• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MAFUNZO YA AWALI YA UCHUNGUZI KWA MAAFISA UCHUNGUZI WAPYA TAKUKURU

Posted on: May 15th, 2023

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene ameushauri uongozi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini TAKUKURU kuanza utaratibu wa kutoa mafunzo ya teknolojia ya habari na mawasiliano kwa watumishi wake ili kuwajengea uwezo zaidi wakati wa kutekeleza majukumu yao.


Mhe. Simbachawene alitoa ushauri huo Mei 15, 2023  Mkoani Kilimanjaro wakati akifungua mafunzo ya awali ya uchunguzi kwa waajiriwa wapya wa TAKUKURU yanayofanyika kati Shule ya Polisi Tanzania (TPS).


"Watumishi wa TAKUKURU wanafanyakazi ya kuchunguza maswala mbalimbali yanayohusiana na maendeleo; kwa sasa kuna wale ambao wanatumia teknolojia ya kisasa kufanya uhalifu ikiwemo ubadhirifu wa fedha hivyo kwa kupata mafunzo haya mtakuwa mmewaongezea uwezo katika kutekeleza majukumu yao", alisema.


Aliongeza, "Ni vyema somo la elimu ya IT likafanywa la lazima kwa kila anaeajiriwa na taasisi hii kwani uhalifu wa kimtandao haswa ule ambao TAKUKURU hutumia kukabiliana nao hufanywa kwa kupitia mitandao; mtumishi hawezei kufanya uchunguzi wa uhalifu wa aina hii bila kuwa utalaam wa IT".


Aidha, alitoa rai kwa uongozi wa TAKUKURU kuendelea kushirikiana na taasisi zingine likiwemo Jeshi la Polisi katika kupambana na rushwa hapa nchini haswa ikitiliwa maanani ya kuwa mpaka mtu afikirie kutumia rushwa huwa tayari ashafanya njama nyingi.


Mhe. Simbachawene aliendelea kusema kuwa Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wake kwa taasisi hiyo ili kuhakikisha inafanikiwa katika kutekeleza majukumu yake kwa manufaa ya Taifa haswa ikitiliwa maanani Serikali imekuwa ikipeleka fedha nyingi kwa ajili ya shughuli za kimaendeleo na ambazo ni lazima matumizi yake yaonekane yanaenda na fedha halisi.


Akiongea katika hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Rashid Salum Hamdun, alisema Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa na inaendelea kutoa ushirikiano mkubwa kwa taasisi hiyo katika kutekeleza majukumu yake.


"Kwa mfano ndani ya kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais Dr Samia, Serikali imetoa kibali cha kuajiri jumla ya watumishi wapya 700 ambao ni sawa na robo ya watumishi wote ambao wamejiriwa na taasisi hii tangu inanzishwe mwaka wa 1975 wakati huo ikijulikana kama PCB", alisema na kuongeza, huu ni mchango mkubwa sana kwa PCCB katika kutekeleza majukumu yake.


Kuhusu mafunzo hayo, ACP Hamdun alisema kuwa ambao kabla ya kuteuliwa kwao kujiunga na taasisi hiyo kulifanyika vetting ya hali ya juu.


"Zilipotangazwa nafasi hizi, uongozi wa taasisi ulipokea maombi takribani 33,000 na baada ya usahili walipatikana 320 ambao ndiyo wanaanza mafunzo yao leo", alisema.


Alisema mafunzo hayo ni ya lazima kwa kila mtumishi aneajriwa na taasisi hiyo, ambapo alisema wahusika hao watapata mafunzo ya kinadharia na vitendo, ambayo alisema yatahusisha pamoja na elimu nyingine, ile ya uchunguzi wa jinsi ya kutambua na kupambana na vitendo vya rushwa.


Awali Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babau aliwaasa wahusika wa mafunzo hayo kuhakikisha wanaweka uzalendo mbele wakati wakitimiza wajibu wao kwa manufaa ya Taifa na wananchi wake.


"Uzalendo ndiyo silaha ya kwanza na muhimu kabisa katika mapambano dhidi ya rushwa; Tanzania itapata maendeleo ya kweli na kuendelea kupata heshima duniani kote iwapo mtazingatia uzalendo wakati wakutekeleza majukumu yenu haswa katika kufuatilia miradi ya kimaendeleo inayotekelezwa na fedha nyingi zinazotolewa na Serikali yetu", alisema.





Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA CHANGAMKIENI FURSA ZA MKOPO WA SERIKALI

    June 29, 2025
  • WEKEZENI KWENYE MIRADI KUONGEZA AJIRA

    June 29, 2025
  • KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE KITAIFA AWEKA JIWE LA MSINGI SOKO JIPYA LA MBUYUNI, MOSHI

    June 28, 2025
  • MWENGE WA UHURU UTAZINDUA, KUWEKA MAWE YA MSINGI NA KUTEMBELEWA MIRADI 52 YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 84

    June 28, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa