• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC KILIMANJARO ATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTII SHERIA NA KANUNI ZA KAZI ILI KUONGEZA KAZINI

Posted on: May 1st, 2025

RC KILIMANJARO ATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTII SHERIA NA KANUNI ZA KAZI


Serikali katika Mkoa wa Kilimanjaro imewataka watumishi wa umma kuendelea kutii sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika maeneo yao ya kazi, ili kuongeza ufanisi katika kuwatumikia wananchi.


Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mheshimiwa Nurdin Babu, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi), yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi tarehe 1 Mei, 2025. Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Babu alieleza kuwa baadhi ya watumishi wamekuwa na tabia zisizofaa kazini, ikiwemo kuchelewa kazini, kutoroka bila ruhusa na matumizi ya vileo, akiwataka waache mara moja na wajikite kutimiza majukumu yao kwa weledi na uadilifu.


"Baadhi ya wafanyakazi hawafanyi kazi ipasavyo. Unakuta saa tisa na dakika 28 tayari mtu anaondoka, anataka saa tisa na nusu awe ameshatoka getini. Huu sio utaratibu mzuri wa kuwatumikia wananchi," alisema Mhe. Babu.


Katika hatua nyingine, RC Babu aliwataka waajiri wote mkoani hapa kuacha mara moja vitendo vya unyanyasaji kwa watumishi, ikiwemo kuwapa majukumu nje ya muda wa kazi bila malipo na kuwazuia kuunda au kujiunga na vyama vya wafanyakazi.


Aidha, aliwapongeza viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Mkoa wa Kilimanjaro kwa kuendelea kusimamia maslahi ya watumishi katika nyanja mbalimbali.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Kiseo Nzowa, aliwataka watumishi wote wa umma kufanya kazi kwa juhudi, maarifa na uadilifu ili waache alama nzuri zitakazowakumbusha pale watakapomaliza muda wao wa utumishi.


Naye Katibu wa TUCTA Mkoa wa Kilimanjaro Ndg.Jackson Nyanganilwa alipongeza serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali watumishi na kutatua changamoto zao kwa wakati.


Maadhimisho hayo yaliambatana na kauli mbiu isemayo: "Uchaguzi wa Mwaka 2025 Utuletee Viongozi Wanaojali na Kuthamini Maslahi ya Wafanyakazi," ambapo pia watumishi hodari kutoka taasisi mbalimbali mkoani Kilimanjaro walitunukiwa zawadi kwa kutambua mchango wao katika utumishi bora.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • RC KILIMANJARO ATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTII SHERIA NA KANUNI ZA KAZI ILI KUONGEZA KAZINI

    May 01, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Kiseo Nzowa, akihutubia wananchi na viongozi mbalimbali katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.

    May 01, 2025
  • MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO ATOA SIKU 14

    April 26, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa