• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UHAMASISHAJI WA MATUMIZI YA MATOKEO YA SENSA 2022

Posted on: October 2nd, 2023

Viongozi wa Mkoa wa Kilimanjaro wamehimizwa kutumia matokeo ya Sensa ya mwaka 2022 kuwaletea wananchi maendeleo endelevu.

Wito huu umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Kasilda Mgeni aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu wakati wa ufunguzi wa Semina ya Usambazaji na Uhamasishaji wa Matumizi ya Matokeo ya Sensa kwa Viongozi, Watendaji na Wadau wa Mkoa wa Kilimanjaro iliyofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa CCP Oktoba 2,2023.

Mhe. Kasilda amesema mipango ya maendeleo izingatie matokeo ya Sensa na mwenendo wa kasi ya ongezeko la idadi ya watu katika mkoa wa Kilimanjaro hasa katika utoaji wa huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo Elimu,Afya,Maji,na barabara.

 “Sisi kama mkoa wa Kilimanjaro tumeshaanza kutumia matokeo ya Sensa 2022 katika kupanga miradi ya maendeleo kwa wananchi wetu” amesema Mhe. Kasilda.

Ameongeza kuwa, semina hii itawajengea uwezo viongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kutumia matokeo ya Sensa kwa ajili ya kupanga mipango ya maendeleo ya wananchi katika ngazi zote za utawala.

Kwa upande wake Mtakwimu Mkuu wa Serikali Dkt. Albina Chuwa amesema Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) imejipanga kuhakikisha matokeo ya Sensa 2022 yanawafikia wadau wote katika Nyanja mbalimbali ili yaweze kutumika katika kupanga na kufuatilia utekelezaji wa mipango ya maendeleo.

Dkt. Chuwa amesema, NBS inaendelea kuchakata matokeo ya Sensa 2022 ili kutoa takwimu nyingi zaidi zitakazokidhi mahitaji ya Serikali na wadau wa maendeleo.

“Ofisi ya Taifa ya Takwimu inaendelea kuyasambaza matokeo ya Sensa kwa wadau wote ili yatumike kuwaletea wananchi maendeleo. Leo hii tupo hapa Kilimanjaro ili viongozi wa Kilimanjaro, wadau na wananchi wajue takwimu za mkoa wao na wazitumie kujiletea maendeleo” amesema Dkt. Chuwa.

Naye Kamisaa wa Sensa Mhe. Anne Makinda amesema Sensa 2022 imefanyika kwa mafanikio makubwa na sasa ni wakati wa kufaidika na matunda ya Sensa kwa kuyatumia matokeo hayo kuleta maendeleo.

Aidha, amesema watanzania aslimia 99.99 walihesabiwa na kufanya Sensa 2022 kuwa ya kihistoria na iliyopata uungwaji mkono mkubwa na wanachi na wadau wote ndani na nje ya nchi.  

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Tixon Nzunda amesema atahakikisha mipango yote ya Mkoa na bajeti inayokwenda kupangwa kwa mwaka wa fedha ujao itazingatia takwimu halisi za Sensa ya mwaka 2022 katika maeneo yote ya halmashauri saba za Mkoa kwa kuxingatia mipango ya fursa na maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro.


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa