• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

VIJANA WILAYANI ROMBO WAMEHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

Posted on: July 2nd, 2025

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2025, Ndg. Ismail Ussi, ametoa wito kwa  vijana wa Wilaya ya Rombo na maeneo mengine nchini kuchangamkia mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu inayotolewa na Serikali kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmshauri kwa lengo kajiinua kiuchumi.

Ndg. Ussi ametoa  wito huo leo Julai 2,2025 wakati alipotembelea na kukagua kikundi cha Vijana Mapambano Mafundi uliopo Tarafa ya Mkuu – Ushiri  wanaojihusisha na utengenezaji wa samani mbalimbali kama vile meza, viti, makabati, fremu na madirisha.


“Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeweka mkazo mkubwa katika kuwawezesha wananchi kiuchumi. Halmashauri zote nchini zimeelekezwa kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani ili kuwawezesha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Ni jukumu la vijana kuchangamkia fursa hizi kwa kuunda vikundi na kuandika miradi ya maana,” alisema Ndg. Ussi.


Akiwa katika eneo la mradi huo, amepongeza  ubunifu wa vijana wa Mapambano Ufundi kwa kutumia mikopo hiyo kujiajiri na kuajiri wenzao kupitia utengenezaji wa bidhaa za mbao ambapo ni hatua ambayo inachangia kupunguza tatizo la ajira na kuongeza kipato kwa vijana wa eneo hilo.

Akisoma taarifa Mwenyekiti wa kikundi hicho Nicky Gabriel Mng’anya amesema kikundi kilianza rasmi mwaka 2024 kikiwa na vijana 5 na kupatiwa mkopo wa milioni 20 kwa ajili ya kuendeleza shughuli yao na kimefanikiwa kwa kupata kandarasi ndogo ndogo kutoka kwa wananchi.

Bw. Nicky ameishukuru Halmashauri kwa kuwapatia mkopo huo usio na riba, na kuahidi kuutumia vizuri kwa kuendeleza shughuli zao za uzalishaji mali, huku wakitoa wito kwa vijana wengine kujitokeza kuchangamkia fursa hizo badala ya kukaa bila kazi.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • SERIKALI KUBORESHWA HUDUMA ZA AFYA ROMBO

    July 02, 2025
  • IDADI YA VIFO VYA AJALI YA MOTO SAME YAFIKIA 42

    July 02, 2025
  • VIJANA WILAYANI ROMBO WAMEHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

    July 02, 2025
  • MIUNDOMBINU YA ELIMU YAZIDI KUIMARIKA KWA WANANCHI WA KWAKTAU, ROMBO.

    July 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa