• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE KILIMANJARO

Posted on: January 7th, 2024

Mkoa wa Kilimanjaro umepewa heshima kubwa na Serikali ya Awamu sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2024. Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika tarehe 02 April, 2024 katika Uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika, Moshi (MoCU) uliopo katika Manispaa ya Moshi. Aidha, baada ya uzinduzi huu Mwenge wa Uhuru utakimbizwa katika Halmashauri zote Saba (07) ndani ya Mkoa kuanzia tarehe 02/04/2024 hadi tarehe tarehe 08/04/2024.


Pamoja na ujumbe na maudhui muhimu ya mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2024. Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu zinaenda sanjari na kumbukizi ya matukio adhimu  katika Taifa letu ambayo ni;

Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kuunda taifa la Tanzania,

Miaka 60 tangu kuanzishwa kwa Mbio za Mwenge wa Uhuru ambapo zilianza rasmi mwaka 1964, sambamba na;

Miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Aidha, mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 zinaadhimisha kumbukizi ya miaka 25 ya kifo cha muasisi wa Taifa letu Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.



Mwaka huu ujumbe wa Mwenge wa Uhuru utahusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uhifadhi wa Mazingira chini ya Kaulimbiu isemayo, “Tunza mazingira na Shiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa ujenzi wa Taifa Endelevu’’.


Aidha, pamoja na ujumbe huu mkuu zipo jumbe za kudumu ambazo zinawekewa mkazo kila mwaka na mwenge wa Uhuru kuhusu: -


•Mapambano dhidi VVU/UKIMWI, chini ya kauli mbiu isemayo; “Jamii iongoze kutokomeza UKIMWI”.


•Mapambano dhidi ya Malaria, chini ya kauli mbiu; “Ziro Malaria Inaanza na Mimi - Nachukua hatua kuitokomeza”.


•Mapambano dhidi ya dawa za kulevya, chini ya kauli mbiu isemayo; “Zingatia Utu; boresha huduma za Tiba na Kinga”.


•Mapambano dhidi ya rushwa, chini ya kauli mbiu isemayo; “Kuzuia Rushwa ni Jukumu lako na Langu; Tutimize Wajibu Wetu”.


•Uzingatiaji wa Lishe Bora, chini ya kauli mbiu isemayo; “Lishe sio kujaza Tumbo; Zingatia unachokula”.



Ratiba ya Mbio za Mwenge wa Uhuru ndani ya Mkoa;

Baada ya uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa katika viwanja vya Chuo cha Ushirika Moshi, Mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 zitafanyika Kimkoa kwa kila Halmashauri kwa ratiba ifuatayo:-


-Tarehe 02/04/2024 – Wilaya ya Moshi- Manispaa ya Moshi


-Tarehe 03/04/2024 – Utakuwa Wilaya ya Moshi - Halmashauri wa               Moshi

-Tarehe 04/04/2024 – Utakuwa Wilaya ya Hai


-Tarehe 05/04/2024 – Utakuwa Wilaya ya Siha


-Tarehe 06/04/2024 – Utakuwa Wilaya ya Rombo


-Tarehe 07/04/2024 – Utakuwa Wilaya ya Mwanga


-Tarehe 08/04/2024 – Utakuwa Wilaya ya Same.



Baada ya uzinduzi wa Mwenge wa Uhuru halmashauri ya Manispaa ya Moshi itakua ya kwanza kati ya halmshauri  zote 195 za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupokea na kukimbiza Mwenge wa uhuru tarehe 02/4/2024 hivyo wananchi wote wa Mji wa Moshi na Viunga vyake mnaombwa kujitokeza kwa wingi kwenye uzinduzi pamoja na kwenye maeneo yote ya miradi itakayopitiwa na Mwenge pamoja na kushiriki katika mkesha wa Mwenge.


Aidha, Tarehe 09/04/2022 – Tutakabidhi Mwenge wa uhuru kwa wenzetu wa Mkoa wa Tanga katika Kijiji cha Bendera, Kata ya Bendera Wilayani Same kuanzia saa 12:00 asubuhi hivyo wananchi wa Wilaya ya Same tunahamashishwa kiujitokeza kwa wingi  kukabidhi Mwenge wa Uhuru.


Kwa upande wa Vyombo vyote vya habari ikiwa televisheni, Redio, magazeti pamoja na mitandao ya kijamii tushirikiane kuhamasisha wananchi juu tukio hili kubwa katika Mkoa wetu,


Tunafahamu Serikali inatambua uwepo wa vipaji mbalimbali katika mkoa wetu hivyo tunawahamasisha kutumia fursa hii kuonyesha vipaji vyao na kuvitumia kuhamasisha wananchi kujitokeza na kushiriki katika uzinduzi wa mwenge.


Hata hivyo kama tulivyosema tukio hili la kitaifa ni kubwa tunatarajia kupokea wageni wengi kutoka maeneo mbalimbali katika nchi yetu hivyo ni wakati wetu mzuri wa kutumia fursa hii vizuri katika kuongeza pato letu huku tukiwahudumia wageni wetu kwa ukarimu, uaminifu na uchangamfu kama ilivyotabia wa Wanakilimanjaro.


Shime wamiliki na watoa huduma mbalimbali kama huduma za malazi na chakula, huduma usafiri n.k kujipanga vizuri kwa kuboresha huduma hizo.


Kama ilivyodesturi ya wanakilimanjaro juu ya suala zima la usafi na utunzaji wa mazingira nachukua fursa hii kuwakumbusha tuendelee kudumisha suala zima la usafi katika makazi yetu, maeneo ya biashara, mitaa na maeneo ya wazi ya kijamii. Aidha, mitaro na barabara zetu ziwe safi wakati wote na tuepuke utupaji wa taka ovyo. Hata hivyo kwakua ni msimu wa masika  nawakumbusha kupanda miti katika maeneo yetu kuihudumia na kuitunza.



Sisi Mkoa wa Kilimanjaro tunasema Mwenge umerudi nyumbani ikiwa na maana kwamba mwaka 1964 Mwenge wa Uhuru ulipandishwa katika kilele cha Mlima Kilimanjaro hivyo tunaona fahari miaka 60 baadaye mwenge wa uhuru umerudi kuzinduliwa Mkoani Kilimanjaro ndoamana tunasema Mwenge wa Uhuru umerudi nyumbani.


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa