June 29 mwaka huu, mwenge wa uhuru ulikagua miradi nane yenye thamani bilion 1.9
Katika miradi hiyo, Mwenge umeridhishwa na mradi wa vijana wa win youth group wenye thamani ya milioni 40 kutoka katika mkopo wa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu uliotolewa na halimashauri.
Akisoma taarifa ya Mradi huo, katibu wa kikundi hicho Flavia Tengia alisema walipokea milion 40 kutoka halmashauri kwa miradi miwili ukiwemo wa kusindika siagi ya karanga na mradi wa stationary lenye lengo la kuboresha uchumi kwa vijana na tayari wamesharesha milion nane, alisema wametoa ajira kwa vijana 13 na wanatarajia kuendelea kutoa ajira hizo kutoka na uchumi kwa kupata masoko zaidi ndani na nje ya nchi.
Akizindua mradi huo kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa Bw. Ismail Ali Ussi aliridhishwa na mradi huo na kuwataka viongozi wa wilaya hiyo kuhakikisha wanasajili kikundi hicho kwenye mfumo wa Nest kwa lengo la kufunguliwa ndani na nje ya nchi.
Alisema kikundi hicho kimeonyesha namna ambavyo serikali ya Dkt. samia Suluhu Hassan inaleta umahiri katika kutokomeza umaskini kwa vijana na kuongeza ajira.
Aidha amewataka vijana kujitokeza kwa wingi katika kuhakikisha wanachangamkia fursa za mikopo kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu katika kuanzisha na kupanua biashara zao.
Amesema, Hii ni nchi pekee inayowajali wananchi wake hasa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu ili waweze kujiajiri nakuajiri wengine.
17 Barabara ya Florida
Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi
Simu: +255 (027) 2754236/7
Mobile:
Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz
Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa