• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MEI MOSI

Posted on: May 1st, 2023

Sekta binafsi Mkoani Kilimanjaro zimeelekezwa kuendelea kuboresha maslahi ya wafanyakazi pamoja na kuweka mikakati bora ya namna ya kutatua changamoto za waajiriwa wao kwa wakati ili kuondoa migogoro isiyo ya lazima ambayo hupunguza ufanisi wa kazi na kurudisha nyuma maendeleo.

Hayo yamesemwa leo Mei 1, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu katika siku ya Wafanyakazi Duniani ambapo Kimkoa yameadhimishwa katika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika na kuhudhuriwa na taasisi mbalimbali za serikali na binafsi.

Mhe. Babu amewaelekeza Viongozi wa Vyama vya wafanyakazi kuendelea kuwatembelea na kufanya vikao kazi na wanachama wao katika maeneo yao ya kazi ili kujua changamoto wanazokabiliwa nazo na kuzitatua kwa wakati.

Aidha, uongozi wa Serikali ya Mkoa inaenda kushughulikia changamoto wanayokutana nayo wafanyakazi ya kutokupewa ushirikiano mzuri katika ofisi ya kazi mkoa pindi wanapopeleka malalamiko yao ya mfanyakazi mmoja mmoja au kupitia chama cha wafanyakazi.

Hata hivyo Mhe. Babu ameendelea kukemea suala la mmomonyoko wa maadili unaoendelea kwa sasa katika jamii zetu kwa ukatili na ulawiti unaofanywa kwa watoto na vitendo vya mapenzi ya jinsia moja na kusema kila mmoja anajukumu la kukemea na kuchukua hatua katika kutoa elimu.

Mratibu wa TUKTA Bw. Kanuti Magashi  akisoma risala kwa mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amesema kuna baadhi ya taasisi binafsi wamekua wakitoa mikataba yamuda mfupi katika kazi ambazo ni endelevu jambo ambalo limefanya wafanyakazi kutochangai katika mifuko ya hifadhi ya jamii hii inapelekea maumivu kwa watumishi hao mara wanapofika ukomo wakazi au kupatwa na majanga kazini na kutokwenda kazini.

Aidha, Bw. Kanuti ameomba kama itawezekana suala la kikokotoo liangaliwe tena kwa mtumishi kwani bado linawaumiza ikiwezekana mara baada ya kustaafu mtumishi apewe mafao yake yote.

Hata hivyo ametoa shukrani kwa taasisi mbalimbali ambazo zimekua mstari wa mbele katika kushughulikia changamoto za wafanyakazi ndani ya mkoa.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa