• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Wanaume wamfurahisha RC Mghwira Upimaji VVU

Posted on: September 13th, 2018

Wanaume  Mkoani Kilimanjaro wamepongezwa kwa kuitikia wito wa  kampeni ya Furaha Yangu na kujitokeza kwa wingi katika kampeni ya upimaji wa virusi vya UKIMWI.

Pongezi hizo zimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira wakati wa kuzindua rasmi kampeni hiyo kimkoa ulifanyika katika viwanja vya Shree Hindu Mandal mjini Moshi.

Mhe. Mghwira amesema kuwa kumekuwa na tafsiri potofu kwa wanaume wengi kutegemea majibu ya vipimo vya afya za wenzi wao kuyachukulia kama ndiyo hali zao jambo ambalo amesema kiafya ni hatari kwa ustawi wa mtu binafsi, familia na taifa kwa ujumla.

Ili kuunga mkono juhudi za serikali na wadau wote wa afya katika vita dhidi ya virusi vya UKIMWI na UKIMWI, Mhe. Mghwira amesema kila mtu anawajibu wa kupima afya yake ili aweze kujitambua na hatimaye aweze kuishi akiwa anaijua hali yake ya maambukizi.

Aidha Mhe. Mghwira amewataka wananchi wote kujitokeza kwa wingi katika zoezi la upimaji lilioanza tarehe 10/09/2018 na kuishia tarehe 16/09/2018.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa kampeni hiyo kwa kipindi cha siku tatu kuanzia tarehe 10/09/2018 hadi tarehe 13/09/2018, mratibu wa masuala ya UKIMWI katika mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Eligy Mosile amesema jumla ya watu  1369   wamejitokeza kupima virusi vya UKIMWI ambapo kati yao wanaume kakiwa 905 sawa na asilimia 66 na wanawake 464    sawa na asilimia 34.

Katika taarifa hiyo Dkt. Mosile amesema watu11sawa na silimia 0.8 wamegundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya UKIMWI ambapo kati yao wanaume walikuwa 6 sawa na asilimia 0.7 na wanawake 5 sawa na asilimia 1.1

Uzinduzi wa kampeni ya Furaha Yangu, Pima, Jitambue, Ishi kimkoa  ni mwendelezo wa kampeni iliyozinduliwa rasmi na Mhe. Kassim Majaliwa Waziri, Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa