• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Maazimisho ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Sunday 18th, May 2025
@kijiji cha Mkalama kata ya Rundugai wilayani Hai mkoani Kilimanjaro

MKUU wa mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu amewataka wananchi mkoani humu kuendelea kuuenzi, kuudumisha na kuulinda Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kutowapa nafasi baadhi ya watu wenye chokochoko ya kutaka kutia maneno ya chuki kuhusu Muungano.

Babu alitoa kauli hiyo Aprili 26, 2025 alipokuwa akiwahutubia Wananchi wa kijiji cha Mkalama kata ya Rundugai wilayani Hai mkoani Kilimanjaro ambapo maadhimisho hayo yalifanyika kimkoa kwa kupanda miti 15000 katika eneo la uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) na badae kuzungumza na wananchi.

Alisema kuwa, muungano huo umepelekea Wananchi kutoka Tanzania bara kwenda Zanzibar kifua mbele huku wengine wakitoka Zanzabar kuja Tanzania bara kifua mbele ambalo yote hayo yamechangiwa na uwepo wa muungano huo.

“Watanzania bara wengi wapo Zanzibar wanapata elimu na wapo Wazanzibar wanapata elimu kwenye vyuo vikuu na vyuo vingine kwa uhuru na upendo mkubwa kwa sababu ya tunu ya muungano wetu hivyo Wanakilimanjaro tunawajibu wa kuendelea kuulinda muungano” alisema Babu.

Mkuu huyo wa mkoa alisema kuwa, viongozi wameweza kuwaweka wananchi pamoja na kuhakikisha dosari za muungano zilizokuwa zinasemwa zimetatuliwa ambapo kwa sasa zimebaki tatu ambapo nazo zinafanyiwa kazi.

Alisena kuwa, Watanzania wanayo kazi ya kuendelea kuulinda Muungano na kutowapa nafasi baadhi ya watu wenye chokochoko za kutaka kutia maneno yao ya chuki kuhusu muungano na kuwataka kuulinda kwa nguvu zao zao.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro,  katibu Tawala wa Mkoa, Yusufu Nzowa  amesema tukio hili la Muungano ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha Muungano Kati ya Tanganyika na Zanzibar hivyo wananchi waendelee kuudumisha Kwa kulinda Amani ya nchi yetu.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa