• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

CHANGAMOTO YA MAJI YASIYO SALAMA KWISHA LANG'ATA BORA WILAYANI MWANGA

Posted on: July 1st, 2025

WANANCHI wa kijiji cha Lang'ata bora wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro wameondokana na changamoto ya matumizi ya maji yasiyo safi na Salama baada ya serikali kutekeleza mradi wa kisima cha maji safi.


Wananchi hao walitoa kilio chao hicho leo wakati Mwenge wa Uhuru ulipofika kijijini hapo kuzindua kisima hicho chenye urefu wa mita 152 kilichogharimu milioni 80.181.

Akizungumza mbele ya Mkimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ismail Ali Ussi,  mmoja wa wananchi hao, Happiness Mathayo alisema kuwa walikuwa wanalazimika kutumia maji yasiyo safi na salama ya Bwawani  hali iliyokuwa ikipelekea kupata magonjwa ya mlipuko.

"Furaha yetu sisi wakinamama ni kupata maji haya safi na salama maana tumekuwa tukitumia maji yasiyo safi ya Bwawa  ambapo samaki huvuliwa huko huko, punda hufia huko, watoto wanaoga huko huko bwanani na kujisaidia kwa hiyo sisi magonjwa ya mlipuko yalikuwa hayachezi mbali kila wakati tumekuwa watu wa kuharisha na kutapika" Alisema Happiness.


Alisema kuwa, kupitia mradi huo ambao umetekelezwa na Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweza kuwatua wakinamama ndoo kichwani na kuwafanya kutowapeleka watoto zahanati kila mara kwa ajili ya magonjwa ya mlipuko.

Aliongeza kuwa, kwa mambo makubwa aliyofanya Rais ifikapo mwezi Oktoba watamlipa madeni yake kwa kumpa kura nyingi na za kishindo ili kumlipa kutokana na kazi kubwa alizozifanya.


Kwa upande, Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru, Ismail Ali Ussi alisema kuwa, Mwenge huo umekuwa na lengo la kuleta matumaini pasipo na matumaini na wananchi walikuwa na tatizo la maji kwa muda mrefu lakini Serikali ya awamu ya sita imeweza kutatua kwa vitendo.


"Kwa mara ya kwanza Rais Dkt. Samia akiwahutubia wananchi kupitia ndani ya Bunge la Jamhuri moja ya jambo ambalo aliwaahidi Wananchi ni swala zima la kuhakikisha anaenda kutengeneza na kuboresha miundombinu ya maji safi na salama ndio maana leo kupitia Wizara ta maji imekuwa ikitatua kero za maji vijijini' alisema Ussi.


Kiongozi huyo, alisema kuwa eneo hilo lilikuwa linakabiliwa na changamoto kubwa ya miundombinu ya maji safi na salama lakini  Rais ameliona hilo na kwa upendo mkubwa kwa Wananchi Mwenge wa Uhuru umekuja kuweka amani, upendo na Heshima ambayo Dkt. Samia aliwaahidi wanalang'ata.


Aidha aliwataka Wananchi kuulinda na kuitunza miundombinu hiyo ya maji safi na salama ili iweze kudumu na kuwahudumia kwa muda mrefu kwani Serikali imetumia fedha nyingi.


Awali akisoma taarifa ya mradi huo kwa kiongozi wa Mwenge, Meneja wa Wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini wilaya ya Mwanga, Mhandisi Christine Kessy alisema kuwa, kisima cha Lang'ata Bora ni miongoni mwa programu ya visima 900 inayotekelezwa na Wizara ya maji.


Mhandisi Christine alisema kuwa, utekelezaji wa mradi ulianza Oktoba 2024 na kukamilika Februari 2025 ambapo walichimba kisima chenye urefu wa mita 152 ambacho kina uwezo wa kutoa maji lita 14000 kwa saa ambapo utawahudumia wananchi wapatao 3340.


Alisema kuwa, gharama za mradi huo ni shilingi milioni 80,181,620. kutoka benki ya Dunia kupitia programu ya PforR na kwa sasa umeshakamilika na kutoa maji kwa wananchi wa kijiji cha Lang'ata na Handeni.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • UPANUZI WA SKIMU YA MAJI YA LAWATE (GARARAGUA - KIDICO) KUNUFAISHA WANANCHI ZAIDI YA 7,000 WILAYANI SIHA.

    July 03, 2025
  • SERIKALI KUBORESHWA HUDUMA ZA AFYA ROMBO

    July 02, 2025
  • IDADI YA VIFO VYA AJALI YA MOTO SAME YAFIKIA 42

    July 02, 2025
  • VIJANA WILAYANI ROMBO WAMEHIMIZWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

    July 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa