• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

TAASISI LINDENI MAENEO YENU

Posted on: February 23rd, 2022

Taasisi zote za Umma zilizopo Mkoani Kilimanjaro zimeelekezwa kulinda maeneo yao ili kuruhusu zoezi la anuwani za makazi kufanyika kwa urahisi.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Stephen Kagaigai ametoa maelekezo hayo februari 22, 2022 wakati wa uzinduzi wa anuwani za makazi lililofanyika katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa na kuzindua  anuwani  katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, na kuweka  kibao cha anuwani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi  Moshi, sheli ya PUMA na nyumba 2 za makazi za wananchi wa  Manispaa ya Moshi.

Mhe. Kagaigai amesema watendaji wa taasisi wanatakiwa  kuwa makini kwenye kulinda maeneo yao  wanayoyamiliki kihalali ili kufanya uwekaji wa anuwani za makazi kufanyika kwa wepesi na hivyo itapelekea kuepusha migogoro ya ardhi na wananchi.

Ameendelea kusema baadhi ya taasisi zimekua zikiingia kwenye migogoro ya ardhi na wananchi ambao wamekuwa wakivamia maeneo yao na wengine kupelekea kujenga nyumba za kudumu.  

Aidha, Katibu Tawala Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Willy Machumu amesema Wakuu wa Taasisi watapelekewa sampuli za anuwani za makazi zenye maelekezo husika katika ofisi zao wakati huo watumishi wa Manispaa ya Moshi wanaofanya zoezi hilo la uwekaji wa anuwani wataweka alama kwa kutumia chaki huku mchakato wa vibao vyenye ubora na viwango vilivyopangwa ukiendelea kuandaliwa kwa ajili ya kubadikwa.

Akiwasilisha taarifa ya uzinduzi wa anuwani za makazi Mratibu wa zoezi hilo Mkoa Bw. Richard Emily amesema zoezi hili limetokana na changamoto zilizojitokeza katika Posta na anuwani za makazi ambapo masanduku ya posta yako 143,000/= nchi nzima ambayo ni  idadi ndogo ukulinganisha na idadi ya wananchi kwa sasa. Amesema anuwani za makazi zinaundwa na vitu vitatu ambavyo ni namba ya nyumba au jengo, jina la barabara au mtaa na namba ya posti codi. Post codi ni namba maalumu inayotambulisha kanda,mkoa,wilaya na Kata.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Same Edward Mpogolo aliyeshika nafasi ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi amesema wilaya zinaendelea na zoezi la uwekaji wa anuwani za makazi ambapo wanaendelea kutoa ushirikiano wakutosha  na kusimamia kwa weledi zoezi hilo pia kutumia muda uliopangwa kuhakikisha zoezi linakamilika kwa wakati.




Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa