• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UPANDAJI MITI

Posted on: April 25th, 2023

Taasisi Mkoani Kilimanjaro zikiwemo TANROADS, TARURA, TFS na zingine zimeelekezwa kuuga mkono juhudi za kubadilisha Mkoa kuwa wa kijani kwa kupanda miti kando kando ya barabara na maeneo mengine. Amezitaka taasisi hizo kupanda miti mchanganyiko ikiwemo ya matunda.


Maelekezo hayo yametolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu kwenye uzinduzi wa upandaji miti zaidi ya 1000 uliofanyika katika chanzo cha maji cha Miwaleni Kata ya Kahe Wilayani Moshi Aprili 25,2023 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa mwaka huu yamebeba kauli mbiu isemayo MIAKA 59 YA MUUNGANO, ”UMOJA NA MSHIKAMANO NDIYO NGUZO YA KUKUZA UCHUMI WETU.


Mhe. Babu ametoa wito kwa viongozi na watumishi wote wa Mkoa kuhakikisha kuwa miti iliyopandwa na itakayoendelea kupandwa inatunzwa na kuelekeza kila familia kupanda na kutunza angalau miti mitano (5) kila mwaka kulingana na ukubwa wa eneo ili kurejesha Kilimanjaro ya kijani kama ilivyokuwa hapo awali hii ni kutokana na uharibifu mkubwa wa mazingira unaofanyika katika Mkoa wetu jambo linalopelekea mabadiliko ya tabia nchi na kukauka kwa vyanzo vya maji, mvua kuchelewa kunyesha na wakati mwingine kunyesha mvua kidogo hali inayopelekea kuwa na  uhaba wa chakula katika maeneo mengi ya Mkoa wetu na nchi yetu kwa ujumla.


Aidha, Mhe. Babu amesema Muungano wetu umedumu kutokana na mizizi yake kujikita kwa wadau wakuu wa Muungano ambao ni wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, umakini na usikivu wa viongozi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kufuatilia kwa karibu changamoto zinazojitokeza na kuzipatia ufumbuzi umekuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha Muungano. Ameendelea kusema utamaduni uliowekwa na viongozi wetu wakuu wa nchi wa kuwa na vikao vya pamoja vya kujadili na kuzipatia ufumbuzi changamoto zinazojitokeza kwa kuzingatia misingi ya umoja, haki, usawa  na mshikamano, umeimarisha na kudumisha Muungano kwa kiasi kikubwa.


Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilmanjaro Bw. Tixon Nzunda amesema katika kampeni hii ya kurudisha outo wa asili wa Mkoa wa Kilimanjaro utunzaji wa mazingira utaanzia kwenye ngazi ya Kaya, Kitongoji, Kijiji, Kata, Halmashauri na ngazi ya Mkoa.

Nzunda ameendelea kusema kunahaja ya kuwajengea wananchi uwezo na wadau wa ndani ya mkoa kuona umuhimu wa utunzaji wa mazingira kwa faida za vizazi vya sasa na vya baadaye, vile vile kujenga mwitikio kwa wadau kupenda, kuthamini, kupanda, kutunza na kuendeleza kazi ya utunzaji wa mazingira.


Akiwasilisha taarifa ya Wilaya Afisa Maliasili na Mazingira Wilaya ya Moshi Bw Inno Paul amesema takwimu za mwaka 2023 zinaonyesha kuwa jumla ya miche ya miti  25,150 imepandwa katika msimu wa vuli kwa kushirikiana na wadau wa mazingira.

Bw.Paul amesema halmashauri imeanza kutekeleza mfumo wa Masijala ya Miti(Tree Registry System) ambapo katika mfumo huo miti yote itakayopandwa itasajiliwa kwa kuchukuliwa taarifa muhimu ambazo ni pamoja na namba ya mti, aina ya mti, data za majira ya nukta, mahali, na afya ya mti. Amesema faida ya mfumo huu ni kuchukua taarifa za maendeleo ya miti iliyopandwa mwaka hadi mwaka itasaidia kuongeza ufanisi wa miti iliyopandwa.





















Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa