• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

JITOKEZENI KUBORESHA TAARIFA ZENU KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA

Posted on: December 11th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Nurdin Babu, Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Kiseo Nzowa pamoja na viongozi wengine wameshiriki zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika Kata ya Kilimanjaro Manispaa ya Moshi ambapo zoezi hilo limeanza rasmi Disemba 11 hadi 17, 2024 Mkoani hapa.

Mhe.Nurdin Babu ametoa pongezi kwa Tume Huru ya Uchaguzi kwa kazi nzuri ambayo wameanza kufanya katika Mkoa wa Kilimanjaro na kusema kuwa Mkoa wa Kilimanjaro ni miongoni mwa Mikoa ambayo imeanza kufanya uboreshaji wa daftari la mpiga kura kwa mwaka huu wa 2024, aidha amesema zoezi hili la uboreshaji wa taarifa ni muhimu sana kwa wananchi wote na Watanzania kwa ujumla.

“Ndugu wananchi zoezi hili la uboreshwaji wa taarifa ni la muhimu sana katika nchi yetu kwahiyo leo mimi pamoja na viongozi wenzangu na nyinyi wananchi tumejitokeza kwa wingi kuja kuboresha taarifa zetu”

Aidha ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro kujitokeza kufanya maboresho ya taarifa zao ili ifikapo Oktoba 2025 waweze kupiga kura kuwachagua viongozi wanaowataka.

“Nipende kutoa wito kwa wananchi wa Mkoa huu mjitokeze kwa wingi kuboresha taarifa zenu ili ifikapo uchaguzi Mkuu 2025 muwe na kibali na haki ya kupiga kura na kuwachagua viongozi wa nchi yetu pia kwa wale ambao wanakaribia kufikisha umri wa miaka 18 wafike kwenye vituo ili wapewe maelekezo na viongozi wa Tume Huru ya uchaguzi ili na wao waweze kujiandikisha” Amesema Babu

 Hata hivyo Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Bi.Mwajuma Nasombe ametaja makundi yanayotakiwa kwenda kufanya uboreshaji wa taarifa zao, ambao ni wale watakao timiza umri wa miaka 18 kabla ya tarehe ya uchaguzi Mkuu  2025 ,wale waliojiandikisha awali na kuama Kata au Jimbo kwenda maeneo mengine, wale wenye taarifa zilizokosewa wakati wa uandikishaji hapo awali na wale waliopoteza kadi zao ya kupiga kura au wenye kadi zilizo aribika.

Kwa upande wake Mratibu wa uandikishaji Mkoa Bw. Jasper Ijiko amesema kuwa “tumejipanga vema kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa na jambo kubwa la mahususi kwa kushirikiana na Tume Huru ya Uchaguzi ni kuendelea kutangaza na kuhabarisha wananchi wale wote wenye sifa tunatarajia wananchi wote hadi kukaribia tarehe 17 Disemba 2024 watakuwa wamejiandikisha katika vituo vipatavyo 1300 katika Mkoa wetu wa Kilimanjaro.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO ASISITIZA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANANCHI WILAYANI HAI

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA SIHA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI BORA WA MAPATO

    June 17, 2025
  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa