• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

WAZIRI MKUU AMUWAKILISHA RAIS SAMIA, AHIMIZA JAMII KUZINGATIA MISINGI YA MAADILI

Posted on: July 13th, 2025

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ametoa wito kwa viongozi wa madhehebu ya dini nchini kuendelea kuihimiza jamii kuzingatia msingi ya maadili na kuepuka mienendo iliyo kinyume na tamaduni, mila na desturi ya Mtanzania, 

Amesema kuwa moja ya eneo ambalo viongozi hao wanapaswa kukemea ni kuhusu  matumizi, biashara na usambazaji wa dawa za kulevya kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kunusuru maisha ya Watanzania hususan vijana.

Amesema hayo leo (Jumapili, Julai 13, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ibada ya kumweka wakfu na kumuingiza kazini Askofu Mteule Dkt. Daniel Henry Mono wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mwanga, mkoani Kilimanjaro.

“Tuendelee kupambana vikali na matumizi ya dawa za kulevya sababu athari yake ni kubwa hasa kwa vijana wetu, vijana ni kundi tegemewa, matumizi ya dawa za kulevya yanaharibu uelewa na afya za vijana wetu”

Mheshimiwa Majaliwa amesema Serikali kwa upande wake imeendelea kuweka sheria kali pamoja na kuimarisha ukaguzi wa kubaini uingizaji wa dawa za kulevya nchini. “Tupo imara usikubali kushiriki katika biashara hii”.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa ameyapongeza madhehebu ya dini ikiwemo Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika kuihudumia jamii ya Watanzania.

“Serikali itaendelea kushirikiana na madhehebu ya dini katika kufanikisha masuala mbalimbali yanayounganisha Taifa letu ikiwemo Agenda za kitaifa, kuimarisha masuala ya maadili na kujenga jamii inayozingatia misingi ya kudumisha upendo, amani na utulivu”

Ameongeza kuwa madhehebu hayo yamekuwa yakitoa mchango mkubwa katika kutoa huduma za afya, elimu, malezi ya vijana, utunzaji wa mazingira pamoja na huduma kwa makundi maalum yenye uhitaji ikiwa ni kuinga mkono Serikali katika kutoa huduma.


Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali wakati wote itaendelea kufanya kazi na kushirikiana na madhehebu ya dini nchini kwa ajili ya manufaa ya watanzania wote.

Pia, Waziri Mkuu amesema Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia itaendelea kufanya kazi usiku na mchana ili kuimarisha ustawi wa wananchi katika nyanja zote za utoaji huduma pamoja na kusimamia uwepo wa Amani na Utulivu katika jamii.

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 488 kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya nia nne kuanzia Mailisita, Kiboriloni hadi Holili.


Mheshimiwa Majaliwa amepongeza Baba Askofu Mteule Dkt. Mono kwa kupewa nafasi ya kuiongoza Dayosisi ya Mwanga ambapo amesema uteuzi wake ni ishara kuwa amekidhi vigezo na kustahili kupewa daraja hili kubwa katika jamii.

“Ninakupongeza sana kwa kuwa umethibitika mbele ya Mungu na wanadamu, nafasi ya Askofu ni kubwa kwenye kanisa kwa kuwa askofu ni msimamizi wa kanisa. Kwa maneno mengine wewe ndiye kiongozi wa kiroho wa washarika wote wa Mwanga, hili ni jukumu kubwa sana ambalo unapaswa kulitekeleza kwa hekima kuu”.

Naye Askofu Mteule Dkt. Daniel Henry Mono ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kuliombea Taifa hasa katika kipindi cha kuendelea uchaguzi mkuu utakaofanyika Mwezi Oktoba 2025 ili haki na amani viweze kudumua na mapenzi ya Mungu yaweze kutimia kwa kupata viongozi watakaoongoza kwa maslahi ya Taifa zima.

Ameongeza kuwa Dayosisi hiyo itaendelea kushirkiana na Serikali kama mdau mkubwa na mshirika wa karibu wa kanisa bila kuathiri misingi ya imani na kanisa.


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • WAZIRI MKUU AMUWAKILISHA RAIS SAMIA, AHIMIZA JAMII KUZINGATIA MISINGI YA MAADILI

    July 13, 2025
  • MHE BABU AKIUKABIDHI MWENGE WA UHURU 2025 MKOANI ARUSHA

    July 05, 2025
  • UPANUZI WA SKIMU YA MAJI YA LAWATE (GARARAGUA - KIDICO) KUNUFAISHA WANANCHI ZAIDI YA 7,000 WILAYANI SIHA.

    July 03, 2025
  • SERIKALI KUBORESHWA HUDUMA ZA AFYA ROMBO

    July 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa