• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC Ataka Weledi Uandishaji Darasa la Kwanza na Awali

Posted on: January 13th, 2022

Halmashauri mkoani Kilimanjaro zimehimizwa kusimamia kwa weledi zoezi la uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali, darasa la kwanza na mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa shule za sekondari.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha tarehe 13.01.2022 kilichojumuisha viongozi wa Chama, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi pamoja na Makatibu Tawala Wilaya, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Stephen Kagaigai ameyasema zoezi hili ni muhimu kwa ustawi wa taifa hivyo lisimamawe kwa umakini.

Aidha, Mhe. Kagaigai amesema kwa mwaka 2022 wanafunzi wapya wa awali walioandikishwa hadi sasa kufikia 15,135 ambapo jumla ya wavulana ni 7,559 na wasichana 7,576 sawa na silimia 50 ya maoteo ya kuandikisha Watoto 30,47. Kwa upande wa elimu ya msingi darasa la kwanza  jumla ya wanafunzi walioandikishwa hadi sasa ni 17,525 ambapo wavulana 8,747 na wasichana 8,778 sawa na asilimia 58 ya lengo la uandikishaji ambapo maoteo ni kuandikishwa wanafunzi 30,039.

Kwa upande wa elimu ya sekondari jumla ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ni 30,710 ambapo wavulana 15,011 na wasichana 15,699.  Amesema ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha wanafunzi waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza wanaripoti shuleni mapema ili kuendelea na masomo yao kwa wakati. Hata hivyo ameendelea kuweka msisitizo kwa wazazi na walezi kuhakikisha wanafunzi wote waliotimizia umri wa kuanza shule za awali na darasa la kwanza kwa muhula wa masomo 2022 kuhakikisha waandikishwa bila kisingizio chochote maana elimu hii haina malipo ya ada.

‘‘ ni jukumu letu sote kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza wanaripoti shuleni mapema kwa kuzingatia muda ili waweze kuendelea na masomo yao pamoja na kuhakikisha tunaweka msisitizo kwa wazazi na walezi kuandikisha wanafunzi wote waliotimiza umri wa kuanza shule za awali na darasa la kwanza kwa muhula wa masomo mwaka 2022’’.

Mbali na maelekezo hayo Mhe. Kagaigai ametoa shukrani zake za kipekee kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada za kuboresha miundombinu ya Elimu kupitia fedha za UVIKO-19. Ambapo kwa sekta ya elimu pekee mkoani Kilimanjaro ilifanikiwa kupata jumla ya shilingi Bilioni sita na milioni arobaini (6,040,000,000/=) kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 276, vituo shikizi 18 na mabweni 2.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa