• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC BABU AWAAGIZA VIONGOZI WA HALMSHAURI KUTUNZA BARABARA

Posted on: December 13th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amewataka Wakurugenzi, Wenyeviti wa Halmashauri, Meya, Wakuu wa Wilaya zote sita kuhakikisha barabara zote zisizo chini ya TARURA na TANROADS kuhakikisha zinafanyiwa marekebisho na kupitika muda wote katika mwaka.

Ameyasema hayo Disemba 13,2024 katika kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro ambapo alisema barabara zote lazima zijengwe na kukarabatiwa kurahisisha mambo ya kiuchumi.

Amesema "Niwaagize na kuwasisitiza Wakurugenzi wa Malaka za Serikali za Mitaa katika Mkoa huo na viongozi wengine wa ngazi mbalimbali katika wilaya, barabara zote ambazo hazihudumiwi na wakala wa barabara TANROADS na TARURA ni wajibu wao kuzifanyia marekebisho na kuweka taa za barabarani kwani huchangia asilimia kumi ya pato, "

Amesema lengo kuu la Serikali ya Awamu ya Sita ni kuhakikisha kuwa miundombinu ya Barabara inakuwa rafiki yaani zinapitika majira yote na hivyo kuwawezesha wananchi kufika kwa wakati maeneo yote na kujiongezea kipato katika shughuli za kiuchumi.

Amesema licha ya Serikali kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ukarabati wa barabara, kumekuwa na uharibifu mkubwa wa miundombinu kama vile uvamizi wa hifadhi ya barabara, wizi na uharibifu wa taa za barabarani kinyume na sheria za barabara.

"Kumekuwa na ucheleweshaji wa kuchukuwa hatua za kisheria , hivyo naelekeza kuwa Wakuu wa Wilaya , Meya, Wenyeviti wa Halmashauri na Mamlaka za Kisheria wakishirikiana na TANROADS na TARURA kulinda miundombinu na watakaokaidi wachukuliwe hatua mara moja,"amesema Babu.

Amesema Mkoa utaendelea na utaratibu wa kufanya ukaguzi wa matengenezo ya barabara   lengo ni kuhakikisha barabara zote zimejengwa katika viwango vilivyokabaliwa.

Kwa upande wake Katibu Tawala Mkoa Kilimanjaro, Yusufu Nzowa alisema barabara ni moyo wa uchumi hapa nchini hivyo ni wajibu wa kila aliyepewa dhamana kuhakikisha anatekeleza wajibu wake.

Amesema watakuwa wakali kwa wakandarasi wazembe, wanaofanya kazi chini ya kiwango na wanaochelewesha kazi hizo.

"Wananchi wetu wanategemea barabara hizi katika kufanya shughuli za kiuchumi, huu ni moyo wa Uchumi wetu. Tunataka kazi zinazofanyika zionyeshe thamani ya pesa zinazotolewa,"Amesema Nzowa.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa