• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

IDADI YA VIFO VYA AJALI YA MOTO SAME YAFIKIA 42

Posted on: July 2nd, 2025

Idadi ya watu waliopoteza maisha katika ajali ya mabasi mawili kugongana na baadaye kushika moto wilayani Same, mkoani Kilimanjaro, imeongezeka na kufikia 42, kutoka 39 vilivyoripotiwa awali.


Akizungumza na waandishi wa habari Jumatano, Julai 2, 2025, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, amesema kuwa kati ya waliopoteza maisha, 31 walikuwa wakisafiri katika basi dogo aina ya Coaster, huku wengine 11 wakiwa kwenye basi kubwa.


Kuhusu hali ya majeruhi, mkuu huyo wa mkoa amesema jumla ya watu 24 waliokuwa wamelazwa tayari wameruhusiwa kurudi nyumbani baada ya hali zao kuimarika, huku majeruhi wawili wakiendelea kupokea matibabu hospitalini.



Aidha, Mhe. Babu amesema Mkoa tayari umeshapokea majibu ya vipimo vya vinasaba kutoka kwa mkemia Mkuu wa Serikali mapema leo tarehe 02 Julai 2025, hivyo zoezi la kukabidhi miili ya marehemu kwa ndugu na jamaa litafanyika siku ya Alhamisi tarehe 03 Julai 2025 katika hospitali ya Rufaa ya KCMC. Ambapo Serikali inatarajia kukabidhi jumla ya miili 36 kwa wanafamilia husika ili kuweza kuendelea na taratibu za mazishi. Gharama za majeneza, Sanda na kusafirisha miili ya marehemu zitagharamiwa na Serikali kwa kutoa kiasi cha fedha kwa kila familia ili kufanikisha mazishi ya wenzetu hao.

Aidha maziko ya miili sita (6) ya wenzetu ambao wao walitambulika kirahisi na kutohitaji DNA yalifanyika tarehe 30 Juni, 2025.

Amesema katika ajali hiyo hadi kufikia leo jumla ya watanzania wenzetu 42 wamefariki ambapo 31 (ikiwa ni wanawake 21 na wanaume 10) walikuwa kwenye coaster na 11 (ikiwa ni wanawake 7 na wanaume 4) walikuwa kwenye basi la channel one.  Aidha, majeruhi waliopatikana katika ajali hii ni 28 ambapo kati yao 13 ni wanaume na wanawake 15. Majeruhi wote hao waliendelea kupata matibabu katika Hospitali zetu ikiwa ni pamoja na hospitali ya Wilaya ya Same, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi pamoja na Hospitali ya Rufaa ya Kanda (KCMC) ambapo kati ya majeruhi hao, majeruhi 24 wameruhusiwa, wawili (2) wameaga dunia wakati katikati ya matibabu na wawili (2) waliobaki wanaendelea na matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda (KCMC) na Hospitali ya Wilaya ya Same.


mnamo tarehe 28 Juni, 2025 majira ya saa 11 jioni, mkoa wetu ulipata tukio la ajali mbaya ya barabarani katika eneo la Saba Saba, Kitongoji cha Mahuu, Kata ya Same takriban kilomita 4 kutoka Same Mjini, Wilaya ya Same – Mkoa wa Kilimanjaro ikihusisha basi kubwa la abiria lenye usajili wa namba T-179 la Kampuni ya Channel One lililokuwa likitokea Arusha kuelekea Tanga na Coaster ya abiria yenye namba za usajili T-199 EFX inayomilikiwa na kampuni ya MWAMI TRANS iliyokuwa ikitokea Same kuelekea Manispaa ya Moshi.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • SERIKALI KUBORESHWA HUDUMA ZA AFYA ROMBO

    July 02, 2025
  • IDADI YA VIFO VYA AJALI YA MOTO SAME YAFIKIA 42

    July 02, 2025
  • VIJANA WILAYANI ROMBO WAMEHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

    July 02, 2025
  • MIUNDOMBINU YA ELIMU YAZIDI KUIMARIKA KWA WANANCHI WA KWAKTAU, ROMBO.

    July 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa