• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MAZAO YA CHAKULA YASISAFIRISHWE NJE YA NCHI

Posted on: June 26th, 2017

Serikali hapa nchini imepiga marufuku uuzaji na usafirishaji wa mazao ya nafaka katika  nje ya nchi bila kuwa na kibali cha serikali  na kuagiza kamati za mikoa kusimamia kikamilifu agizo hilo .

Marufuku hiyo imetangazwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muuungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kasim majaliwa alipokuwa akiwahutubia waumini wa dini ya kiislam na wananchi kwa ujumlakwenye baraza la Iidd lilifanyika kitaifa mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro ambapo alilakwa kama mgeni rasmi katika ibada hiyo.

Waziri Mkuu majaliwa amesema serikali imechukua hatua hiyo ili kuliepusha taifa na upungufu wa chakula kutokana na mahitaji makubwa ya chakula waliyonayo wananchi kabla ya chakula kusafirishwa kwenda nchi jirani.

Aidha Waziri Mkuu Majaliwa amewataka wakulima na wafanyabiashara wa mazao ya nafaka kuomba vibali vya kusafirisha nje ya nchi bidhaa ambazo zimeshaongezwa thamani ili waweze kupata faida zaidi.

Akitoa mfano wa zao la mahindi Mhe. Waziri Mkuu Majaliwa amefafanua kuwa nivema wafanyabiashara wakasafirisha unga wa mahindi baadala ya kusafirisha mahindi ghafi kwani kwa kufanya hivyo wanapoteza faida katika biashara hiyo na kuhamishia nje ya nchi fursa za ajira kwa watanzani.

Mhe majaliwa alitoa mfano wa maroli kumi na moja   yanayoshikiliwa na jeshi lapolisi Mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kujaribu kusafirisha mahindi nje ya nchi amesema iwe mwisho kwani mtu au kikundi chochote kitakachojihusishs na usafirishaji wa mazo ya nafaka nje ya nchi kinyume na sheria mazao hayo pamoja na vyombo vya usafiri vitakavyotumika vitaaifishwa.

Kuhusu vita dhidi ya dawa za kulevya Mhe. Waziri Mkuu amesema serikali inatambua na kuthamini  ushirikiano unaotolewa na Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) pamoja na madhehebu ya mengine ya dini katika kuunga mkono juhudi za seriali kwenye vita dhidi ya dawa za kulevya.

Kuhusu  viashiria vya uvunjifu amani katika baadhi ya maeneo hapa nchini ikiwemo wilaya za Kibiti na Rufiji mkoani Pwani, Mhe. Majaliwa amesema serikali inaendelea kuwasaka, kuwakamata na kuwapeleleza wahusika wote wa vitendo hivyo na watakapoabainika kuhusika watafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Awali akiwasilisha taarifa ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA), Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza hilo Sheikh  Salum Abeid amesema waislamu nchini wanaunga mkoano juhudi za serikali ya wamu ya tano katika vita dhidi ufisadi na ubadhirifu wa mali za umma.

Sheikh Salum Abeid amesema waislamu wanatambua na kuthamini nia njema ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli za kuzirejesha mali zote za baraza hilo zilizoporwa kinyemela na watu wachache kwa njia za kuwarubuni baadhi ya viongozi wa baraza hilo.

Kwa upande wake Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania amewataka waislamu nchini na wananchi wote kuwa na mienendo mema ili amani iliyopo nchini iendelee kudumu.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO ASISITIZA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANANCHI WILAYANI HAI

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA SIHA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI BORA WA MAPATO

    June 17, 2025
  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa