• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

HIFADHI YA KILIMANJARO NI SALAMA KWA MAJIRANI ZAKE

Posted on: August 28th, 2017

Wananchi wanaoishi jirani na Hifadhi ya Taifa ya Kilimanjaro (KINAPA) wamehakikishiwa kuwa hifadhi hiyo ni salama kwa wananchi walioruhusiwa kuingia  ndani ya msitu wa kifadhi kwa aliji ya  kujipatia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuokota kuni na kukata majani kwa ajili ya malisho ya mifugo.

Akijibu hoja za baadhi ya wananchi wa Kijiji cha  Ubetu ambacho ni moja ya vijiji vinavyopakana na hifadhi hiyo wilayani Rombo Kaimu Mkuu wa hifadhi hiyo Charles Ngendo (pichani)  amewahakikishia wananchi hao kuwa hawatopata madhara yoyote endapo wataingia ndani ya hifadhi hiyo bila kukiuka sheria na taratibu za hifadhi.

Aidha Ngendo aliwataka viongozi wa vijiji vinavyozunguka msitu wa hifadhi watumie kamati za mazingira  za vijiji husika kuratibu namna ya kusimamia wanawake wanaoingia hifadhini kutafuta mahitaji  waingie kwa usalama bila ya kupata bughudha yoyote.

Kuhusu utaratibu wa kuruhusu wanawake pekee kuingia ndani ya hifadhi Ngendo alisema huo ni utaratibu uliowekwa baada ya kufikiwa maamuzi ya kulinda hifadhi yalifanywa na Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Maendeleo ya Mkoa (RCC) hivyo  hauwezi kukiukwa.

Awali mwananchi wa kijiji cha Ubetu  aliyejitambulisha kwa jina la Mama Silayo amedai kuwa  baadhi ya wanawake  wamekuwa wakichapwa kwa fimbo  na baadhi askari wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro wanapokutwa ndani ya hifadhi wakiokota kuni.

Ngendo alimtaka  Mama silayo awasilishe malalamiko pamoja  na ushahidi  katika utaratibu rasmi ikiwa ni pamoja na kuonana na uongozi wa hifadhi mapema iwezekanavyo ili uongozi huo uweze kuchukua hatua kwa mtumishi aliyetenda kitendo hicho.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro amewataka wanawake wanaongia ndani ya hifadhi  kuwa waaminifu na waadilifu wapoingia ndani hifadhi kwa kuhakikisha kuwa hawavunji sheria na kanuni za hifadhi.

Kuhusu utoaji wa taarifa amewataka watoe taarifa sahihi na si za kudanganya ili kuisaidia serikali kutenda haki.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa