• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Uhamisho wa Wakuu wa Shule Unalenga Kuboresha Utendaji - Dkt. Mghwira

Posted on: April 21st, 2020

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna Mghwira amesema uhamisho wa aliyekuwa Mkuu wa Shule ya Sekondari Lyamungo, Mwalimu Adrian Maro  ulilenga kuimarisha utendaji na uwajibikaji katika kusimamia elimu katika na si vinginevyo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Dkt. Mghwira amesma  uhamisho huo uliotekelezwa na Katibu Tawalawa wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Khatib Kazungu ulizingatia mapendekezo ya tume iliyochunguza malalamiko kutoka kwa baadhi ya waalimu wa shule ya sekondari Lyamungo dhidi ya Mwalimu Adrian Maro  .

Miongoni mwa mambo yaliyobainika baada ya uchunguzi wa tume hiyo ni pamoja na uwezo mzuri wa mwalimu Maro katika kusimamia shule ya sekondari Kimochi ya kutwa yenye kidato cha kwanza hadi cha nne jambo ambalo lilipelekea wasimamizi wake wa kazi kumbadlishia majukumu na kumpa kazi ya kusimamia shule ya  sekondari Lyamungo ambayo ni ya bweni  yenye kidato cha tano na sita.

Aidha Mhe Mghwira alibainisha kuwa tume imegundua uwezo mdogo wa kiutendaji wa Mwalimu Maro katika kusimamia shule ya bweni nyenye kidato cha tano na cha sita hali iliyosababisha wasimimizi wake wa kazi kumpungizia ukubwa wa kazi kwa kumpa usimamizi wa shule ya kutwa kama ya awali.

Ameongeza kuwa miongoni mwa mambo ambayo yameonesha udhaifu wa kiutendaji kwa Mwalimu Maro ni kufanya teuzi bila kufuata taratibu na miongozo na kutowapa barua waalimu ambao amewateua kwa kuwapa majuku.

Mbali na hilo Mhe. Dkt, Mghwira amesema Mwalimu Maro alishindwa kudhibiti jaribio la mgomo wa wanafunzi lililotokea tarehe 24/02/2020 jambo ambalo ni ishara ya kutomudu nidhamu kwa waanafunzi.

Kuhusu fedha za ukarabati wa shule kongwe unaotekelezwa na serikali ya awamu ya tano, Mhe. Dkt. Mghwira amesema shule ya sekondari Lyamungo si shule pekee iliyopata fedha za utekelezaji wa miradi hiyo katika mkoa wa Kilimanjaro, hivyo basi si sahihi kuhusisha uhamisho wa mkuu wa shule na kuletwa fedha za utekelezaji wa mradi huo.

Amebanisha kuwa tangu mwaka 2017 halmashauri za mkoa wa Kilimanjaro zimekua zikipokea fedha za kukarabati wa shule kongwe ndani ya mkoa.

Mhe. Dkt. Mghwira amefafanua kwamba Halmashauri ya wilaya  Same imepokea kiasi cha milioni 91,6927,960 kwa ajili ya ukarabati wa shule ya sekondari Same,

Katika Manispaa ya Moshi  shule ya ufundi moshi imepokea Shilingi  bilion 2.8 na shule ya sekondari Mawenzi imepokea shilingi milioni 750,332,637. Katika halmashauri ya Moshi shule ya sekondari Langasani ilipokea shilingi milioni 121,600,000, shule ya sekondari Umbwe imepokea shilingi milioni 969,669,148 , shule ya sekondari Ashira imepokea shilingi milioni 851,955,447.50 na shule ya sekondari Weruweru imepokea shilingi milioni 749,179,604.

Katika Halmashauri ya wilaya ya Hai shule ya sekondari Lyamungo  imepokea kiasi cha shilingi milioni 799,443,156 kwa ajili ya ukarabati wa shule hiyo.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ameeleza kuwa muongozo wa matumizi ya fedha hizo uatolewa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ( TAMISEMI ) ambao unatakiwa kusimamiwa na mamlaka zote katika usimamizi wa fedha.






Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa