Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2025, Bw. Ismail Ussi, ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa soko jipya la Mbuyuni lililopo katika Manispaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. Ujenzi wa soko hilo umegharimu kiasi cha shilingi bilioni zaidi ya bilioni 2 na unatarajiwa kuboresha mazingira ya biashara wa Manispaa na maeneo ya jirani.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Bw. Ussi amepongeza juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kusikiliza na kutatua changamoto za wananchi, hususan wafanyabiashara waliopoteza maeneo yao ya kufanyia biashara baada ya soko la awali kuteketea kwa moto.
Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa Soko hilo Afisa Biashara wa Manispaa ya Moshi Bw.Prosper Msele amesema ujenzi mradi huo umegharimu zaidi shilingi bilioni 2 ambapo ujenzi huo unatekelezwa kwa awamu mbili.
Aidha, wafanyabiashara wa soko hilo wameeleza kufarijika na hatua hiyo ya ujenzi mpya, wakimshukuru Rais Dkt. Samia kwa kusikia kilio chao na kuchukua hatua za haraka kuhakikisha wanarejea katika shughuli zao katika mazingira bora na salama.
Soko hilo linatarajiwa kuwa na miundombinu ya kisasa, ikiwa ni pamoja na vizimba vya biashara, vyoo vya kisasa, sehemu ya kuhifadhia mizigo na maeneo ya huduma za kijamii, hivyo kuongeza tija katika sekta ya biashara ndani ya Manispaa ya Moshi.
17 Barabara ya Florida
Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi
Simu: +255 (027) 2754236/7
Mobile:
Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz
Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa