• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC KAGAIGAI: HALMASHAURI TOENI 10% KWA WAKATI

Posted on: June 25th, 2021

Halmashauri Mkoani Kilimanjaro zimetakiwa kuhakikisha zinatenga  asilimia 10 kwa wakati kutoka kwenye mapato ya ndani  kwa ajili ya  Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu.

Aliyasema  hayo wilayani Rombo  Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Stephen  Kagaigai katika kikao cha Baraza Maalum la Madiwani  cha kujadili  Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

Alisema ni wajibu wa kila halmashauri kufuata kanuni  namba 5.5(1)ya Sera ya Mikopo kwa vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu iliyofanyiwa mabadiliko mwaka 2019 lengo likiwa ni kusaidia ukuzwaji wa  mwananchi mmoja moja na taifa kwa ujumla.

"Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassani anamatamanio makubwa sana ya nchi  hii kusonga mbele, lakini haiwezi kusonga mbele bila kufanya kazi, hivyo naagiza fedha hizo  zitolewe ili kwenda kuinua wananchi kiuchumi hasa yale makundi yaliyoelekezwa, Vijana, Wanawake na  Watu wenye Ulemavu''.

Wakati huo  huo Mhe. Kagaigai aliwataka wananchi wa mkoani hapa,   kuchukua taadhari dhidi ya ugonjwa wa Corona (COVID -1 9) huku akisema ni wajibu wa kila mmoja kwa mujibu wa taratibu za Wizara ya Afya.

Alisema kuwa  ugonjwa huu upo lakini haipaswi kuchukuliwa kwa hofu bali ni kwa taadhari kama yalivyo magonjwa ya malaria kwa  kuweka  chandarua .

"Ugonjwa huu upo na ningependa wananchi tuendeleze  utamaduni wetu tuliokuwa tunaufanya awali wa kunawa mikono mara kwa mara, kupaka vitakasa mikono  na kuvaa barakoa pale mnapokuwa kwenye mikusanyiko, na uzingatie umbali wa kutosha   kwa mujibu wa Wizara ya Afya".

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Rombo Kanali Hamis Maiga akiwa kwenye Baraza Maalum la Madiwani Wilayani humo aliwataka madiwani kuongeza ushirikiano na watendaji ili waweze kupata matokeo bora katika halmashauri hiyo.

Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Serikali za Mitaa Grace Makiluli, amewataka Watendaji kuhakikisha wanazingatia na kutekeleza hoja zote zinazotolewa na Mkaguzi  ili waweze kubaki na hati safi.





Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa