MAELEZO KUHUSU
HALMASHAURI YA WILAYA YA ROMBO
UTANGULIZI
Wilaya
ya Rombo ilianzishwa tarehe 1 Julai 1972 kwa kuimega
Wilaya ya Moshi. Wilaya hii ni moja kati ya wilaya sita (6) zinazounda mkoa wa
Kilimanjaro. Wilaya nyingine ni Hai, Siha, Same, Mwanga, Moshi Vijijini , aidha mkoa una manispaa moja.
UTAWALA
Wilaya ina tarafa 5, kata 20, vijiji 60 na vitongoji 295. Baraza la Madiwani linaundwa na madiwani 30 ikiwa ni pamoja na Mbunge wa Jimbo na Mbunge
Viti Maalum. Madiwani 28 ni wa CCM na 2 ni wa CHADEMA.
ENEO NA MIPAKA
Eneo
Ukubwa wa Wilaya ni Kilometa za mraba 1,442 au Hekta 144,200. Eneo kubwa la
mlima Kilimanjaro na vilele vyake viwili (Kibo na Mawenzi) liko ndani ya
Wilaya ya Rombo.
Hk 44,144 zinafaa kwa kilimo; Hk 57 zinafaa kwa
ufugaji; Hk
38,194 ni misitu ya asili na ya kupandwa na Hk 16,692 ni za malisho ya mifugo. Hk 45,113 ni eneo la maji,milima na
miamba.
Mipaka
Wilaya inapakana na nchi
ya
IDADI YA WATU NA MGAWANYO WA
KIUTAWALA
Idadi ya Watu
Idadi ya
watu kwa mwaka 2008, ilikadiriwa kuwa jumla ya watu 267,092
kwa kukokotoa matokeo ya sensa ya kitaifa ya mwaka 2002 ya watu 245,749 na
ongezeko la 1.4% kwa mwaka. Msongamano wa watu kwa kilometa moja ya mraba; ni kati ya watu 200 Ukanda
wa Chini na watu 500 Ukanda wa Juu. Hali
hii imesababisha uhaba mkubwa wa ardhi kwa ajili ya
shughuli za kilimo, ufugaji, ujenzi wa huduma za jamii
Aidha Wilaya ya Rombo ina jumla
ya watumishi wapatao 2,529. Halmashauri ya wilaya watumishi 2,220 na wa Serikali Kuu 309.
MWELEKEO WA HALMASHAURI (DHIMA)
Halmashauri itajiendesha kwa
misingi ya utawala bora ikiwashirikisha wadau wote katika kuleta maendeleo
endelevu ya kiuchumi na ya kijamii kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa njia
endelevu na kwa kuzingatia vipaumbele vinavyopangwa na jamii.
Dira ya
Halmashauri
Kuwa wilaya inayotoa huduma bora na yenye jamii inayojitosheleza kwa mahitaji ya kiuchumi na
kijamii na inayoishi kwa amani na utulivu.
UCHUMI WA HALMASHAURI
Uchumi wa wilaya
unategemea kilimo, ufugaji, mazao ya misitu na madini ya pozollana.
VYANZO VIKUU VYA MAPATO YA
HALMASHAURI
Uendeshaji wa Halmashauri
ya Wilaya ya Rombo unategemea
Mapato
ya vyanzo vya ndani yameongezeka kutoka Tshs. 140,000,000/= mwaka 2004 hadi
shs. 400,000,000/= mwaka 2008.
Ukusanyaji wa mapato ya
halmashauri kwa mwaka 2007/2008 ulikuwa mzuri. Lengo lilikuwa
kukusanya shs. 554,340,416.67. Mpaka mwezi Juni 2008
zilikusanywa shs. 624,371,621.13 sawa na
asilimia 103.25 ya lengo la mwaka.
Mapato ya Serikali Kuu
Makusanyo ya kodi za ndani 2007/2008
yalikuwa Tshs.456,930,659.00 sawa na asilimia 175.
Lengo lilikuwa kukusanya Tshs 261,519,560.00
Makusanyo
ya ushuru wa forodha vituo vya Holili na Tarakea yalikuwa shs.22,106,863,865.70
sawa na asilimia 81.8 ya lengo la kukusanya shs.27,005,000,000.00.
Ufungaji wa
hesabu za Halmashauri umekuwa ukifanyika ndani ya muda uliowekwa kisheria. Taarifa za Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali za halmashauri yetu ni nzuri.
KILIMO NA MIFUGO
Hali ya
hewa
Wilaya haipati mvua za kutosha hivyo hukumbwa na ukame wa mara kwa mara.
Wilaya inazo jumla ya Hk. 281 za umwagiliaji wa mazao mbalimbali
Shughuli
kubwa zinazofanywa na wananchi wa wilaya ya Rombo za
kujipatia kipato ni kilimo, ufugaji, na biashara.
Mipango
iliyopo inalenga katika kuongeza wingi na ubora wa
mazao ya mimea na mifugo.
Kahawa
Zao
kuu la biashara ni kahawa inayolimwa na wakulima
kwenye vishamba vidogo. Tunao wakulima wadogo 30,000 wenye jumla ya hekta 10,000. Lengo ni kila hekta
izalishe kilo 600 ifikapo mwaka 2010; na gharama za uzalishaji ziwe wastani wa
shs. 410,000/- kwa hekta. Mkakati wa kufikia
malengo haya ni kuotesha kahawa chotara (clonal coffee) miche 7,500,000 ifikapo
mwaka 2010. Tunazo
bustani mama 21 zenye miche 7,500 ya kahawa chotara. Bustani hizi zitazalisha miche 525,000 ya
kahawa kwa mwaka.
Wilaya inazo jumla ya Hk. 15,837 za kahawa ambazo
zimepandwa pamoja na migomba. Kwenye mashamba ipo
mibuni ya kahawa 11,315,689, kati ya hiyo asilimia 20 imezeeka sawa na mibuni 2,263,138.
Vimemeanzishwa
vikundi vya
wakulima na tunashirikiana kwa karibu na taasisi za dini kuboresha kilimo cha
kahawa.
Shughuli ya kuiondoa na kuiendeleza mibuni ni
Kung’oa asilimia 10 kwenye Hk 170.
Stumping
asilimia 25 kwenye Hk 383.
Kuendelea
kuotesha asilimia 25 kwenye Hk 791.85.
Kuendeleza
miche michanga asilimia 10 kwenye Hk 1,583.7.
Chakula
Lengo
la kila mwaka ni kuzalisha mazao ya chakula ya kutosha
na ziada kwa biashara. Mazao haya ni ndizi, mahindi, maharage, viazi, mhogo, ulezi, mbaazi na
alizeti. Mahitaji yetu ya chakula kwa mwaka ni tani 38,576 za wanga na tani 19,288 za protini.
Matarajio
ya wilaya ni kupanua kilimo cha matunda, uyoga na
ufugaji wa nyuki ili kuwaongezea wakulima wetu kipato. Uzalishaji wa
kutosha unahitajika ili kuweza kuanzisha viwanda vidogo vya kusindika mazao.
Mwaka
2007/2008 zilivunwa wanga tani 196,685 na protini tani
3,921. Chakula kingi kilizalishwa ukanda
wa juu; ambao wakazi wake wengi walijitosheleza na waliuza
ziada.
Wakulima
wa Ukanda wa Chini wanashauriwa kuzingatia zaidi
kilimo cha mhogo na mbaazi.
Ushirikiano na taasisi za
Tengeru na SUA umewezesha kupanua kilimo cha maparachichi aina ya Alfonso.
Miche 9,000 imeshaoteshwa na yapo matarajio ya
kuongeza miche 3,000 msimu ujao. Msimu huo pia kuna matarajio
ya kuotesha miche 4,000 ya maembe.
Ndizi
Lengo
ni kuongeza uzalishaji hadi tani 236,850 kwa mwaka ili
kuongeza pato la wakulima. Aina ya ndizi
tunazozipa kipaumbele zinazalishwa kwa teknolojia ya
“tissue culture”. Mwaka 2007/2008 hekta 24
zilistawishwa na zilizalisha tani 351 za ndizi.
Vipindi
virefu vya unyaufu na fursa ndogo za kuendesha kilimo
cha umwagiliaji zinadumaza mafanikio ya kilimo hiki. Utaratibu mzuri wa kuwa na soko la uhakika
la ndizi ili wakulima
wapate bei nzuri unahitajika.
Matunda
Lengo
ni kupanua kilimo cha maparachichi aina ya “hass” na
maembe aina ya “alfonso” kwa ajili ya lishe na biashara. Kuotesha miche 20,000 ya maparachichi na 25,000
ya maembe yatakayozalisha tani 4,320 za matunda haya na kuwaingizia wakulima
shs.216,000,000.00 kwa mwaka ifikapo mwaka 2010.
Mifugo
Lengo la Wilaya ni
kuwa na mifugo bora inayotoa nyama, maziwa na mayai kwa wingi. Uzalishaji wa nyama uongezeke kwa mwaka kutoka kilo
1,350,461 za sasa hadi kilo 1,620,553; maziwa yaongezeke kwa mwaka kutoka lita
15,769,976 hadi lita 21,350,121. Mayai yaongezeke kwa mwaka kutoka 21,090,631
hadi 42,181,262;
ifikapo mwaka 2010.
Wilaya ina ng’ombe wa
kisasa 22,636 na ng’ombe wa kienyeji 37,200. Mbuzi wa
kisasa na kienyeji 135,248. Tatizo kubwa
linalowakabili wafugaji ni kupata malisho kwani mifugo hufugwa ndani na ukame wa mara kwa mara unaoathiri malisho ukichangiwa na uhaba
mkubwa wa ardhi.
Zaidi ya asilimia 90 ya Wakazi wa
Wilaya hii ni wafugaji wadogo. Wanyama wanaofugwa ni
Asilimia kubwa ya ng’ombe na
mbuzi wa maziwa hufugwa katika Ukanda wa Juu na Ukanda wa Kati. Hali ya hewa ni nzuri na mchanganyiko wa malisho hupatikana kwa
wingi. Mifugo hii hufugwa ndani na uzalishaji wa maziwa ni wastani wa lita 5 kwa siku.
Ng’ombe wa kienyeji hufugwa kwa wingi Ukanda wa Chini
na hutoa wastani wa lita 2 za maziwa kwa siku.
MALIASILI NA MAZINGIRA
Misitu
Tuna misitu ya aina 3. Msitu wa Lindimaji (
Lengo ni kuotesha miti laini kwa ajili ya mbao na kuzipatia
Halmashauri na Serikali Kuu mapato. Eneo lote la Halmashauri litamalizika kuoteshwa miti mwishoni mwa
mwaka 2009.
Wilaya ina vikundi 22 vya
ufugaji nyuki. Huzalisha asali na nta. Huzalisha kiasi cha kg. 2,000 za asali kwa
mwaka ila lengo ni kufikia hadi kg. 12,000 ifikapo mwaka
2010.
Jumla ya mizinga ni 3,981
na inamilikiwa na vikundi vya kina mama/vijana na watu binafsi.
Hifadhi ya Mazingira
Hifadhi ya
mazingira imegawanyika sehemu tano. Ambazo
ni Hifadhi ya Mlima
Kilimanjaro; Msitu wa Lindimaji (water
catchment forest); Msitu wa Nusu Maili; Mashamba ya Wananchi na machimbo ya
pozollana.
Lengo la wilaya ni kudhibiti
moto kwenye Hifadhi ya Mlima, kuhifadhi Msitu wa Lindimaji, kuotesha miti eneo
lote la Nusu Maili na mashamba ya wananchi.
Kwenye machimbo ya pozollana Kampuni ya
Saruji Tanga ina utaratibu wa kuchimba na kufanya ukarabati wa eneo baada ya
kuchimba.
Vijiji 14 vimeingia mkataba wa usimamizi shirikishi katika kulinda, kutunza na
kuendeleza mazingira. Maeneo
yanayochimbwa mawe, mchanga na morrum yanakarabatiwa
kwa kurudishia udongo na kuotesha miti. Aidha
wananchi wanaoshi karibu na msitu wanashiriki
kuzima moto mara unapotokea ndani ya msitu.
Kazi ya kuimarisha Kamati
za Mazingira za vijiji inaendelea ili zisimamie sheria ndogo za mazingira, na
kudhibiti shughuli za binadamu kwenye maeneo yote ya hifadhi.
Elimu
ya hifadhi ya mazingira inaendelea kutolewa kwa
wananchi katika mikutano ya hadhara kwa kushirikiana na Taasisi zisizo za
Kiserikali
Doria
120 zimefanywa katika misitu na mpakani na nchi jirani
ili kuzuia wanyama waharibifu.
USHIRIKA, VIWANDA NA
BIASHARA
Wilaya
ina Vyama vya Ushirika vya Msingi 16; vya Akiba na Mikopo 16 na Ushirika wa
Viwanda 1. Vina jumla ya wanachama 34,290.
Mikopo yenye thamani ya Tshs. 14.0m ilitolewa kwa SACCOS 7 na SACAS 2.
Wajasiriamali 173 walipata mikopo yenye thamani ya
Tshs. 210,025,000/= kutoka fedha za uwezeshaji wananchi NMB na
CRDB.
Lengo ni
kuhamasisha wanachama wapya na kuongeza akiba, na amana ya vyama hivi. Aidha kuimarisha ukaguzi na
elimu kwa wanachama.
Biashara na
Masoko
Kuwa
na soko la nafaka maeneo ya mpakani Holili na Tarakea;
ifikapo mwaka 2010. Aidha kuvijengea
uwezo vikundi 407 na kuviunganisha na masoko; na kuwa na vituo 5 vya upatikanaji wa taarifa za masoko.
Tumefanikiwa
kujenga soko moja Tarakea na kuvijengea uwezo vikundi 42.
Ukosefu
wa maeneo ya kuanzisha masoko na fedha za kuyajenga vinaviza juhudi hizi.
Utalii
Wilaya ina njia moja ya watalii ya kupanda mlima Kilimanjaro huko
Nalemuru. Shughuli za utalii zinatarajiwa kuongezeka ujenzi wa
barabara kuu kwa kiwango cha lami utakapokamilika.
Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Mamtukuna
kinaendeleza utalii wa utamaduni na mazingira (eco-cultural
tourism) na nchi ya
Viwanda Vidogo
Wilaya ina viwanda vidogo
40 vya kupasua mbao na 3 vya kusindika mafuta. Msukumo mpya umewekwa kwa kushirikiana na SIDO katika kuendeleza viwanda hivi
wilayani. Viwanda hivi vinatarajiwa kusindika mazao ya kilimo na kuendeleza mafunzo kwa vitendo. Fursa zilizopo za
kuliwezesha jambo hili ni pamoja na kuweko kwa umoja
wa mafundi wilayani (Rombo DALTA) na mazao ya kilimo yanayozalishwa.
BARABARA
Wilaya in mtandao wa km.
593 za barabara. Kila kitongoji kinafikiwa kwa gari.
Barabara Kuu ina urefu wa
km. 75. Barabara za Mkoa km.56. Barabara
za wilaya km. 257 na za vijiji km. 205. Barabara kuu
ya Marangu/Kilacha – Kamwanga inajengwa kwa kiwango
cha lami. Wananchi wa vijiji vyote wamejiwekea utaratibu wa kutunza barabara za
vijiji na vitongoji na changamoto kubwa ni jinsi ya kudhibiti
maji ya mvua yanayosababisha uharibifu wa haraka wa barabara hizo.
Ujenzi wa
barabara kuu kwa kiwango cha lami umekamilika sehemu ya kwanza km. 32. Sehemu ya pili km. 33 inaendelea kujengwa na sehemu ya tatu km. 32, iko kwenye maandalizi.
Simu
Huduma za simu zimesambazwa sehemu zote Wilayani. Hizi ni pamoja na simu
za mikononi. Pamoja na huduma za Shirika
la Posta na Simu makampuni mengine ni yale ya Simu za Mikononi likiwemo VODACOM,
TIGO na ZAIN. Ndani ya
wilaya pia kuna Radio Calls.3.
MAJI
Mtandao
wa bomba za maji wilayani una jumla ya urefu wa Km.1,050.
Wilaya
ya Rombo ina vyanzo vya maji 30 vinavyotoa wastani wa
mita za ujazo 20,000 kwa siku. Kiwango
cha huduma kinakadiriwa kufikia kati ya 65% - 70% kwa
nyakati za kawaida. Maji hayo hupungua
nyakati za kiangazi hadi kufikia mita za ujazo 15,000 kwa
siku. Kuanzia mwaka 2001 wafadhili wa GTZ wamesaidia mpango wa kuondoa mabomba ya zamani yenye
kipenyo kidogo na kuweka mabomba mapya yenye kipenyo kikubwa kuanzia chanzo cha
maji huko Marangu. Asilimia 70 ya wakazi
wa Rombo ndio wanapata maji
Katika mwaka 2007/2008 miradi ya maji
yenye thamani ya shs.244,806,000.00 ilijengwa na
kukamilika.
Wilaya inao Mradi wa
ukarabati utakaogharimu Euro 6.4m (Tshs.10.24).
Mradi huu ulitegemewa kumalizika mwishoni mwa mwaka 2008 na ungeongeza meta za ujazo 5,700 kwa siku katika mtandao wa
sasa.
Lengo la Wilaya ni
kuongeza asilimia ya watu wanaopata maji
Tunaendeleza
teknolojia ya kuvuna maji ya mvua na mwaka 2008/2009 yatajengwa
matanki 20 yenye ujazo wa jumla ya lita
100,000 Ukanda wa Chini. Changamoto ni kupata vyanzo
vya kuongeza maji kwenye mtandao wa mabomba tulionao. Changamoto nyingine ni
kutumia maji kutoka Ziwa Challa.
Kamati 53 za maji kati ya kamati 73 zimepewa mafunzo.
ELIMU
Elimu ya Awali
Lengo
ni kuwa na madarasa ya awali katika shule zote za
msingi 156.
Wilaya ina madarasa ya
awali 159. 142 ni
ya serikali. 17 ni ya binafsi.
Elimu ya Msingi
Wilaya ina shule 156 za
msingi (moja ni ya taasisi). Zina jumla ya wanafunzi 67,828.
Wilaya ina mahitaji ya walimu 1,893. waliopo ni
1,501. Upungufu ni
walimu 392 sawa na asilimia 21. Upungufu mwingine ni
madarasa 441, nyumba za walimu 1,650, vyoo (matundu) 11,121, madawati 4,790, meza 740 na kabati 546.
Darasa la IV walifanya mtihani wanafunzi 7,761; wakafaulu 7,465 (96%). Walichaguliwa 7,465
(96%).
Darasa la VII walifanya mtihani 11,887; wakafaulu
7,645 (64%). Walichaguliwa 7,645
(100%).
Watoto 8,322 waliandikishwa darasa la
kwanza mwaka 2008 kati ya waliotazamiwa 7,625.
Hii ni sawa na 109.14%
Msongamano
darasani umepungua,
kiwango cha utoro kimepungua na kiwango cha kufaulu kimepanda
kutoka asilimia 42 hadi 65. Aidha shule zote hutoa chakula
cha mchana.
Elimu ya Sekondari
Wilaya ina shule za
sekondari 47. 40 ni za serikali na 7 ni za taasisi.
Shule 22 ni shule mpya zenye mikondo minne minne.
Kwenye kata nyingine ujenzi umekuwa mgumu kutokana na uhaba wa ardhi hivyo
kulazimika kujenga majengo ya
ghorofa.
Kati
ya shule 47; 34 hazijawa na kidato hadi cha nne. Lengo ni kuendelea
na ujenzi wa madarasa, maabara na nyumba za walimu kwa shule zote mpya.
Vyumba 70 vya madarasa ya
sekondari vimejengwa. Vyumba
8 katika shule za “A” level”.
Shule 5 za kutoa mafunzo ya kidato cha V na VI
zimebainishwa nazo ni: Horombo, Kisale, Makalema, Matolo na Mahida.
Hosteli moja inajengwa sekondari ya Mahida
Elimu ya Watu Wazima
Chini ya Mpango wa MEMKWA
kuna wanafunzi 264 katika vituo 17. Wanafunzi 48 walifaulu kuingia darasa la V
mwaka jana. Mwaka huu watakaofanya mtihani wa darasa la IV ni 181 na la VII ni 83. Vipo
vituo 21 vya MUKEJA vyenye wanafunzi 2,969. Matarajio ni
kuwa mwakani tutakuwa na jumla ya vituo 30.
AFYA
Wilaya ina
hospitali 2, vituo vya afya 5 na zahanati 34.
Hospitali zote 2 zinamilikiwa na Kanisa
Katoliki. Kulingana na
mpango wa Serikali wa kuwa na zahanati kwenye kila kijiji na kituo cha afya
kwenye kila Kata, tumeanza kutekeleza mpango huo kwa kuanza ujenzi wa zahanati
6 na vituo vya afya 2. Upungufu uliopo
ni wa zahanati 16 na vituo
vya afya 15.
Malengo
ya Wilaya ya huduma za afya ni kuimarisha kinga na
tiba dhidi ya malaria; kupunguza vifo vya uzazi na watoto walio chini ya miaka
5, kutokomeza ugonjwa wa vikope, kumaliza tatizo la utapiamlo, kuimarisha afya
ya jamii ya msingi na kuongeza
wanachama wa Bima ya Afya.
Vifo vya watoto
wachanga waliozaliwa hai vimepungua kutoka 39/1000 hadi 10/1000. Vifo vya watoto
chini ya umri wa miaka mitano vimepungua kutoka
21/1000 hadi 5/1000. Vifo
vya uzazi vimepungua kutoka 104/100,000 hadi 84,100,000. Wazazi wanaozalishwa na
wakunga waliopata mafunzo wameongezeka kutoka asilimia 67 hadi 70. Kiwango cha ubora wa vyoo
kimepanda toka 65% hadi 72%. Kiwango cha chanjo kimefikia
90%.
Maambukizi ya malaria yalipungua hadi 20% . Vyandarua 9,000 vyenye viuatilifu viligawanywa
kwa akina mama na 5,000 vilinunuliwa na wananchi wenyewe. Ugonjwa wa vikope umepungua kwa 1%. 99% ya watoto
walio chini ya miaka 5 walipata matone.
Mfuko wa afya unafanya
kazi na hadi sasa una jumla ya wanachama 18,574. Lengo letu ni
kuongeza idadi ya wanachama hadi kufikia 30,000 ifikapo mwaka 2010. Kiasi cha
shs.92,000,000/= zimeshachangwa. Baada ya kupokea
mchango wa serikali mfuko una kiasi cha shs.
187,223,535/=. Wanachama wa Bima ya Afya
wameongezeka hadi kufikia 12,200.
Juhudi za kuhamasisha zinaendelea ili kila kaya iweze kujiunga na kuwa Wanachama wa Mfuko wa
Jamii ili waweze kupata huduma hii ya Afya kwa urahisi.
Tunahakikisha kuwa madawa muhimu
yanapatikana kwenye vituo.
Watumishi
30 wa afya walipewa mafunzo ya utambuzi wa magonjwa ya
moyo.
Ukimwi
Kiwango cha maambukizi kinakadiriwa
kuwa 1.4% Watu 6,500 wanaishi na virusi vya
UKIMWI. Mikakati ya Wilaya ya mapambano
ni uhamasishaji ngazi zote, wenye virusi vya UKIMWI wanaelimishwa umuhimu wa kuhudhuria kliniki kupata dawa na
ushauri nasaha, na mafunzo kwa kamati za kudhibiti UKIMWI ngazi ya kata na
vijiji.
Lengo
letu ni kupunguza maambukizi mapya na kuhamasisha
jamii kupima afya mara kwa mara.
Mafanikio
ni mwitikio mzuri na ushirikiano chanya tunaoupata
kutoka taasisi za dini.
Wadau wanaohusishwa katika kutekeleza azma hii ni
pamoja na KIWAKUKI, KINSHAI, CHAKUWAYA, KIKUURO na RCC.
Mbinu zinazotumiwa na Wilaya
kupambana na UKIMWI
Kuanzisha Kamati
shirikishi za kuthibiti UKIMWI kuanzia ngazi ya Kitongoji, Kijiji na Wilaya.
UKIMWI
umekuwa ajenda ya kudumu kwenye mikutano katika ngazi mbali mbali hapa
Wilayani.
Kuhamasisha na kuimarisha upimaji damu wa hiari na kuendelea kutoa
ushauri nasaha kwa Jamii.
Vituo vya kupima vimeongezeka toka
22 hadi 30.
Idadi ya wanaopima imeongezeka kwa
11%.
Watumishi 12
wamejengewa uwezo wa kutoa dawa za kurefusha maisha.
Vijana
Tuna
vijana takriban 3,400 wasiokuwa na ajira za hakika.
Sensa ya kubaini mahitaji/stadi za
vijana wetu imefanyika.
Wilaya ina
mtandao wa mafundi – ROMBO DALTA wenye mafundi vyuma, useremala, uashi na
cherehani. Aidha kwa ushirikiano na
SIDO, wilaya inajenga
Kombania ya Viwanda (Industrial Cluster) kwa lengo la kusaidia
vijana wetu. Tumeimarisha SACCOS kwa ajili ya vijana kupata mikopo ya biashara na uzalishaji
Lengo
la wilaya ni kuwawezesha vijana hawa waweze kujiajiri
katika kilimo, ushonaji na ufundi.
Tumefanikiwa kuwezesha vijana 48 kufungua
mashamba nje ya Wilaya.
Changamoto
ni kuwawezesha vijana wengi zaidi kufungua mashamba
nje ya Wilaya; na kuwapatia mafunzo ya ufundi wale wenye mwelekeo wa ufundi.
UTAWALA BORA
Wilaya ina
Ofisi ya TAKUKURU inayoratibu na kusimamia mikakati ya kudhibiti rushwa.
Mikakati hiyo ni pamoja na
kuainisha mianya ya rushwa, kuelimisha wananchi kuhusu haki
zao kupitia mijadala ya wazi, semina na
mikutano. Wananchi 1,812 wamepewa elimu hiyo na kutakiwa kutoa ushirikiano
kudhibiti rushwa. Aidha klabu 23 za
wapinga rushwa zimeanzishwa na zinaendelea kwa
kupitia maigizo, nyimbo, ngonjera na
mashairi. Mashindano ya insha
na uchoraji
katuni yanafanyika.
Mpango umeandaliwa wa kuimarisha
utawala bora. Fedha za mishahara ya watumishi kwa kiwango kipya cha mishahara zinalipwa
ili kupunguza vishawishi vya rushwa. Aidha waheshimiwa madiwani wamerekebishiwa viwango vipya vya posho zao.
Fedha za mafunzo ya kuijengea uwezo halmashauri; watumishi
na Waheshimiwa Madiwani zimetengwa.
Vijiji vyote 60 vitanunuliwa shajara kwa ajili ya kuongeza nguvu katika utekelezaji wa kazi za
ofisi za vijiji.
Imefanyika semina kwa watu na Waheshimiwa madiwani kwa kupitia Kamati zote
za halmashauri. Watumishi wote 2,275
wamepata semina kupitia vikao vya kila idara na pia
kwa njia ya vipeperushi na kalenda toka ofisi ya TAKUKURU.
Wenyeviti na wajumbe wa
Serikali za Vijiji wamepewa mafunzo kuhusu vita dhidi ya Rushwa.
Ratiba za vikao kwa mwaka
mzima ziliandaliwa na zinafuatwa kwa ngazi zote.
HALI YA SIASA
Hali ya Wilaya kwa ujumla
ni shwari kwa kipindi cha zaidi ya miezi sita iliyopita. Makosa yaliyoripotiwa
Polisi ni unyanganyi kwa kutumia nguvu, silaha,
kujeruhi.
VYAMA VYA KISIASA VIMEKUWA VIKIJISHUGHULISHA
NA:
Kuhamasisha
wananchi kushiriki katika shughuli za maendeleo.
Kufafanua sera mbalimbali za
Serikali kwa wananchi.
Kutoa hamasa kwa
wananchi kushiriki katika kampeni mbalimbali za kitaifa km. Vita dhidi ya
rushwa, maambukizi ya Ukimwi na shughuli za kujitolea.
UWAJIBIKAJI WA HALMASHAURI KWA
WANANCHI (LLGAS)
Wananchi 87 walipata mkopo wa jumla
shs.59,600,000.00 kupitia benki ya NMB na
wamesharejesha jumla sh.59,915,670 hadi
Julai 2008. Wananchi wengine 86 wamepata
mkopo wa shs.150,425,000.00 kutoka benki ya CRDB
kupitia Saccos za Motamburu na Nanjara Reha.
Nao hawa wamerejesha shs.116,045,054.00 hadi
mwezi Julai 2008.
Mafunzo kwa watendaji wa
kata 20 na VEOS 60 yamefanyika.
Mihtasari ya vikao vya ngazi zote
imekaguliwa.
Mashirika ya dini na
taasisi mbalimbali wameanzisha vituo vya kulelea watoto yatima, mfano: Ngaleku
Orphan Centre na Huruma Tumaini Centre.
Jamii imeelimishwa
kuhusu madawa ya kulevya.
Walemavu wote wanashiriki katika chaguzi za ngazi
zote kuanzia vitongoji, vijiji, kata, wilaya na zile
za Kitaifa.
Vijiji vyote 60 vimeshiriki ujenzi wa shule za sekondari za kutwa hadi kufikia sekondari 34.
Idadi ya walemavu walioko wilayani imebainishwa ili waweze kuingizwa kwenye mpango wa Halmashauri.
Taarifa za mapato ya Halmashauri zinasambazwa
katika ngazi za chini kwa kutumia mbao za matangazo na
kwenye mikutano ya ngazi zote.
Kiasi cha shs. 18,000,000 kimetolewa kwa vijiji 60 kusaidia
shughuli zao za maendeleo.
USHIRIKISHWAJI WA LLGAS KATIKA
KUPANGA MIPANGO (O&OD)
Mafunzo ya O & OD yamefanyika kwa viongozi wa ngazi zote za serikali za mitaa tangu mwaka
2004/05.
Mipango ya miradi ya sekta zote huwa inaandaliwa na Kamati za O&OD zilizoko katika kila kijiji baada ya
kujadiliwa na kikao cha serikali ya kijiji na kisha kufikishwa kwenye kikao cha
WDC kwa kuratibiwa na baada ya hapo kuwasilishwa wilayani.
MIKUTANO
YA KISHERIA KWENYE HALMASHAURI NA LLGAS INAYOPASWA KUFANYIKA
Viongozi katika ngazi za
vijiji na vitongoji wamekuwa wakihimizwa kuitisha na kuhakikisha kwamba vikao
vinafanyika na mikutano mikuu
Viongozi wa halmashauri
hushiriki kikamilifu vikao/mikutano hii ili kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali
yakiwemo yale ya kitaalam na pia kuwaelimisha/kuwafahamisha juu ya haki zao za
kimsingi kisheria, nk.
Utawala Bora
Vikao
vyote vya Halmashauri vimefanyika kulingana na
ratiba. Mikutano ya halmashauri za
Vijiji, Vijiji na Vitongoji inaratibiwa na Wilaya. Vikao vya Halmashauri zinatangazwa na hutumia vipaaza sauti.
Vijiji vina sheria ndogo za kilimo, mazingira na
afya. Masanduku ya maoni yako maeneo
mbalimbali na yanatumika. Mahusiano kati ya viongozi na
watendaji ni mzuri. Aidha mahusiano
baina ya Halmashauri na wadau wengine; mfano; asasi
zisizo za serikali ni mazuri.
Viongozi
ngazi za vijiji walipewa mafunzo kuhusu majukumu na
wajibu wao. Taarifa za mapato na matumizi hutolewa kwenye mikutano ya vijiji. Mwenyekiti wa
halmashauri huwwaeleza wananchi maendeleo na mafanikio ya Halmashauri kila
mwaka.
HITIMISHO
Changamoto Zinazoikabili Wilaya
Kushuka kwa kipato cha wananchi wa wilaya ya
Rombo. Pato la mwananchi wa Rombo linakadiriwa kuwa ni
shs. 250,000/= kwa mwaka (DGDP Survey, 2007). Hii ni sawa na dola za Amerika 167 kwa mwaka. Dola 14 kwa mwezi au dola 0.5 kwa siku.
Zao kuu la biashara linazalishwa chini ya viwango vya kitaalam.Eneo
lilimwalo kahawa lina uwezo wa kuzalisha tani 6,000
kwa mwaka.
Msongamano wa watu ni mkubwa mno unaosababisha
ufinyu wa ardhi kwa ajili ya shughuli za kilimo. Watu
wanalazimika kuzalisha mazao kwenye eneo dogo.
Mahitaji ya shule za sekondari ni makubwa
kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi wanomaliza elimu ya msingi. Tatizo hili
linakuzwa kutokana na uhaba wa maeneo ya kujenga shule
na huduma nyingine za jamii.