• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Kilimanjaro

Posted on: March 5th, 2025

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro imetoa Msaada kwa Wanawake Waliojifungua na Watoto Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi,ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani,Machi 8,Mwaka huu.


Akikabidhi msaada huo, Mkuu wa Mkoa Nurdin Babu amesema kwamba msaada huu ni ishara ya upendo na kujali kwa wanawake hao na watoto wao, akisisitiza kuwa ni muhimu kuwaunga mkono katika nyanja mbalimbali za maisha, hasa katika kipindi hiki cha maadhimisho ya wanawake.


Kwa upande wake, kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Mawenzi, Jonas Kessy, amesema kuwa vifaa walivyokabidhiwa vitasaidia kuboresha huduma kwa wanawake na watoto wao. Kessy alieleza kuwa hospitali hiyo itahakikisha vifaa hivyo vitatumika ipasavyo ili kusaidia katika maendeleo ya wamama na watoto hao.


Miongoni mwa misaada iliyotolewa ni pamoja na taulo za kike, sabuni za kufulia, na pampasi, vifaa ambavyo vinatarajiwa kuboresha huduma za afya kwa wanawake na watoto katika hospitali hiyo.


Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ameshiriki pia katika zoezi la upandaji miti katika Shule ya Msingi Mshikamano, iliyopo kata ya Boma Mbuzi, Manispaa ya Moshi. Zoezi hili ni sehemu ya juhudi za kuhamasisha utunzaji wa mazingira na kuwajengea jamii dhamira ya kupenda mazingira.


Huu ni mfano mwingine wa juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro katika kuhakikisha maendeleo ya jamii na mazingira yanapewa kipaumbele.


Hadi kufikia tarehe 8 Machi, mwaka huu, maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yanaendelea, huku wanawake na watoto wakikumbukwa na kutolewa msaada mbalimbali ili kuboresha hali zao.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa