48% |
|
Feb 06 |
54,021,666.00 |
56,445,636.57 |
104.49% |
|
March 06 |
84,194,274.00 |
173,005,445.26 |
205.48% |
|
April 06 |
39,089,750.00 |
51,226,011.72 |
131.05% |
|
May 06 |
47,204,981.00 |
55,459,158.50 |
117.45% |
|
June 06 |
46,506,375.00 |
81,043,215.61 |
174.26% |
|
JUMLA |
518,466,454.00 |
728,226,964.92 |
140.46% |
MWAKA WA FEDHA 2006/2007
|
MWEZI |
LENGO KWA
MWEZI |
MAKUSANYO
HALISI |
ASILIMIA |
|
Julai 06 |
51,513,623.00 |
66,833,131.44 |
129.74% |
|
August 06 |
65,631,623.00 |
83,104,137.08 |
126.62% |
|
Sept 06 |
75,299,320.00 |
155,015,682.28 |
205.87% |
|
Oct 06 |
53,826,870.00 |
71,751,066.48 |
133.30% |
|
Nov 06 |
53,518,490.00 |
79,595,372,40 |
148.72% |
|
Dec 06 |
66,152,580.00 |
185,243,831.07 |
280.03% |
|
Jan 07 |
51,969,520.00 |
83,281,584.71 |
160.25% |
|
Feb 07 |
63,271,610.00 |
112,801,646.64 |
178.28% |
|
March 07 |
301,599,310.00 |
340,726,041.90 |
112.97% |
|
April 07 |
191,273,509.00 |
245,128,842.84 |
128.16% |
|
May 07 |
60,842,761.00 |
103,951,897.28 |
170.85% |
|
June 07 |
223,698,857.00 |
317,809,355.41 |
142.07% |
|
JUMLA |
1,258,598,134.00 |
1,845,242,589.53 |
146.61% |
MWAKA WA FEDHA 2007/2008 [JULY 2007 – DESEMBA 2007]
|
MWEZI |
LENGO KWA
MWEZI |
MAKUSANYO
HALISI |
ASILIMIA |
|
Julai 07 |
155,195,592.00 |
148,078,298.49 |
95.41% |
|
August 07 |
187,816,596.00 |
149,614,141.32 |
79.66% |
|
Sept 07 |
241,717,847.00 |
339,760,329.46 |
140.56% |
|
Oct 07 |
185,281,367.00 |
98,118,298.67 |
52.96% |
|
Nov 07 |
182,801,373.00 |
103,466,533.63 |
56.60% |
|
Dec 07 |
270,461,254.00 |
401,194,856.38 |
148.34% |
|
JUMLA |
1,258,598,134.00 |
1,845,242,589.53 |
101.39 |
1.1
UTAWALA
Kiutawala,
Wilaya ina Tarafa 3 (Lyamungo, Machame na Masama) Kata 10, Vijiji 55 na
Vitongoji 260.
Wilaya
ina Jimbo moja la uchaguzi. Katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2005 vyama vitano
vya siasa vilishiriki navyo ni; CCM, CHADEMA, TLP, CUF na SAU. Chama
kilichoshinda uchaguzi ni CCM kwa kumpata Mbunge Mheshimiwa Fuya . G. Kimbita.
Pia
katika uchaguzi huo tuliwapata Madiwani wa kuchaguliwa 8 kutoka chama cha
Mapinduzi na 2 kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Aidha wapo
madiwani wa viti maalum wanawake 4 kutoka CCM na 1 kutoka CHADEMA.
1.1.1 HALI YA ULINZI NA USALAMA
Hali
ya ulinzi na usalama ni shwari kwa ujumla.
Wananchi wanaendelea kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii
bila kujali tofauti zao za kidini, itikadi, kabila wala rangi.
Changamoto
zinazoikabili wilaya katika ulinzi na usalama ni:
1.
Uthibiti wa
mivutano ya wakulima na wafugaji ambao hutokea katika vijiji vya Mungushi,
Kware, Rundugai, Chekimaji, Chemka na Kawaya.
2.
Uthibiti wa
matukio ya ujambazi
3.
Uhamasishaji wa
wananchi kuhifadhi chakula cha kutosha kwa kila kaya
4.
Ufumbuzi wa
migogo ya mashamba na mipaka yake.
1.1.2 HALI YA KISIASA
Wilaya
ya Hai ina Jimbo moja la Uchaguzi. Katika uchaguzi uliofanyika mwaka 2005 vyama
vitano vya siasa vilishiriki navyo ni CCM, CHADEMA, TLP, CUF na SAU. Chama kilichoshinda uchaguzi ni CCM kwa
kumpata Mbunge Mheshimiwa Fuya G. Kimbita. Kwa ujumla hali ya kisiasa katika
Wilaya yetu ni shwari pamoja na mchanganyiko wa vyama tulionao, kwani tuna Kata
kumi kati ya kata hizo tuna jumla ya madiwani nane wa kuchaguliwa kutoka CCM na
wawili kutoka CHADEMA. Madiwani wa kuteuliwa tunao wanne kutoka CCM na mmoja
kutoka CHADEMA ambao kwa ujumla wao pamoja na Mbunge wanakuwa kumi na sita
ambao wanaunda Baraza la Madiwani.
2.0
UTEKELEZAJI WA MKUKUTA NA ILANI YA UCHAGUZI
2005
2.1
MALENGO, MAFANIKIO NA CHANGAMOTO 2006/2007
2.1.1
UKUAJI WA UCHUMI NA KUPUNGUZA UMASKINI WA KIPATO
2.1.1.1 KILIMO/MIFUGO 2006/2007:
Katika wilaya ya Hai kuna
hekta 46,506 zinazofaa kwa kilimo. Wilaya ina watu 183,712 ambao wanahitaji
tani 50,291.16 za wanga na tani 5,029.11
za utomwili. Kutokana na uzalishaji wa tani 183,760 za wanga na tani
18,376 za utomwili zilizozalishwa 2005/2006 wilaya ilikuwa na chakula cha
kutosha.
Katika mwaka wa 2006/2007
Halmashauri ilipata TSh. 15,998,400 kwa matumizi ya kawaida na TSh.
1,109,044,480 kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kujenga uwezo wa wadau
mbalimbali.
MALENGO:
i)Mwaka
2006/2007 Halmashauri ililenga kulima jumla ya hekta 58,749 za mazao ya chakula kwa misimu ya masika,
vuli na umwagiliaji na kuzalisha jumla ya tani 239,350 za mavuno.
ii)Kuendelea
kutunza hekta 12,655 za kahawa na kuzalisha tani1,800.
iii)Kuimarisha
kilimo cha umwagiliaji
iv)Kuongeza
tija katika mazao ya chakula na biashara
v)Kuwajengea
uwezo wadau mbalilmbali wa sekta ya kilimo na mifugo
UTEKELEZAJI:
i)Jumla ya hekta 62,930 za
mazao ya chakula zililimwa katika misimu ya masika, vuli na umwagiliaji na
kuvuna tani 172,512 za chakula
ii)Jumla ya hekta 12,655 za
kahawa ziliendelea kutunzwa na kuzalisha tani 1,543.9
iii)Mifereji 13 ya
umwagiliaji yenye thamani ya TSh. 498,098,730 ilikarabatiwa na
kuongeza eneo la umwagiliaji
kutoka hekta 3,120 hadi 4,215. Kumekuwa na ongezeko la uzalishaji kahawa,
ndizi, mahindi mpunga, maharage, mbogamboga na hatimaye ongezeko la kipato kwa
mkulima
iv)Miradi 9 ya ngo’ombe wa maziwa yenye thamani ya TSh.
258,750,000/= ilitekelezwa. Uzalishaji wa maziwa umeongezeka kutoka lita 5 hadi
lita 8 kwa ng’ombe kwa siku
Wakulima
285 wameitikia kilimo cha mazao yanayostahimili ukame mfano mihogo na ngwara.
Uzalishaji
wa kahawa umeongezeka kutoka tani 1,300 mwaka wa 2005/2006 hadi tani 1,543.9 mwaka 2006/2007
v)Warsha za utambulisho wa
programu ya kuendeleza sekta ya kilimo (ASDP) ziliendeshwa kwa viongozi, watendaji na wadau wengine wa
kilimo, pia mafunzo kwa wagani yalitolewa na vitendea kazi vilinunuliwa kwa
gharama ya TSh. 29,748,000/=.
Mahitaji ya wilaya
yalikuwa tani 6,300 za aina mbalimbali za mbolea na tani 542 za aina mbalimbali za mbegu. Wilaya ilipata
tani 2,087.4 za mbolea na tani 195 za mbegu zenye ruzuku na kuzisambaza kwa
wakulima kupitia mawakala 22.
Mahitaji ya dawa
za kuogesha mifugo aina mbalimbali yalikuwa lita 6,000. Wilaya ilipata lita 502
za dawa aina ya granade na kutumika kwenye majosho 2 na wafugaji 15 wanaotumia
mabomba ya mikono.
Changamoto:
2.1.1.2
VIWANDA NA BIASHARA 2006/2007
VIWANDA
Kwa ujumla Wilaya yetu
imekuwa na kiwanda kimoja kikubwa cha
‘Tanzania Machine Tools’ ambacho kilikuwa kinatengeneza zana za kilimo na
vipuri vya mashine, kiwanda hicho hakifanyi kazi yake sawasawa kwa sasa kwa
kuwa kipo chini ya PSRC bado kinatafutiwa mwekezaji.
MALENGO
Katika utekelezaji wa MKUKUTA
na Ilani ya Uchaguzi kama inavyotuelekeza katika ukurasa wa 36 Ibara ya 36,
Wilaya ya Hai ililenga kuhamasisha jamii na vikundi waweze kuanzisha viwanda
vidogo vidogo vya kusindika mazao
UTEKELEZAJI
Sekta ya Biashara kwa
kushirikiana na idara ya Maendeleo ya jamii ilitoa mafunzo kwa vikundi ishirini
vya wajasiriamali ili viweze kupatiwa mikopo tayari kuanzisha viwanda vidogo
vidogo.
MAFANIKIO
Viwanda vidogo vidogo 15 vya
usindikaji vimeanzishwa mfano;
usindikaji wa unga, maziwa, mafuta ya alizeti, uyoga nk.
CHANGAMOTO
1. Bajeti ni finyu na hivyo
kushindwa kutoa mafunzo kwa vikundi vingi zaidi ili viweze kuanzisha viwanda
vya usindikaji zaidi..
2. Kiwanda cha “Tanzania
Machine Tools” kutofanya kazi yake sawa sawa na hivyo kuathiri soko la ajira.
BIASHARA
Eneo
lingine ambalo Halmashauri inawajibika ni kuratibu shughuli zote za biashara
zinazofanyika Wilayani Hai Katika eneo
hili Halmashauri inawajibika kuhakikisha biashara zote zinafuata taratibu,
kanuni na sheria zilizowekwa kwa mujibu
sheria mama za biashara na sheria ndogo
ndogo za Halmashauri.
MALENGO
Katika
kipindi cha 2006/2007 malengo yalikuwa kuongeza utambuzi wa wafanyabiashara na
lesseni za biashara ili kuongeza mapato ya Halmashauri. Hali ya biashara katika
Halmasahuri ya Wilaya ya Hai ilikuwa
kama ifuatavyo:-
|
KIPINDI |
IDADI YA WAFANYA BIASHARA
WALIOKUWEPO |
LESENI MPYA ZILIZOTOLEWA WAFANYA
BIASHARA (WAPYA) |
|
2006/2007 |
1766 |
69 |
MAFANIKIO
Kutokana na kukua Kibiashara katika Wilaya yetu
mwaka mwaka 2006/2007 wafanyabiashara waliongezeka 69 na kufanya idadi kuwa jumla ya
wafanyabiashara 1,766.
CHANGAMOTO
4.
Ufinyu
wa bajeti.
5.
Wafanyabiasgara
wengi kutolipia lesseni zao za biashara kwa wakati.
2.1.1.3 MALIASILI, MAZINGIRA NA ARDHI 2006/2007
Katika
utekelezaji wa MKUKUTA na Ilani ya
Uchaguzi Halmashauri ya Wilaya imetunga na kupitisha sheria ndogo ya hifadhi ya
mazingira, ambayo pamoja mambo mengine, inakataza ukataji miti ovyo, uchomaji
wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya
maji. Pia sheria hiyo inaelekeza ni sehemu gani ambazo mifugo inatakiwa kufugwa
na sehemu ambazo kilimo kinatakiwa kufanywa.
Kwa
mwaka wa 2006/2007 malengo katika Ardhi na uhifadhi wa mazingira yalikuwa
Bajeti:
|
SEKTA |
2006-2007 |
||
|
|
H/SHAURI |
RUZUKU |
JML |
|
Ardhi |
7,423,755.00 |
|
7,423,755.00 |
|
Maliasili |
4,763,986.00 |
|
4,763,986.00 |
Utekelezaji:
Utekelezaji
ulikuwa
1.
Viwanja 200
vilipimwa na 300 kurudishiwa ‘beacons’ kwa kuwa ziling’olewa katika kitalu N.
2.
Upandaji
Miti - Jumla ya miti 1,200,000 ilipandwa
katika maeneo mbali mbali ambayo ni sawa na asilimia 80% ya lengo la miti
1,500,000.
3.
Kila Kijiji kina
Kamati ya Mazingira jumla ya Kamati 55 zimeundwa na zinafanya kazi.
4.
Sheria ndogo za
Halmashauri ya Wilaya za kudhibiti uharibifu wa Mazingira zipo na zinatumika.
5.
NGOs 5
zinashiriki kupanda miti.
6.
Vikundi 6
vinashiriki katika upandaji wa Miti.
Mafanikio:
Changamoto
Katika
kipindi hiki cha 2006/07 changamoto zifuatazo ziliikabili Idara:-
Technolojia duni.
2.1.1.4 USHIRIKA
Katika Halmashauri ya wilaya
ya Hai kuna jumla ya vyama vya Ushirika 67 vya aina mbalimbali kama ifuatavyo:
Katika utekelezaji wa malengo
ya MKUKUTA na Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005-2010, Halmashauri ya
wilaya ya Hai kupitia Idara ya Ushirika imetekeleza mambo yafuatayo:
MALENGO KWA MWAKA 2006/2007
BAJETI
Ili kufikia malengo hayo, Halmashauri ya
wilaya ilitenga jumla ya Tshs:
12,000,000/= toka DADPs na Tshs: 4,000,000.00 toka mapato ya ndani ya
Hamashauri.
UTEKELEZAJI
Mambo yaliyotekelezwa kwa
mwaka huu ni kama yafuatayo:
·
Elimu ya ushirika ilitolewa kwa viongozi wa vyama vya
ushirika 55.
·
Jumla ya viongozi 440 wa vyama vya ushirika
walihudhuria mafunzo hayo
·
Vyama vilivyokaguliwa, ukaguzi wa mara kwa mara vilikuwa vyama 4 na ukaguzi wa mwisho ilikuwa
vyama 34
·
Elimu ya ubaya wa rushwa umeelezwa katika mikutano na
vikao vya vyama vya ushirika.
MAFANIKIO
·
Hadi kufikia mwishoni mwaka 2006/2007 wanachama 780 waliongezeka, kutoka wanachama 25,024
hadi kufikia wanachama 25,804
·
Vyama vya ushirika wa Akiba na mikopo (SACCOS)
viliongezeka toka vyama vya Akiba na mikopo (SACCOS) 13 hadi vyama 20
·
Wanachama wa SACCOS waliongeza hisa zao kufikia Tshs: 316,082,441.00, waliongeza akiba zao
hadi kufikia Tshs:
913,146,249.00,amana ziliongezeka kufikia Tshs: 225,945,073.00 na
Mikopo iliyotolewa kwa wanachama ni
Tshs: 1,334,823,331.00
2.1.1.5 MASHAMBA MAKUBWA 2006/2007
MASHAMBA MAKUBWA
YANAYOMILIKIWA NAVYAMA VYA USHIRIKA
Katika wilaya ya Hai kuna mashamba 17 yanayomilikiwa na vyama vya
ushirika kama inavyoonekana kwenye Jedwali
ORODHA YA MASHAMBA
YANAYOMILIKIWA NAVYAMA VYA USHIRIKA.
|
Na. |
Jina la Shamba |
Hekta |
Mmiliki |
Mwekezaji |
Mazao |
|
1. |
Narumu |
17,116 |
Chama cha Msingi -
Lyamungo |
African |
Kahawa |
|
2. |
Xeno |
82.0 |
Chama cha Msingi -
Lyamungo |
African |
Kahawa |
|
3. |
Edelweiss |
59.2 |
Chama cha Msingi -
Lyamungo |
African |
Kahawa |
|
4. |
|
33.5 |
Chama cha Msingi - Lyamungo |
Chama cha Msingi -
Lyamungo |
Kahawa mahindi |
|
5. |
Two bridges |
421.6 |
Chama cha Msingi Narumu na Manushi |
Afican Plantation |
Kahawa |
|
6. 7. |
Silverdale na Mbono |
397.24 |
Kyeeri, |
M/s Fiona Tz. Ltd. |
Kahawa mahindi mbogamboga |
|
8. |
Glastra |
68.3 |
Chama cha Msingi Foo, Wari na Nronga |
Mkomari & Godbless
Farm Enterprises |
Kahawa Mahindi Vanilla |
|
9. |
Sirra |
21.92 |
Chama cha Msingi Foo, Wari na Nronga |
Mkomari & Godbless
Farm Enterprises |
Kahawa mahindi |
|
10. |
Lambo |
625.2 |
Chama cha Msingi Foo, Wari na Nronga |
SHITECO |
Kahawa Mahindi Snap beans |
|
11. |
Makoa estate. |
143.2 |
Chama cha Msingi Uduru Makoa |
Tierhife (T) Ltd. |
Kahawa Mahindi |
|
12. |
Makuru |
194 |
Chama cha Msingi Nshara |
N.G. Emanuel & Sons |
Kahawa mahindi |
|
13. |
Mkufi |
310.8 |
Chama cha Msingi Machame Nkuu |
N.G. Emanuel & Sons |
Kahawa na |
|
14. |
Kibo/Kikafu |
814 |
Vyama vya Msingi Roo, Saawe,Sonu,Ngira, Mudio na Masama Mula |
Tudeley Estates Ltd. |
Kahawa Mahindi |
|
15. |
Nkwansira |
218 |
Vyama vya Msingi Nkwansira, Kyuu, Isuki, Marukeni, Lemira na Mroma |
P H Ghikas & Sons Ltd. |
Kahawa Mahindi |
|
16. |
Mbosho/Uwau |
217.3 |
Chama cha Msingi Masama Mula |
Shira farming Co.ltd |
Kahawa Mahindi Mboga |
|
17. |
Boloti |
196.8 |
Lukani Losaa |
Bourbon Coffee Estate |
Kahawa |
|
18 |
Bondeni Estate |
311.2 |
Chama cha Mashua na Kashashi |
Shira Farming |
Kahawa mahindi |
MALENGO 2006/2007
MAFANIKIO
·
Mashamba 17 yalikuwa na wawekezaji
·
Ongezeko la ajira kwa wananchi
CHANGAMOTO
2.1.1.6 BARABARA:
Wilaya
ya Hai ina barabara zenye urefu wa
Km.466.2. Kati ya kilomita hizo, km. 32 ni za barabara Kuu (Trunck Roads), km.
42 ni za Mkoa (Regional Roads), km.
175.93 ni za Wilaya (District Roads) na km.150.27 ni za vijiji (Feeder
roads) na barabara za Hai Mjini ni km.66 (Hai urban roads)
Katika
kutekeleza MKUKUTA na Ilani ya
Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2005 hadi 2010 ukurasa wa 52.( ibara ya 44) Halmashauri ya Wilaya ya Hai imeendelea
kuboresha miundombinu ya barabara za Wilaya kadri bajeti ilivyoongezeka na
hivyo kupunguza adha ya usafiri na usafirishaji wa mazao mbalimbali kwa
wananchi wa Hai.
MALENGO YA MATENGENEZO YA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA WA
2006/2007 :-
Matengenezo ya kawaida ya
(km.140.4)
matengenezo
ya sehemu korofi (km
26.2)
matengenezo
ya muda maalum ( km 5 )
kuimarisha
madaraja na makalvati
usimamizi
na matengenezo ya gari la barabara,
UKARABATI WA MIUNDOMBINU WA MIRADI YA
MIFUMO YA MASOKOYA KILIMO (AMSDP)
barabara
ya Kwasadala – Longoi (km. 17.3)
Barabara
ya Mungushi – Kware (km. 3.2)
Katika
mwaka wa fedha 2006/07 barabara zenye urefu wa km. 291.2 zilifanyiwa
matengenezo kwa gharama ya TShs. 515,049,000/=
kutoka Mfuko wa barabara na mradi wa Mazao na Masoko (AMSDP). Kati ya
fedha hizo Tshs. 147,600,000/= zilitoka mfuko wa barabara (Road Fund) na
zilitumika kutengeneza km. 271.2 ambapo km. 140.4 zilifanyiwa matengenezo ya
kawaida kwa TShs. 62,870,000/=, km 26.2 zilifanyiwa matengenezo ya sehemu
korofi kwa Tshs. 35,024,000/=, km. 5 zilifanyiwa matengenezo ya muda
maalum kwa TShs. 35,000,000/=, kuimarisha madaraja na makalvati
kwa TShs. 2,080,000/= na
gharama za usimamizi na matengenezo ya gari la barabara, ni TShs. 8,000,000/=.
Mradi
wa Mazao na Masoko (AMSDP) ulitoa kiasi cha Tshs. 367,449,000/= kwa ajili ya
kukarabati barabara ya Kwasadala – Longoi (km. 17.3) kwa gharama ya Tshs.
312,449,000/= na barabara ya Mungushi – Kware (km. 3.2) kwa gharama ya Tshs.
55,000,000/=.
Mapato
haya ni sawa na asilimia 100 ya
utekelezaji wa kazi ya
lengo lililokusudiwa.
MAFANIKIO
Halmashauri
ya Wilaya ya Hai inapata mafanikio makubwa kwa kuboresha miundo mbinu
mbalimbali kutokana na kuongezeka kwa bajeti ya barabara kila mwaka (Road Fund)
na vianzia mbali mbali na kufanya barabara nyingi kupitika wakati wote.
Barabara
kupitika kwa wakati wote kumepunguza kero na adha ya usafiri na usafishaji wa
mazao mbalimbali ya wananchi kutoka mashambani kwenda nyumbani na masoko
mbalimbali ya ndani na nje ya Wilaya.
CHANGAMOTO
Halmashauri
ya Hai inafanya juhudi kubwa ya kuendeleza kuboresha miundo mbinu lakini bado
kuna baadhi ya wananchi wa korofi wanarudisha nyuma juhudi hizo kwa kupitisha
maji barabarani wakati wanamwagilia mashamba yao,kufukia mifereji ya
kuzuia/kutolea maji yasiende barabarani, wanaiba alama/samani za barabara,
wanaweka matuta barabarani bila utaratibu wa kiutaalam, wanaharibu kingo za
mito kwa kuchimba mawe na michanga hivyo kuhatarisha misingi ya madaraja,
wanaswaga/kupitisha mifugo barabarani wakati wa kupeleka malishoni au kurudisha
nyumbani.
2.1.2
UIMARISHAJI WA HUDUMA ZA JAMII
2.1.2.1MAJI 2007/2008
Wilaya
ya Hai imeweka mipango ya utekelezaji wa miradi ya maji kwa kutoa huduma ya
maji
Wilaya
inakadiriwa kuwa na wakazi wapatao 183,712 kwa sasa na wananchi wanaopata
huduma ya maji
UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI MWAKA
2006/07
Malengo:
Kupeleka
huduma ya maji katika vijiji sita vya kata ya Machame Mashariki na Zahanati ya
Mkalama.
Skimu ya maji Lyamungo.
Gharama za mradi: Mradi huu umegharimu Tshs. 1.2 billion ambazo
zimetolewa na Serikali ya Ujerumani
(KFW) kwa kushirikiana na serikali ya
Utekelezaji: Kazi zilizotekelezwa katika mradi huu ni ujenzi wa
matanki mbalimbali yenye ujazo wa lita 1,500, ununuzi wa bomba na viungio 18km na ujenzi wa matanki ya vunja msukumo matatu.
Mafanikio: Vijiji vitatu vya
Lyamungo Kilanya, Kati na Sinde vilifanikiwa kupata huduma ya maji
Uvunaji wa maji ya mvua:
Gharama za Mradi: - Mradi
huu umegharimu Tshs. 10,500,000/=
Utekelezaji: - Ujenzi
wa tanki la kuvuna maji ya mvua lenye
ujazo wa lita 50,000.
Mafanikio: - Zahanati ya Mkalama imefanikiwa kupata maji
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA
MAJI KATIKA WILAYA YA HAI
Hadi
sasa wananchi wanaopata huduma ya maji
ni asilimia 77% na inatarajiwa
kuwezesha
upatikanaji wa huduma ya maji
Changamoto:
Tatizo
la mazoea. Miradi yote ya Wilaya ya Hai ni ya Mtiririko hivyo wananchi
hawajui aina nyingine ya mradi wa maji.
Mfano
Mradi wa Kisima kirefu (borehole) wa Kijiji cha Mtakuja.
Elimu
duni juu ya aina ya vyanzo vya maji.
Biashara
ya vyuma chakavu inasababisha wananchi wasio waaminifu kuharibu miundo mbinu ya
maji.
Huduma
ya maji kuonekana kwamba ni ya bure.
Wananchi
kutoelewa madhara ya uhabifu vyanzo vya maji na
uchafuzi wa mazingira.
Mkakati
Kushirikisha
kamati ya maji
Mkuu
wa Wilaya kwa kushirikiana na kamati ya maji Safi na Mazingira ya Wilaya
kuelimisha wananchi wa kijiji cha
Mtakuja ili waweze kufikia uamuzi wa kuchagua mradi wa maji endelevu na
unaowafaa.
2.1.2.2 AFYA
Katika
kutekeleza MKUKUTA na Ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005 Ibara ya 66 kifungu (a)
hadi (j) Idara imetekeleza huduma zake kulingana na malengo ya Idara
HALI HALISI YA WILAYA
Wilaya
ya Hai ina jumla ya Hospitali 2, Vituo vya afya 3, Zahanati 48
|
AINA YA KUTUO CHA HUDUMA |
IDADI |
UMILIKI |
||
|
Serikali
|
Shirika
la Dini |
Binafsi
|
||
|
Hospitali
|
2 |
1 |
1 |
0 |
|
Vituo
vya Afya |
3 |
3 |
0 |
0 |
|
Zahanati
|
48 |
22 |
10 |
16 |
Pamoja
na Vituo hivyo vya kutolea huduma Wilaya pia ina maduka ya kuuza madawa
yapatayo 22 na kila kijiji kina wahuduma wa Afya wawili (2) wanaofanya kazi
ambao idadi
USHIRIKISHWAJI WA JAMII
Katika
utekelezaji wa huduma za Afya, Wilaya imeanzisha mfuko wa Afya ya Jamii, na
Jamii imeshirikishwa kwa kuunda Kamati za usimamizi za Hospitali, Vituo vya
Afya, na Zahanati pia Bodi ya Afya ya Wilaya imeundwa na kufunya kazi.
UIMARISHAJI WA HUDUMA ZA AFYA.
Katika
kipindi cha mwaka 2006/2007 idara iliidhinishiwa jumla ya Tshs 2,158,252,910/= kati ya fedha hizo jumla ya Tshs. 1,261,793,659/= zilitumika kulipa
mishahara ya watumishi na kiasi cha Tshs.
619,212,151/= matumizi ya kawaida.
MIRADI YA MAENDELEO
Idara
iliidhinishiwa kiasi cha Tsh.
277,247,100/= ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
MALENGO:
Utekelezaji:
TT2+ 91%
Changamoto
Mkakati:
MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI
yafutayo yalilengwa kwa mwaka 2006/2007
Fedha
zilizoidhinishwa na Halmashauri kwa mwaka wa 2006/2007 kutumika katika kazi
hizo zilikuwa Tsh 67,000,000/=
Utekelezaji:
Mafanikio:
Changamoto:
Mkakati:
2.1.2.3
ELIMU
MALENGO, MAFANIKIO NA CHANGAMOTO
2006/2007
Kulingana
na malengo ya MKUKUTA na ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005 kwa upande wa Elimu
ililenga yafuatayo:-
BAJETI YA IDARA YA ELIMU:
|
MAELEZO |
2006/2007 |
|
|
YA KASMA |
|
|
|
|
MAKISIO |
MATUMIZI |
|
PE & OC |
5,046,168,758.00 |
4,919,194,266.84 |
|
MMEM CAP |
414,344,000.00 |
227,262,904.96 |
|
MMEM DEV |
792,300,000.00 |
110,525,000.00 |
Utekelezaji wa malengo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Hai:
Ø
Uandikishaji
wa wanafunzi:
Ø
Elimu ya Awali:
Idadi
ya wanafunzi waliandikishwa katika madarasa ya Awali ni
Wav: 2028
Was: 1875 Jml: 3903
Ø
Elimu ya Msingi.
Katika
swala la uandikishaji,wa wanafunzi wa darasa la kwanza tumeandikisha watoto
wote wenye wenye umri wa miaka 7 na kuondoa mlundikano wa waliozidi umri wa miaka saba waliostahili kuandikishwa
shule ya msingi kama inavyooneshwa
katika Jedwali lifuatalo.
Uandikishwaji wa wanafunzi
darasa la I
|
MWAKA |
WALIOATARAJIWA |
WALIOANDIKISHWA |
|||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
% |
|
|
2006 |
4072 |
3921 |
7993 |
3992 |
3992 |
7915 |
99 |
|
2007 |
3175 |
2739 |
5914 |
2766 |
2595 |
5361 |
90 |
Ø
Ufaulu wa
wanafunzi na kujiunga na kidato cha kwanza
Wanafunzi waliofanya mtihani wa darasa la VII na kufaulu kuanzia mwaka 2005 – 2007 wamepata
nafasi ya kujiunga na kidato cha kwanza
kutoka asilimia 59% hadi 100% .
Mafanikio haya yametokana na kuwepo kwa juhudi za ujenzi wa vyumba vya
madarasa katika shule za Sekondari za
wananchi
Ufaulu wa wanafunzi na kuchaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza
|
MWAKA |
WALIOFANYA |
WALIOFAULU |
WALIOPATA NAFASI |
||||||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
% |
WAV |
WAS |
JML |
% |
|
|
2006 |
3225 |
3507 |
6732 |
2631 |
3177 |
5808 |
84.35% |
2435 |
2682 |
5117 |
92.4% |
|
2007 |
2425 |
2399 |
4822 |
1083 |
1267 |
2350 |
48.73% |
1083 |
1267 |
2350 |
100% |
Ø
Kusajiliwa kwa wanafunzi wote waliokosa Elimu ya
Msingi:-
Kumekuwepo
jitihada za kuanzisha
vituo kwa ajili ya kuwapatia wanafunzi Elimu ya Msingi kwa wale
walioikosa ( MEMKWA) kwa wale wote wenye
umri zaidi miaka 10 ambao walikuwa hawajaandikishwa darasa la kwanza. Mafanikio yameonekana kuwa mazuri
kwani wanafunzi 37 waliofanya mtihani wa
darasa la nne mwaka 2007 wote wamefaulu kuendelea darasa la tano
UANDIKISHAJI WA MEMKWA
|
MWAKA |
WALIOANDIKISHWA |
|
|||||||
|
KUNDI RIKA I |
KUNDI RIKA II |
JUMLA
|
|||||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
|
|
2005 |
52 |
38 |
90 |
46 |
34 |
80 |
98 |
72 |
170 |
|
2006 |
79 |
46 |
125 |
64 |
26 |
90 |
143 |
72 |
215 |
|
2007 |
22 |
15 |
37 |
- |
- |
- |
22 |
15 |
37 |
Ø
Elimu kwa wenye mahitaji maalum.
Wilaya
inafanya juhudi kuhakikisha watoto wenye mahitaji maalum wanatambuliwa na
kuthaminiwa. Katika mchakato wa kuhakikisha kwamba wanapata Elimu kama watoto wengine tayari imeanzisha
vituo vya kutolea Elimu Maalum
ELIMU KWA WENYE MAHITAJI MAALUM
|
NA |
SHULE |
WASIIONA |
VIZIWI |
ALBINO |
ULEMAVU WA AKILI |
||||||||
|
|
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
|
1 |
St.Francis
wa Asis |
9 |
5 |
14 |
17 |
27 |
44 |
11 |
5 |
16 |
1 |
1 |
2 |
|
2 |
Mbweera |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
31 |
16 |
47 |
|
3 |
KIA |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
5 |
6 |
11 |
|
4 |
Rundugai |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
- |
4 |
4 |
8 |
|
|
Jumla |
9 |
5 |
14 |
17 |
27 |
44 |
11 |
5 |
16 |
41 |
27 |
68 |
ELIMU YA UFUNDI:
Wilaya inayo vituo vya Ufundi Stadi 3 na kituo kimoja cha VETA. Vituo hivi 3 viko katika shule za msingi. Idadi ya wanafunzi katika vituo vya Ufundi
Stadi
|
KITUO |
MWAKA WA 1 |
MWAKA WA II |
JUMLA KUU |
||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
||
|
NSHARA |
29 |
- |
29 |
18 |
- |
18 |
47 |
|
MROMA |
14 |
- |
14 |
18 |
- |
18 |
32 |
|
SERE |
12 |
- |
12 |
16 |
- |
16 |
28 |
|
JUMLA |
55 |
- |
55 |
52 |
- |
52 |
107 |
MIUNDO MBINU :Wilaya kupitia idara ya Elimu ilikusudia kuongeza
miundo mbinu yakiwemo madarasa, nyumba za
walimu vyoo na utengenezaji wa madawati. Taarifa za 2005, 2006 na 2007 zinahusiana na Wilaya ya Hai na Wilaya ya
Siha
MAFANIKIO: MWAKA 2006/2007
Changamoto katika Elimu ya Msingi
2006/2007
ELIMU YA SEKONDARI:2006/2007
Wilaya
ya Hai ina shule 40 za Sekondari zikiwemo 27
za Serikali na 13 binafsi. Shule za Serikali zina wanafunzi 8202 kati
Mwaka
2005 tulikuwa na Sekondari za Serikali 14
Mwaka
2006 tulikuwa na shule za Sekondari za Serikali
27.
Mwaka
2007 na 2008 lengo ni kuongeza vyumba vya madarasa 26.
MIUNDO MBINU: 2006/2007
(i)
Mwaka 2006
vilijengwa vyumba vya madarasa 44.
(ii)
Mwaka 2007 –
Vilijengwa vyumba vya madarasa 18.
Jumla ya vyumba vya madarasa vilivyojengwa ni 62.
MAFANIKIO:
CHANGAMOTO KATIKA SHULE ZA SEKONDARI
2006/2007
2.1.3
UTAWALA BORA NA UWAJIBIKAJI
Katika
kutekeleza MKUKUTA na Ilani ya CCM 2005 -2010 kwa kuhakikisha kuwa serikali
inawajibika katika kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuzingatia Demokrasia
Ushirikishwaji na uwazi,Halmashauri imejiwekea malengo yafuatayo;
1.Kujaza
nafasi wazi za viongozi wa kuchaguliwa ngazi ya vijiji na vitongoji.
2.Kuweka
mbao za matangazo katika ofisi 10 za kata na 55 za vijiji.
3.Kuweka
masanduku ya maoni katika kata vijiji na sehemu zote za kutolea huduma.
4.Kutoa
mafunzo kwa viongozi wa kuchaguliwa ngazi ya kata na vijiji ili wafahamu wajibu
wao.
5.Kufanya
vikao vya kisheria kuanzia ngazi ya kitongoji hadi wilaya.
6.Kutoa
elimu kwa wananchi jinsi ya kupambana na Rushwa na madawa ya kulevya.
7.Kuweka
wazi taarifa zote za mapato na matumizi ya Halmashauri ili wananchi wote waweze kusoma.
8.Kuelimisha
wananchi namna ya kuibua miradi kwa kuzingatia dhana shirikishi.
Utekelezaji
wa malengo hayo unaonekana katika nyanja za Demokrasia, Uwazi na
Ushirikishwaji.
DEMOKRASIA
Kwa
mwaka 2006/2007 nafasi wazi za uongozi ngazi za chini zilijazwa
-Wenyeviti
wa vijiji - 2
-Wenyeviti
wa vitongoji -15
-Wajumbe
wa Serikali ya Kijiji - 34
Kwa
mwaka 2007/2008 nafasi hizo zilijazwa
-Wenyeviti
wa vijiji - 1
-Wenyeviti
wa vitongoji -10
-Wajumbe
wa Serekali ya Kijiji - 77
Aidha
Halmashauri imesimamia uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura, zoezi
lililoanza tarehe 22-27 Septemba 2008 ambapo wananchi wenye sifa
waliojiandikisha
Kwa
mara ya kwanza walikuwa 5,315 , walirekebisha taarifa walikuwa 3,897 na
waliofuta taarifa walikuwa 322.
Kwa
mwaka 2006/2007 vikao na mikutano ngazi ya Halmashauri, ilifanyika kwa asilimia
100%
Wilaya
inaendelea kuhamasisha na kusimamia
ngazi zote ziweze kufanya mikutano na vikao
JEDWALI A.
|
NA |
MKUTANO/VIKAO |
VILIVYOTARAJIWA |
VILIVYOFANYIKA |
ASILIMIA |
|
1 |
Mikutano
ya Halmashauri |
4 |
4 |
100 |
|
2 |
Vikao
vya Maendeleo ya Kata (WDC) |
40 |
16 |
40 |
|
3 |
Mikutano
mikuu ya Vijiji |
220 |
112 |
51 |
|
4 |
Vikao
vya serekali ya Vijiji |
660 |
412 |
62.4 |
|
5 |
Vikao
vya Vitongoji |
3084 |
1424 |
46.2 |
UWAZI
Halmashauri
pia imeweka mbao za matangazo katika kata zote 10 na vijiji 55,ambapo taarifa
zote muhimu za Halmashauri na Serikali za vijiji
USHIRIKISHWAJI
Upangaji,
Usimamizi na Utekelezaji wa Miradi mbali mbali ya Maendeleo katika ngazi ya
Vijiji umekuwa ukifanywa kwa kutumia dhana shirikishi ya Fursa na Vikwazo (O & OD).
-Mafunzo
yametolewa kwa viongozi ngazi ya kata na vijiji kuhusu namna ya kuibua
miradi,kusimamia na kutoa taarifa.
MAFANIKIO
-Wananchi wanaibua miradi
-Kata
na Vijiji vyote vimepata wawakilishi wao
katika vikao mbalimbali.
-Wananchi
wameelewa wajibu wao katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.
Changamato
-Hali
ya uitishwaji na mahudhurio kwenye vikao ngazi ya chini ni dhaifu hasa
wakati msimu wa kilimo
-Wananchi
kutokuwa na utamaduni wa kusoma mbao za matangazo
2.1.4 MAENDELEO YA JAMII (JINSIA,
WATOTO NA RUSHWA) 2006/2007
JINSIA NA WATOTO
Katika
kutekeleza Ilani ya Uchaguzi Ibara ya 17.1 ambayo ni kuelekeza nguvu katika
kuwezesha wananchi ili waweze kujiajiri mijini na vijijini, kulikuwa na malengo
yafuatayo kwa mwaka 2006/2007:
MALENGO
Kwa kipindi cha mwaka 2006/2007 malengo yalikuwa
kufanya utambuzi wa watu wanaoishi katika mazingira magumu mfano; watoto,
wazee, walemavu na wanawake kwa lengo la kupata takwimu sahihi na kuwawezesha kuanzisha
miradi midogo midogo ili kumudu maisha
MAFANIKIO
1.
Kwa kushirikiana
na mashirika yasiyo ya kiserikali mfano UNICEF na taasisi za kifedha
zinazowezesha jamii, zoezi la kutambua watoto wanaoishi katika mazingira magumu
lilifanyika pamoja na uundaji wa kamati za kuwahudumia. Jumla ya watoto 350
walisajiriwa.
2.
Halmashauri inatekeleza sera ya jinsia kila
wakati inapofanya zoezi la kuajiri watumishi.
CHANGAMOTO
Kutokana
na idadi kubwa ya watu wanaoishi katika mazingira magumu na ufinyu wa
rasilimali (fedha) bado nguvu kubwa
inahitajika ili kupunguza umaskini uliokithiri miongoni mwa jamii.
MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
MALENGO
MAFANIKIO
1.
Katika kupambana na rushwa, Halmashauri imeteua
Afisa ambaye anashughulika na masuala yote yanayohusiana na rushwa.
2.
Halmashauri kwa kushirikiana na TAKUKURU imeanzisha
klabu za wapinga Rushwa na kuizuia
madawa ya kulevya katika shule za Sekondari ili kuwaelimisha vijana
kutojihusisha katika vitendo vya Rushwa na madawa ya kulevya.
3.
Taasisi ya kupambana na kuzuia Rushwa
imekuwa ikifanya Mikutano na Wananchi kwa minajiri ya kuwaelewesha haki
zao za kimsingi, na namna wananchi wanavyotakiwa kutoa taarifa pale ambapo
wanahisi kuwepo na mianya au dalili za rushwa.
4.
Aidha Zabuni zote zinazotolewa katika kutekeleza
Miradi mbali mbali hupitia ngazi husika
na kubandikwa kwenye mbao za matangazo ili kuwa na uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji wa pamoja.
CHANGAMOTO
UTEKELEZAJI WA MKUKUTA NA ILANI YA
UCHAGUZI 2005
2.2 MALENGO, MAFANIKIO NA CHANGAMOTO
2007/2008
2.2.1 UKUAJI WA UCHUMI NA KUPUNGUZA
UMASKINI WA KIPATO
2.2.1.1 KILIMO/MIFUGO 2007/2008
Katika
wilaya ya Hai kuna hekta 46,506 zinazofaa kwa kilimo. Wilaya ina watu 183,712 ambao
wanahitaji tani 50,291.16 za wanga na tani 5,029.11 za utomwili. Uzalishaji ulikuwa tani 62,917
za wanga na 4,635 za utomwili. Kulikuwa na ziada ya vyakula vya wanga kwa wakazi wa
ukanda wa juu wanaozalisha ndizi.
Upungufu wa utomwili uilifidiwa na mazao ya mifugo mfano nyama, maziwa, mayai
na mbogamboga. Katika ukanda wa tambarare kulikuwa na upungufu wa chakula kwa
vatu 64,848 ambao walihitaji tani 4,438 za wanga na tani 443 za utomwili.
Katika kukabiliana na tatizo
hili wilaya ilipewa chakula cha msaada kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ajili ya
vijiji 16 vilivyokuwa na upungufu. Tani 165.5 zilikuwa ni za kuuza kwa bei ya
soko na tani 151 kwa bei ya Sh. 50 kwa kilo. Pia Ofisi ya Waziri Mkuu ilitoa
Sh. 2,718,000 kwa ajili ya kuchukua tani 151 kutoka SGR – Arusha hadi wilayani.
Katika mwaka wa 2007/2008 Halmashauri ilipata TSh 15,998,400 kwa matumizi ya kawaida na TSh.203,576,692/=
kwa ajili ya miradi ya maendeleo, kujenga uwezo wa wadau mbalimbali na shughuli
za ugani.
MALENGO:
i)
Mwaka 2007/2008
wilaya ililenga kulima jumla ya hekta 68,120 za mazao ya chakula msimu wa
masika, vuli na umwagiliaji na kuzalisha jumla ya tani 186,280 za chakula.
ii)
Kuendeleza na
kutunza hekta 12,655 za kahawa na kuzalisha tani 1,543.9
iii)
Kuimarisha
kilimo cha umwagiliaji
iv)
Kuongeza tija
katika mazao ya chakula na biashara
v)
Kuboresha afya
ya mifugo
vi)
Kuwajengea uwezo
wadau mbalilmbali wa sekta ya kilimo na mifugo
vii)
Kuboresha huduma
za ugani
UTEKELEZAJI:
i)Jumla ya hekta 66,980 za
mazao ya chakula zililimwa katika misimu ya masika, vuli na umwagiliaji na
kuvuna tani 246,275 za chakula
ii)Jumla ya hekta 12,655 za
kahawa ziliendelea kutunzwa na kuzalisha tani 2,568.9
iii) Ukarabati wa Mfereji
mmoja ulikarabatiwa kwa TSh.
20,000,000/= na kuongeza eneo la umwagiliaji kutoka hekta 120 hadi hekta 230. Kumekuwa na ongezeko la
uzalishaji ndizi, kahawa na mbogamboga na hatimaye kipato na lishe bora.
iv) Miradi 2 ya ufugaji bora
wa kuku yenye thamani ya TSh. 2,000,000 ilitekelezwa hivyo kuwa na ongezeko la
mayai kutoka 70 hadi 95 kwa kuku kwa mwaka.
v) Josho moja lenye thamani
ya TSh. 9,550,724/= limejengwa.
vi) Pikipiki 4, baiskeli 20,
vitendea kazi na shajala vilinunuliwa kwa wagani pamoja na mafunzo kwa wagani,
vyama ushirika na kamati za miradi yalitolewa kwa gharama ya TSh. 64,060/729/=
. Regista ya wakulima imetayarishwa na wakulima 26,200 walifikishiwa utaalam wa
uzalishaji mazao mbalimbali na ufugaji.
vii) Mafunzo ya kilimo bora
cha mazao mbalimbali na ufugaji bora yalitolewa kwa gharama ya
TSh.77,430,967/=.
Mahitaji ya mbolea
na mbegu kiwilaya yalikuwa tani 4,375 za mbolea na tani 366.5 za mbegu bora. Wilaya ilipata tani 824
za mbolea na tani 15.65 za mbegu zenye
ruzuku na kuzisambaza kwa wakulima kupitia mawakala 28.
Mahitaji ya dawa za kuogesha
mifugo aina mbalimbali yalikuwa lita 7,000. Wilaya ilipata lita 790 za dawa
aina ya tikfix na kutumika kwenye majosho 4 na wafugaji 56 wanaotumia mabomba
ya mikono.
Changamoto:
2.2.1.2
VIWANDA NA BIASHARA 2007/2008
VIWANDA
Katika utekelezaji wa MKUKUTA
na Ilani ya Uchaguzi kama inavyotuelekeza katika ukurasa wa 36 Ibara ya 36,
Wilaya ya Hai kwa mwaka wa 2007/2008 ilikuwa na malengo yafuatayo:
MAFANIKIO
1.
Vikundi ambavyo vimeanzia viwanda vidogo vidogo vya
usindikaji vimeongezeka kutoka 15 hadi 20
2.
Katika kutambua eneo la mpango wa uanzishwaji wa
viwanda (EPZ), Wilaya imetoa eneo lenye ukubwa wa hecta 463 sawa na ekari 1144
kwa ajili ya zoezi hili na tayari taratibu za mazungumzo zimeanza baina ya
wakazi wa eneo husika ili wapewe fidia na kupisha mradi wa EPZ uanze rasmi. Pia
EPZ makao makuu wameridhia mradi huo kuanzishwa Wilayani Hai kutokana na miundo
mbinu iliyopo.
CHANGAMOTO
BIASHARA
MALENGO
Katika
kipindi cha 2007/2008 malengo yalikuwa kuongeza utambuzi wa wafanyabiashara na
lesseni za biashara ili kuongeza mapato ya Halmashauri. Hali ya biashara katika
Halmasahuri ya Wilaya ya Hai ilikuwa
kama ifuatavyo:-
|
KIPINDI |
IDADI YA WAFANYA BIASHARA
WALIOKUWEPO |
LESENI MPYA ZILIZOTOLEWA WAFANYA
BIASHARA (WAPYA) |
|
2007/08 |
1198 |
81 |
MAFANIKIO
Kwa mwaka huu wafanyabiashara
wameongezeka kufikia 1198, ongezeko
CHANGAMOTO
1.
Ufinyu
wa bajeti.
2.
Wafanyabiashara
wengi kutolipia lasseni zao za biashara kwa wakati.
3.
Katika
mwaka wa Fedha 2007/08 Halmashauri
iligawanyika na kuwa Halmashauri mbili ya Siha na Hai hivyo kusababisha idadi
ya wafanyabiashara kupungua toka 1766 hadi 1198. Punguo
2.2.1.3 MALIASIRI, MAZINGIRA NA ARDHI
2007/2008
Malengo:
Kwa
mwaka wa 2007/2008 malengo katika Ardhi Maliasili na uhifadhi wa mazingira
yalikuwa
Bajeti:
|
SEKTA |
2007 – 2008 |
||
|
|
H/SHAURI |
RUZUKU |
JML |
|
Ardhi |
10,998,734 |
- |
10,998,734 |
|
Maliasili |
20,200,970 |
- |
20,200,970 |
Utekelezaji:
Utekelezaji
ulikuwa
Mafanikio
Changamoto
2.2.1.4
USHIRIKA
MALENGO
KWA MWAKA 2007/2008
·
Kuhamasisha wananchi kujiunga na vyama vya ushirika
·
Kuhamasisha wananchi kuanzisha vyama vya Akiba na
Mikopo (SACCOS)
·
Kufanya ukaguzi wa mara kwa mara na ukaguzi wa mwisho
katika vyama vya ushirika
·
Kutoa mafunzo kwa wanachama wa vyama vya ushirika
BAJETI
Ili kufanikisha malengo haya,
Halmashauri ya Wilaya ilitenga jumla ya Tshs: 9,683,830.00. toka
DADPs na Tshs: 4,683,830.00 toka mapato
ya ndani ya Hamashauri.
UTEKELEZAJI
·
Elimu ya ushirika ilitolewa kwa wanachama 720
katika vyama vya ushirika 55.
·
Ukaguzi wa kawaida ulifanyika kwa vyama 5, na ukaguzi
wa mwisho ulifanyika kwa vyama 26
·
Mikutano mikuu ya vyama vya Ushirika ilifanyika kwa
vyama vyote 67
MAFANIKIO
·
Hadi kufikia mwishoni mwaka 2007/2008 wanachama 2,079 waliongezeka, kutoka wanachama 25,804
hadi kufikia wanachama 27,883
·
Vyama vya ushirika wa Akiba na mikopo (SACCOS)
viliongezeka toka vyama vya Akiba na mikopo (SACCOS) 20 hadi vyama 25
·
Wanachama wa SACCOS waliongeza hisa zao kufikia Tshs: 336,115,613.00, waliongeza akiba zao
hadi kufikia Tshs:
985,146,249.00, amana ziliongezeka kufikia Tshs: 288,945,873.00 na
mikopo iliyotolewa kwa wanachama
Tshs: 1,334,823,331.00
2.2.1.5 MASHAMBA MAKUBWA 2007/2008
MALENGO 2007/2008
MAFANIKIO
·
Mashamba 17 yalikuwa na wawekezaji
·
Ongezeko la ajira kwa wananchi
·
Baadhi ya wawekezaji walianza kulipa kodi ya pango
CHANGAMOTO
2.2.1.6 BARABARA 2007/2008
MALENGO YA MATENGENEZO YA BARABARA KWA MWAKA WA FEDHA WA
2007/2008:-
Matengenezo ya kawaida ya
(km.96 )
matengenezo
ya sehemu korofi (km
22)
matengenezo
ya muda maalum (km 8)
kuimarisha
madaraja na makalvati
usimamizi
na matengenezo ya gari la barabara,
radi
wa Usafirishaji wa Serikali za Mitaa (Local Government Transport Programme – (LGTP)
Katika
mwaka wa fedha 2007/08 Halmashauri ya Wilaya ya Hai ilitarajia kutengeneza
jumla ya km. 130 kwa gharama ya Tshs. 228,858,000/= kutoka mfuko wa barabara na
Mradi wa Usafirishaji wa Serikali za Mitaa (Local Govt. Transport Programme –
LGTP) na utekelezaji ulikuwa kama ifuatavyo:- Mfuko wa barabara zilitolewa
kiasi cha Tshs. 185,350,000/= na kutumika kutengeneza km. 126 ambapo km. 96 ni
matengenezo ya kawaida kwa TShs. 86,950,000/=, km. 8 ni matengenzo ya muda
maalum kwa TShs. 46,400,000/=, km. 22 ni
matengenezo ya maeneo korofi kwa TShs. 25,2000,000/=, makalvati na madaraja yalitengenezwa kwa TShs. 15,200,000/=,
usimamizi na matengenezo ya gari la
barabara. TShs. 11,600,000/=.
Aidha
zilitolewa TShs. 24,693,455/= kati ya makisio ya TShs. 43,508,000/= kutoka
Mradi wa Usafirishaji wa Serikali za Mitaa (Local Government Transport Programme – LGTP) na kutumika kutengeneza km.
1 kwa kuinua tuta la barabara ya Bomang’ome – Kikavu chini(eneo la Cheki Maji
Kawaya), kwa TShs. 20,600,000/=, kutengeneza
makalvati vipande 14 ( 600 mm dia.x 14m.) TShs. 420,000/= na kukusanya na kuandaa
takwimu za barabara za Wilaya kwa TShs. 3,673,455/=
Mapato
haya ni sawa na asilimia 55 ya kazi ya
lengo lililokusudiwa (LGTP) na asilima 100 kwa mfuko wa barabara.
MAFANIKIO KWA MWAKA 2007/2008
Halmashauri
ya Wilaya ya Hai inapata mafanikio makubwa kwa kuboresha miundo mbinu mbalimbali
kutokana na kuongezeka kwa bajeti ya barabara kila mwaka (Road Fund) na vianzia
mbali mbali na kufanya barabara nyingi kupitika wakati wote.
Barabara
kupitika kwa wakati wote kumepunguza kero na adha ya usafiri na usafishaji wa
mazao mbalimbali ya wananchi kutoka mashambani kwenda nyumbani na masoko
mbalimbali ya ndani na nje ya Wilaya.
CHANGAMOTO
Halmashauri
ya Hai inafanya juhudi kubwa ya kuendeleza kuboresha miundo mbinu lakini bado
kuna baadhi ya wananchi wa korofi wanarudisha nyuma juhudi hizo kwa kupitisha
maji barabarani wakati wanamwagilia mashamba yao,kufukia mifereji ya
kuzuia/kutolea maji yasiende barabarani, wanaiba alama/samani za barabara,
wanaweka matuta barabarani bila utaratibu wa kiutaalam, wanaharibu kingo za
mito kwa kuchimba mawe na michanga hivyo kuhatarisha misingi ya madaraja,
wanaswaga/kupitisha mifugo barabarani wakati wa kupeleka malishoni au kurudisha
nyumbani.
2.2.2
UIMARISHAJI WA HUDUMA ZA JAMII
2.2.2.1 MAJI
UTEKELEZAJI MIRADI YA MAJI MWAKA
2007/08
Malengo:-
-
Kupeleka huduma
ya maji katika Kijiji cha Tindigani, Mtakuja,na Kwatito.
-
Kupeleka
huduma ya maji vijiji vitatu vya
Kata ya Machame Mashariki.
-
Kutoa elimu juu ya sera ya maji ya Taifa.
-
Kuendesha
kongamano la utunzaji na usafi wa mazingira katika mji wa Hai.
Skimu ya maji ya Kijiji cha Mtakuja.
Gharama za mradi: Mradi huu umegharimu Tshs. 84,000,000/= ambazo
zimetolewa na Serikali kuu.
Utekelezaji: Kazi zilizotekelezwa katika mradi huu ni ujenzi wa
tanki la juu lenye ujazo wa lita 50,000 pamoja na ununuzi wa bomba na viungio
umbali wa 1.2km.
Mafanikio: Utekekelezaji wa mradi umefikia asilimia 40. Mradi utaendelea kujengwa kwa kutumia
wataalam washauri wa Mradi wa Maji Safi na usafi wa mazingira.
Skimu ya Maji Lyamungo:
Gharama za mradi: Mradi huu umegharimu Tshs. 1.2 billion ambazo
zimetolewa na Seriklai ya Ujerumani (KFW) kwa kushirikiana na Serikali ya
Utekelezaji: Kazi zilizotekelezwa katika mradi huu ni ujenzi wa
tawi la maji umbali wa 14km, Ujenzi wa vilula 8 na matanki mawili ya kuvunja
msukumo wa maji.
Mafanikio: Kazi imekamilika na jumla ya wananchi 3500 na
wanafunzi 260 wanapata huduma ya maji
Maadhimisho ya wiki ya maji
ya taifa
Gharama: Maadhimisho ya wiki ya maji mwezi Machi mwaka 2008
yamegharimu Tshs. 1,200,000/= ambazo zimetolewa na wadau wa maji.
Utekelezaji:
Sera
ya maji imeelimisha katika vijijiji vitatu.
Kamati
za maji zimeundwa katika vijiji viwili
Jumla
ya wadau sitini katika kata ya Hai Mjini
wameelimishwa kuhusu utunzaji wa mazingira.
Mafanikio:
Uelewa
wa sera ya maji ya Taifa na athari za uchafu wa mazingira.
Skimu ya maji ya Kijiji cha Tindigani
Gharama za Mradi:
Mradi
huu umegharimu Tshs. 40,000,000/= ambazo zimetolewa na Serikali kuu
Utekelezaji:
Ununuzi
wa bomba umbali wa km 4.5, kuchimba
mtaro na kufukia bomba umbali wa km.4.5
pamoja na ujenzi wa vilula vitatu.
Mafanikio: Jumla
ya wananchi 1112 na wanafunzi 336 wanapata huduma ya maji
CHANGAMOTO
Kuwezesha
upatikanaji wa huduma ya maji
Kushirikisha
wananchi ili kupinga kwa nguvu zote biashara ya vyuma chakavu kwani
inasababisha kuibiwa kwa miundombinu ya miradi ya maji.
Kuelimisha
wananchi ili kuondoa imani kuwa huduma ya maji ni bure.
Kushirikisha
sekta nyingine za kijamii ili kuelimisha wananchi madhara ya uharibifu wa
vyanzo vya maji na mazingira kwa ujumla.
MIKAKATI
Kukarabati
skimu ya Maji Machame na kuanza ujenzi wa skimu ya Maji Mkalama chini ya mradi
wa maji Hai District Water Supply Project awamu ya nne rudio la pili. Kushirikiana
na wataalam washauri wa Miradi ya Maji na usafi wa mazingira (NRWSSP)
watakaoteuliwa ili kuwezesha ujenzi wa mradi katika vijiji tisa vya ukanda wa
chini wa Wilaya kuanzia mwezi Januari 2009.
Kuendelea
kutoa elimu kuhusu sera ya maji ya Taifa (2002).
2.2.2.2
AFYA
Mwaka
2007/2008
Katika kipindi cha mwaka 2007/2008 idara
iliidhinishiwa jumla ya Tsh.
1,731,521,294/= kati ya fedha hizo jumla ya Tshs. 1,003,411,912/= zilitumiwa kukamilisha kulipa mishahara ya
watumishi na kiasi cha Tshs.
708,588,280/= matumizi ya kawaida.
MIRADI YA
MAENDELEO
Idara iliidhinishiwa kiasi cha Tsh. 19,521,102/= ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Malengo:
-
Hospitali ya
Wilaya ya Hai.
-
Kituo cha Afya
Masama
-
Kituo cha Afya
Kisiki
-
Zahanati ya
Weruweru.
-
Zahanati ya KIA
Utekelezaji:
Mafanikio:
Changamoto:
MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI
Kwa mwaka
wa 2007/2008 yafuatayo yalilengwa
Utekelezaji:
1.
Vikundi vya
wanaoishi na virusi vya UKIMWI vimeundwa katika Kata zote 10 za Wilaya.
2.
Tulipima jumla
ya watu 24,551 kati ya lengo la kupima watu 22,829 hivyo kuvuka lengo kwa
107.5%.
3.
Jengo limejengwa
na kukamilika.
Mafanikio:
Changamoto:
Mkakati:
-
Kuendelea kutoa
elimu ya faida za kujiunga na vikundi kwa wale bado.
-
Kushirikiana na
wadau mbalimbali kuomba fedha za kutoa mafunzo kwa Wataalam wa Afya.
2.2.2.3
ELIMU
MALENGO, MAFANIKIO NA CHANGAMOTO
2007/2008
Kulingana
na malengo ya MKUKUTA na ilani ya uchaguzi ya mwaka 2005 kwa upande wa Elimu
ililenga yafuatayo:-
BAJETI YA IDARA YA ELIMU:
|
MAELEZO |
2007/2008 |
|
|
YA KASMA |
|
|
|
|
MAKISIO |
MATUMIZI |
|
PE & OC |
5,377,819,935.00 |
5,412,608,344.74 |
|
MMEM CAP |
211,635,000.00 |
197,846,956.00 |
|
MMEM DEV |
528,106,020.00 |
- |
Utekelezaji wa malengo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Hai:
Ø
Uandikishaji
wa wanafunzi:
Ø
Elimu ya Awali:
Idadi
ya wanafunzi waliandikishwa katika madarasa ya Awali ni
Wav: 2028
Was: 1875 Jml: 3903
Ø
Elimu ya Msingi.
Katika
swala la uandikishaji,wa wanafunzi wa darasa la kwanza tumeandikisha watoto
wote wenye wenye umri wa miaka 7 na kuondoa mlundikano wa waliozidi umri wa miaka saba waliostahili kuandikishwa
shule ya msingi kama inavyooneshwa
katika Jedwali lifuatalo.
Uandikishwaji wa wanafunzi
darasa la I
|
MWAKA |
WALIOATARAJIWA |
WALIOANDIKISHWA |
|||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
% |
|
|
2007 |
3175 |
2739 |
5914 |
2766 |
2595 |
5361 |
90 |
|
2008 |
2657 |
2522 |
5179 |
2716 |
2475 |
5191 |
100 |
Ø
Ufaulu wa
wanafunzi na kujiunga na kidato cha kwanza
Ufaulu wa wanafunzi kwa mwaka 2007/2008 ni
|
MWAKA |
WALIOFANYA |
WALIOFAULU |
WALIOPATA NAFASI |
||||||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
% |
WAV |
WAS |
JML |
% |
|
|
2007 |
2425 |
2399 |
4822 |
1083 |
1267 |
2350 |
48.73% |
1083 |
1267 |
2350 |
100% |
|
2008 |
2980 |
3092 |
6072 |
|
|
|
|
|
|
|
|
Wavulana 3038
Wasichana 3113. Waliofanya mtihani ni 6072 sawa na asilimia 98.7%. Tunatarajia wanafunzi 5465 watakaofaulu ambao
ni sawa na asilimia 90.
Ø
Kusajiliwa kwa wanafunzi wote waliokosa Elimu ya
Msingi:-
Kwa
mwaka wa 2007/2008 wanafunzi walioandikishwa kwa mpango wa MEMKWA ni
UANDIKISHAJI WA MEMKWA
|
MWAKA |
WALIOANDIKISHWA |
|
|||||||
|
KUNDI RIKA I |
KUNDI RIKA II |
JUMLA
|
|||||||
|
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
WAV |
WAS |
JML |
|
|
2007 |
22 |
15 |
37 |
- |
- |
- |
22 |
15 |
37 |
|
2008 |
22 |
11 |
33 |
|
|
|
|
|
|
MAFANIKIO: MWAKA 2007/ 2008
b.
Kumekuwa na
ongezeko la miundo mbinu katika kupunguza msongamano wa wanafunzi – darasa I
wanafunzi 40 – 50. Dawati 1 wanafunzi 2
– 3.
c.
Shule nyingi
zimeboresha mazingira hasa uoteshaji wa miti ya kivuli, uzio (sawa na shule 68
kati ya shule 103) sawa na asilimia 66%.
d.
Walimu
wamejiendeleza katika programu ya MUKA na waliobaki ni walimu daraja B/C ambao
ni 35 kati ya walimu 539 sawa na asilimia 6.4
e.
Ujenzi wa visima
vya kuvuna maji. Hadi sasa vimejengwa
visima 35 kati ya vituo 103 sawa na asilimia 32%.
Changamoto katika Elimu ya Msingi
2007/2008
(i)
Baadhi ya
familia kuwaficha baadhi ya watoto wenye
kuhitaji Elimu maalum.
(ii)
Miundo mbinu
kutokukamilika kwa wakati kutokana na mfumuko wa bei na kipato cha wananchi.
(iii)
Idadi ya watoto
wanaoandikishwa na wanaomaliza kutofautiana hasa maeneo ya wafugaji.
(iv)
Ujenzi wa kituo
kikuu cha Wilaya cha walimu kwa ajili ya kuendesha mafunzo na semina mbalimbali.
(v)
Kutokana na eneo
la shule kuwa finyu miundo mbinu mingine inashindikana kuwepo shuleni – mfano
nyumba za walimu , maktaba, bwalo la chakula, viwanja vya michezo n.k.
(vi)
Ujenzi wa shule
ya waalemavu ya Wilaya (Multipurpose Centre)
(vii)
Vituo vya Ufundi
vina uhaba mkubwa wa vifaa na upungufu wa walimu wa fani za ufundi
ELIMU YA SEKONDARI: 2007/2008
Wilaya
ya Hai ina shule 40 za Sekondari zikiwemo 27
za Serikali na 13 binafsi. Shule za Serikali zina wanafunzi 8202 kati
MALENGO
Mwaka
2007 na 2008 lengo ni kuongeza vyumba vya madarasa 26.
MAFANIKIO:2007/2008
CHANGAMOTO KATIKA SHULE ZA SEKONDARI
2007/2008
2.2.3 UTAWALA
BORA NA UWAJIBIKAJI 2007/2008
Kwa mwaka 2007/2008 vikao vya ngazi ya Wilaya
vilifanyika kwa asilimia 100, ngazi ya
Kata (WDC), asilimia 77.5, mikutano mikuu ya vijiji na asilimia 55.4, vikao vya
Halmashauri za vijiji asilimia 69 na mikutano ya vitongoji asilimia 51, kama
inavyoonekana katika Jedwali.
JEDWALI
|
NA |
MKUTANO/VIKAO |
VILIVYOTARAJIWA |
VILIVYOFANYIKA |
ASILIMIA |
|
1 |
Mikutano
ya Halmashauri |
4 |
4 |
100 |
|
2 |
Vikao
vya Maendeleo ya Kata (WDC) |
40 |
31 |
77.5 |
|
3 |
Mikutano
mikuu ya Vijiji |
220 |
122 |
55.4 |
|
4 |
Vikao
vya serekali ya Vijiji |
660 |
456 |
69 |
|
5 |
Vikao
vya Vitongoji |
3084 |
1573 |
51 |
2.2.3.1
MAENDELEO YA JAMII (JINSIA, WATOTO NA RUSHWA)
JINSIA NA WATOTO
Katika
kutekeleza Ilani ya Uchaguzi Ibara ya 17.1 ambayo ni kuelekeza nguvu katika
kuwezesha wananchi ili waweze kujiajiri mijini na vijijini, kulikuwa na malengo
yafuatayo kwa mwaka 2007/2008 kwa upande wa jinsia na watoto:
MALENGO
Kwa
kipindi cha mwaka 2007/2008 malengo yalikuwa kuendelea kufanya utambuzi wa
watoto wanaoishi katika mazingira magumu, kutekeleza sera ya jinsia na
kuendelea kuwezesha makundi ya wajasiriamali kutoka vikundi tisini hadi 180
ifikapo mwaka 2008
MAFANIKIO
(i)
Wilaya
imefanikiwa kupata takwimu za watoto waishio katika mazingiara magumu na
hatarishi kutoka kata zote kumi. Jumla ya watoto hao ni 7,392.Me 3873 na Ke
3509. Uhamasishaji wa kuandaa mipango ya kuwezesha watoto hao umefanyika katika
vijiji vyote 55 na kila kijiji kimefungua akaunti kwa ajiri ya kuwawezesha
watoto hao kutokana na taratibu walizojiwekea wenyewe.
(ii)
Vikundi vimeongezeka kwa lengo la kuunganisha
nguvu na kujikwamua kiuchumi kutoka tisini hadi 228 hivyo kuvuka lengo
tulilojiwekea
(iii)
Halmashauri
inatekeleza sera ya jinsia kila wakati inapofanya zoezi la kuajiri watumishi.
CHANGAMOTO
(i)
Kutokana na
idadi kubwa ya watu wanaoishi katika mazingira magumu na ufinyu wa rasilimali
(fedha) bado nguvu kubwa inahitajika ili
kupunguza umaskini uliokithiri miongoni
mwa jamii.
(ii)
Idadi ya watoto
wanaoishi katika mazingira hatarishi inabadilika mara kwa mara kwa sababu ya
vifo vinavyosababishwa na ugonjwa wa UKIMWI, madawa ya kulevya na wazazi wenye
vipato duni.
(iii)
Idadi watu
wanaotakiwa kusaidiwa ni kubwa ukilinganisha na ufinyu wa bajeti iliyopo.
MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA
MALENGO
(i)
Kufanya mikutano
na wananchi kuwaelimisha juu mapambano dhidi ya rushwa.
(ii)
Kuendelea
kuanzisha klabu za wapinga rushwa shuleni.
MAFANIKIO
(i)
Katika kupambana
na rushwa, Halmashauri imeteua Afisa ambaye anashughulika na masuala yote
yanayohusiana na rushwa.
(ii)
Halmashauri kwa
kushirikiana na TAKUKURU imeendelea kuanzisha klabu za wapinga Rushwa na kuzuia madawa ya kulevya katika shule za
Sekondari ili kuwaelimisha vijana kutojihusisha katika vitendo vya Rushwa na
madawa ya kulevya.
(iii)
Taasisi ya
kupambana na kuzuia Rushwa imeendelea
kufanya Mikutano na Wananchi kwa
minajiri ya kuwaelewesha haki zao za kimsingi, na namna wananchi wanavyotakiwa
kutoa taarifa pale ambapo wanahisi kuwepo na mianya au dalili za rushwa.
(iv)
Aidha Zabuni
zote zinazotolewa katika kutekeleza Miradi mbali mbali zimeendelea kupitishwa ngazi husika na
kubandikwa kwenye mbao za matangazo ili kuwa na uwazi, ushirikishwaji na
uwajibikaji wa pamoja.
CHANGAMOTO
1.Elimu zaidi juu ya Rushwa inahitajika kwakuwa
wananchi wana uelewa mdogo juu ya aina mbalimbali za rushwa.
2.Wanachi bado wanahofu ya kutoa taarifa sahii juu
rushwa kwa kuhofia usalama wao na kukosa baadhi ya haki fulani katika jamii
3.0 MWELEKEO NA MPANGO WA BAJETI
2008/2009 KATIKA UTEKELEZAJI
WA MKUKUTA NA ILANI YA UCHAGUZI 2005
3.1 UKUAJI WA UCHUMI NA KUPUNGUZA
UMASKINI WA KIPATO
3.1.1 MWELEKEO KATIKA SEKTA YA KILIMO/MIFUGO
2008/2009
Katika
wilaya ya Hai kuna hekta 46,506 zinazofaa kwa kilimo. Wilaya ina watu 183,712
ambao wanahitaji tani 50,291.16 za wanga na tani 5,029.11 za utomwili.
Uzalishaji ulikuwa tani 80,550 za wanga na 7,500 za utomwili mwaka 2007/2008. Kutakuwepo ziada
ya chakula 2008/2009. Wakulima wanaendelea kushauriwa kuhifadhi chakula na
kutokuuza nje ya nchi.
Idara ya Kilimo/Mifugo
imekasimiwa TSh. 455,250,000/= kwa
matumizi ya kawaida na mishahara na TSh. 500,689,374/= kwa ajili ya miradi ya
maendeleo, kujenga uwezo wa wadau mbalimbali na shughuli za ugani.
MALENGO:
Mwaka 2008/2009 wilaya imelenga kulima jumla ya hekta
68,120 za mazao ya chakula msimu wa masika, vuli na umwagiliaji na kuzalisha
jumla ya tani 186,280 za chakula. Wilaya itahitaji tani 7,800 za aina
mbalimbali za mbolea na tani 803 za mbegu bora ya mahindi. Mahitaji ya dawa
za kuogesha mifugo aina mbalimbali ni lita 7,000.
i)
Kuendeleza na
kutunza hekta 12,655 za kahawa na kuzalisha tani 2,600
ii)
Kuimarisha
kilimo cha umwagiliaji kwa gharama ya TSh. 110,879,750/=
iii)
Kufufua zao la
kahawa kwa gharama Tsh. 4,000,000
iii) Kuongeza tija katika mazao ya chakula
kwa gharama TSh.16,080,000
iv) Kuboresha afya na uzalishaji mifugo kwa
gharama ya TSh. 125,011,723/=
iv)
Kuwajengea uwezo
wadau mbalilmbali wa sekta ya kilimo na mifugo kwa
gharama ya TSh. 166,911,752
vi) Kuboresha huduma za ugani kwa gharama
ya TSh. 66,814,224/=
UTEKELEZAJI:
3.1.2
VIWANDA NA BIASHARA
MWELEKEO
WA VIWANDA 2008/2009
MWELEKEO
WA BISHARA 2008/2009
3.1.3
MALIASILI, MAZINGIRA NA ARDHI
MWELEKEO
Mwenendo na mwelekeo wa
kufanikisha malengo na makusudio ya 2008/2009 ni kama ifuatavyo:
3.1.4
USHIRIKA
MALENGO
KWA MWAKA 2008/2009
·
Kuendesha mafunzo ya awali ya uhasibu kwa SACCOS 40
·
Kuendesha mafunzo ya mbinu ya kutafuta masoko kwa
SACCOS 40
·
Kuendesha mafunzo kwa vyama vya msingi 65 juu ya
urekebishaji wa sheria ndogondogo(Bylaws) kulingana na sheriaya ya vyama vya vyama ushirika ya mwaka 2003.
·
Ukaguzi wa kawaida kwa vyama vya ushirika 6
·
Ukaguzi wa mwisho katika vyama 65
Kwa mwaka wa fedha
2008/2009 Halmashauri imeomba
kibali ili kuajiri maafisa Ushirika
wawili.
3.1.5 MWELEKEO MASHAMBA MAKUBWA 2008/2009
MALENGO 2008/2009
MPANGO WA BAADAYE
3.1.6 MWELEKEO WA BARABARA 2008/2009
Kwa
mwaka wa fedha 2008/09 Halmashauri ya Wilaya ya Hai inatarajia kupata
Tshs.
359,600,000/= kutoka mfuko wa barabara na Mradi wa Usafirishaji wa Serikali za
Mitaa (LGTP) kwa ajili ya
kuimarisha km. 218.6 za barabara
za Wilaya. Kati ya fedha hizo kiasi cha
Tshs. 243,600,000/= zitatoka mfuko wa barabara (Road Fund) kwa ajili ya
matengenezo ya km. 189.6 ambapo kati ya
kilometa hizo km. 170.6 zitafanyiwa matengenezo ya kawaida kwa Tshs.
127,970,000/=, km. 14 zitafanyiwa matengenezo ya maeneo korofi kwa TShs.
22,700,000/=, km. 5 zitafanyiwa
matengenezo ya muda maalum kwa Tshs. 60,000,000/=, ujenzi wa makalvati zitatumika Tshs.
15,000,000/= na kwa ajili ya usimamizi na matengenezo ya gari la barabara
zitatumika
TShs.
18,000,000/=.
Pia
Halmashauri ya Wilaya inatarajia kupokea na kutumia Tshs. 116,000,000/= kutoka
Local Government Transport Programme (LGTP) kwa ajili ya matengenezo km. 29 za
maeneo korofi za barabara mbalimbali za
Wilaya ya Hai na kujenga makalvati yenye
kipenyo cha ( 600 mm.x 168 m.) au line
24 zenye urefu wa mita 7 kila moja.
MIKAKATI
Viongozi
wa ngazi zote wahamasishe wananchi/wadau ili waweze kuelewa kuwa barabara ni
sehemu ya mali yao na waweze kuitunza na kama ikitokea uharibufu wowote ule
watoe taarifa haraka kwa uongozi wa juu ili tatizo hilo litatuliwe mapema
iwezekanavyo.
Halmashauri
ya Wilaya ya Hai kwa kutumia kitengo chake cha sheria itatunga sheria ndogo (BY
LAW) kwa ajili ya utunzaji wa barabara za Wilaya
3.2
UIMARISHAJI WA HUDUMA ZA JAMII
3.2.1 UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAJI
MWAKA 2008/09
Malengo:
Kupeleka huduma ya maji katika vijiji sita vya kata
ya Machame Kaskazini.
Kuanza kwa mradi wa
maji safi na usafi wa mazingira
katika vijiji tisa vya ukanda wa chini wa Wilaya ya Hai.
Kuboresha huduma ya maji katika vijiji saba vya mradi wa maji Losaa Kia.
Skimu
ya maji Machame
Gharama za Mradi
Mradi
huu utagharimu EURO 2.1 million ambazo
ni sawa na Tshs. Billion 4 za
Utekelezaj:
Kazi
ya mradi imeanza mwezi Julai 2008. Ujenzi wa vyanzo vitatu vya maji umefikia asilimia 50.
Matarajio: Mradi ukikamilika jumla ya vijiji sita vitapata
maji
Mradi wa maji
Gharama za Mradi:
Gharama
za mradi ni Tshs. 380,892,000/= ambazo zitatolewa na benki ya dunia kwa
kushirikiana na Serikali ya
Utekelezaj:
Mchakato
wa kumpata mkandarasi mshauri wa
mradi umefanyika na watashindanishwa wawili baada ya kupata kibali cha benki ya dunia.
Matarajio:
Utekelezaji rasmi wa mradi unatarajiwa kuanza
mwezi Januari 2009.
Skimu ya maji ya kijiji cha Sanya
station.
Gharama za mradi: Mradi huu umegharimu Tshs. 42,530,000/= ambazo
zimetolewa na Serikali kuu.
Utekelezaji: Ujenzi wa tanki la juu lenye ujazo wa lita 50,000
na ujenzi umefikia asilimia 50. Kazi ya ujenzi inaendelea.
Skimu ya maji katika vijiji vya Mudio,
Nkwansira, Nguni, Isuki, Mungushi na Mborenyi.
Gharama za mradi: Gharama za ununuzi wa bomba na viungio vyenye urefu wa 4.050km ni Tshs. 22,447,000/=.
Utekelezaji: Kazi ya ulazaji bomba umbali wa km 4.050 inaendelea.
Matarajio: Kazi
hiyo ikikamilika idadi ya wananchi 9,000
watapata huduma ya maji
3.2.2 MWELEKEO WA AFYA 2008/2009
Katika kipindi cha mwaka 2008/2009 Wilaya imeomba
jumla ya Tshs.2,455,246,807.80 kati
ya hizo Tshs. 1,223,351,908.80
zitatumika kulipia mishahara ya watumishi wa Sekta ya afya. Fedha hizo ni sawa
na ongezeko la asilimia 50.28 katika bajeti ya mwaka 2007/2008. na Tsh.
1,195,894,899 kwa matumizi ya kawaida. Fedha zilizoombwa zitatumika
kuendeshea shughuli 144
MIRADI YA MAENDELEO
Idara
iliidhinishiwa kiasi cha Tsh.
36,000,000/= ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo.
Malengo:
Mkakati:
1.
Kukamilisha
chumba cha kuhifadhia maiti kwenye Hospitali ya Wilaya.
2.
Kujenga chumba
cha upasuaji na X-ray Hospitali ya Wilaya.
3.
Kupatikana kwa
gari maalumu la kubebea wagonjwa wa hospitali ya Wilaya.
4.
Kufanya ukaguzi
wa kila kaya ili kuhakikisha kuwa na choo cha kudumu.
3.2.3 MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI
Mwelekeo 2008/2009:
Katika
mwaka wa Fedha 2008/2009 jumla ya Tshs 59,309,000.00 zimeidhinishwa toka Hazina
kwa ajili ya utekelezaji wa afua mbali mbali za UKIMWI zikiwa ni:-
Mkakati:
Idara
itahakikisha malengo yaliyopangwa yatatekelezwa kikamilifu na kuendelea na
uhamasishaji wa wananchi kuhusu upimaji wa hiari wa Afya zao.
3.2.4 ELIMU MWELEKEO WA BAJETI KWA
MWAKA WA 2008/2009
Katika
mwelekeo wa bajeti kwa mwaka wa 2008/2009 fedha zilizoteidhinishwa kutoka
hazina ni
Halmashauri
inayo mkakati wa kuongeza vyumba vya madarasa kwa ajili ya kupokea wanafunzi wa
kidato cha kwanza mwaka 2009. Pia tunao
mkakati wa kuhakikisha kwamba shule zote zenye upungufu wa madarasa na matundu
ya vyoo yanajengwa.
MWELEKEO WA BAJETI YA IDARA YA ELIMU
2008/2009:
|
MAELEZO |
2008/2009 |
|
YA KASMA |
|
|
|
MAKISIO |
|
PE & OC |
5,278,186,835.00 |
|
MMEM CAP |
226,000,000.00 |
|
MMEM DEV |
24,430,000.00 |
ELIMU YA UFUNDI:
Wilaya ina Kituo 1 kipya kinachotarajiwa kuanza mwaka
2009 Januari.
3.3 UTAWALA BORA NA UWAJIBIKAJI
.MWELEKEO
NA MPANGO 2008/2009
Kwa
mwaka 2008/2009, tunatarajia vikao na mikutano yote ya
kisheria ifanyike kwa mujibu wa ratiba, kwani hadi mwezi Septemba 2008, vikao
na mikutano iliyotakiwa kufanyika imefanyika kwa mujibu wa ratiba, katika ngazi
za Kata na Vijiji.
-Halmashauri
imeweka mpango madhubuti wa kuwalipa wenyeviti wa vijiji na vitongoji posho zao
kwa wakati na imeshalipa kiasi cha shilingi 22,000,000/- ili kuwahamasisha
viongozi hao kufanya kazi zao vizuri hasa uitishwaji wa vikao katika maeneo
-Kiasi cha Tshs 7,581,740.00 kitatolewa toka
katika ruzuku ya kujenga uwezo kwa ajili ya kukuza demokrasia katika Ngazi za
Vijiji na Kata kwa kutoa mafunzo kwa Waheshimiwa Madiwani, Wenyeviti wa Vijiji
& Vitongoji, Watendaji wa Vijiji na Kata, [CBG] kati ya jumla ya Tshs
37,906,700.00 zilizoidhinishwa 2008/2009, kiasi hiki ni asilimia 28%
ukilinganisha na Tshs 5,079,232.00 kati ya Tshs 25,396,160.00 ambacho
kilikuwa 20% ya fedha zilizoidhinishwa
mwaka 2007/2008.
3.3.1 MAENDELEO YA JAMII (JINSIA,
WATOTO NA RUSHWA)
Wilaya
itaendelea kukuza sera ya jinsia na watoto
3. 4 UWEZESHAJI WA WANANCHI KIUCHUMI
MWELEKEO WA BAJETI 2008/2009
Bajeti
kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kiuchumikwa mwaka 2008/2009 katika ngazi ya
Halmashauri ni shilingi 17,752,000/=.
Malengo
Malengo
ya idara ni haya yafuatayo:-
1.
kuendelea
kuwajengea uwezo viongozi wa vijiji ili kutekeleza sera za Maendeleo ya Jamii.
2.
Kuendelea
kuwasaidia watu wanaoishi katika mazingira magumu kwa kushirikiana na mashirika
mbalimbaliyanayotoa misaada kwa makundi hayo.
3.
Kuendelea kutoa
mikopo kwa vikundi ili kuwawezesha kiuchumi na kuongeza kipato chao.
4.
Kuhuisha takwimu
za watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.
5.
Kuratibu
shughuli mbalimbali zinazofanywa na
mashirika yasiyo ya kiserikali ndani ya wilaya
kwa lengo la kupunguza umasikini na kuongeza pato la wananchi.
Tunatarajia
kutekeleza malengo haya ili kuweza kuleta mabadiliko katika jamii kwa
kuwajengea uwezo wa kujitegemea na kujiajiri wenyewe ili kujiongezea kipato na
kuondokana na dhana tegemezi. Hii itasaidia kuondokana na umaskini unaoikabili
jamii.
4.0 HITIMISHO
Hayo
hapo juu ndiyo yaliyofanywa na wilaya katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi
ya mwaka 2005.