Mkoa wa Kilimanjaro umepokea Mwenge wa Uhuru leo Juni 28,2025 Kutoka Mkoa wa Kaskazini Pemba katika uwanja wa ndege wa Moshi Manispaa ya Moshi ambapo utapata fursa ya kupitia jumla ya miradi 52 ambayo inapatikana katika Halmashauri zote saba za Mkoa. Katika miradi hiyo; 20 ni ya kuwekewa Mawe ya Msingi, Miradi 22 ni ya Kuzinduliwa, Miradi 10 ni ya Kutembelewa yenye thamani ya bilioni 84.
Akisoma taarifa ya Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amesema Mwenge wa uhuru utapata fursa ya kuona na kutembelea juhudi mbalimbali zinazofanywa na vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye walemavu katika kuzalisha mali ili waweze kujiendeleza kiuchumi, uhamasishaji wa matumizi safi na salama ya nishati mbadala na pia utazindua klabu za kupambana na Rushwa shuleni.
Hata hivyo, Miradi yote ya Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2025 imegusa sekta zote zikiwemo, Afya miradi 8, Barabara na madaraja miradi 7, Elimu miradi 11, Maji miradi 7, Nishati salama miradi 3, Vijana Miradi 7 na miradi ya kijamii 9.
Mhe. Babu amesema kuwa, Mwenge wa Uhuru utakapokuwa unakimbizwa hapa Mkoani utaendelea kuimarisha umoja na mshikamano miongoni mwa Wanakilimanjaro kwa maslahi mapana wa maendeleo ya Mkoa na Taifa letu kwa ujumla.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe. Salama Mubaruku Khatib amesema viongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa walifanya kazi kubwa ya kuweka mawe ya msingi, kuzindua na kutembelea miradi ya maendeleo pia walishiriki katika zoezi la ugawaji la mitungi ya gesi 100
17 Barabara ya Florida
Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi
Simu: +255 (027) 2754236/7
Mobile:
Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz
Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa