• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RAS Ataka Misaada Iwafikie Walengwa Kwa Wakati

Posted on: April 29th, 2020

Wakurugenzi  Watendaji wa halmashauri zilizopatwa na athari za mafuriko mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuwafikishia misaada ya kibinadamu wananchi wote waliokumbwa na athari za mafuriko kwa haaraka na uadilifu.

Akiongea kwa nyakati tofauti akiwa kwenye vijiji vilivyoathirika na mafuriko katika wilaya za Moshi, Siha, Hai na Mwanga, Katibu Tawala wa Mkoa  wa kilimanjaro Dkt. Khatibu Kazungu amewaagiza wakurugenzi wote kuhakikisha wanaifikisha misaada hiyo kwa walengwa na kwa wakati bila kuchelewa .

Aidha Dkt. Kazungu amezitaka halmashauri hizo kuendelea kukusanya taarifa zikiwemo takwimu sahihi za uharibifu wa mali za wananchi zikiwemo nyumba, akiba za vya kula pamoja na idadi ya heka  za mashamba zilizoharibiwa na mafuriko zikiwa na mazao.

Dkt. Kazungu alifanya ziara katika vijiji vyote vilivyoathirika na mafuriko katika wilaya za Mwanga,Moshi,Hai na Siha ili kuwapa pole wananchi waliopatwa na maafa hayo pamoja na kujionea madhara yaliyosababishwa na mafuriko kwa wananchi.

Dkt. Kazungu amewahakikishia wananchi wote waliopatwa na athari za mafuriko kuwa watulivu kwani serikali yao ipo pamoja nao na kuwathibitishia kuwa itahakikisha kila kaya iliyokumbwa na athari za mafuriko itapatiwa misaada ya kibinadamu itakayokidhi mahitaji muhimu ya kiutu.

Mvua zinazoendelea kunyesha katika mkoa wa Kilimanjaro zimeleta madhara katika ambapo kaya zaidi ya elfu moja zimekosa makazi huku zaidi ya ekari elfu moja zilizokuwa na mazao zikiharibiwa kabisa.

Wadau kadhaa wa maendeleo wameshatoa misaada mbalimbali ya kibinadamu kwa waathirika na kumkabidhi Katibu Tawala wa Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna Mghwira.Misaada iliyotolewa ni pamoja na vyakula, magodoro na vyandarua.

Katibu Tawala wa Mkoa ameshaikabidhi  misaada hiyo kwa wakurugenzi watendaji wa halmashauri zilizokumbwa na mafuriko na kuwaagiza waifikishe kwa waathirika wa mafuriko mapema iwezekanavyo.




Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa