SERIKALI mkoani Kilimanjaro, imelitaka kundi kubwa la vijana wenye umri wa miaka 18 na zaidi na wenye kukaribia umri huo kabla ya octoba mwaka huu, kujitokeza kwa wingi katika kuboresha taarifa zao kwenye daftari la kudumu la mpiga kura ili kupata fursa ya kumchagua kiongozi wanaemtaka kwa ustawi na maendeleo ya taifa hili.
Akizungumza mapema Mei 15 katika mkutano wake na wanahabari ofisini kwake, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu amesema zoezi la uboreshaji wa taarifa katika daftari la kudumu litaanza Mei 16 had Mei 22.
Amesema Mkoa wa Kilimanjaro una vituo vya uboreshaji wa daftari hilo 310 vilivyogawanyika katika maeneo mbalimbali Siha 34, Mosh vijijini 64, Hai 31, Mwanaga 24, Manispaa 30, Rombo 56 na Same 71, vituo hivyo vipo ngazi ya kata, ingawa zipo kata nyingine kunavituo zaidi ya kimoja kutoka na ukubwa wa kata na geografia ya eneo.
Aliongezea Mhe.Babu moja ya malengo ya uboreshaji wa daftari hilo ni kutoa nafasi ya kujiandikisha kupiga kura kwa wale wote wenye sifa za kupiga kura ambao hawajajiandikisha kwa sababu mbalimbali, hasa kundi la vijana ili kuweza kupata kiongozi atakayeweza kuleta maendeleo.
Amesema hii ni fursa na haki ya kila mwananchi kuporesha taarifa zake ikiwa alipoteza kitambulisho, kuhama eneo hivyo amewatak kujitokeza.kwa wingi.
"Vijana kura yako ni chanzo cha mabadiliko ya kiuchumu kwa Mkoa na Taifa kwa ujumla, Tume huru ya Uchaguzi, imetoa fursa kwa awamu ya pili kwa wananchi kujitokeze kufanya hivyo,"
17 Barabara ya Florida
Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi
Simu: +255 (027) 2754236/7
Mobile:
Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz
Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa