• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

STENDI YA NGANGAMFUMUNI KUANZA KAZI APRILI, 2026

Posted on: August 28th, 2025

Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Kiseo Nzowa amesema katika juhudi za boresha huduma ya usafiri na usafirishaji Mkoani  Kilimanjaro Serikali imehakikisha ifikapo APRILI, 2026 kituo cha mabasi cha kimataifa cha Moshi (NGANGAMFUMUNI) kinaanza kutoka huduma za usafiri Kwa Wananchi wa Moshi.


Amesema hayo Agosti, 27,2025 katika hafla ya kumkabidhi Site Mkandarasi Mkuu CRJE (EAST AFRICA) LTD wa Dar es Salaam


Bw. Nzowa amesema mradi huu utakapoanza kutoka huduma utaongeza Ajira Kwa wakazi wa Moshi watakaofanya biashara katika STENDI hiyo na wale watakao ajiriwa nafasi mbalimbali pia  itaongeza mapato katika Manispaa ya Moshi na Nchi Kwa jumla.


Hata hvyo, Bw. Nzowa ametoa wito Kwa Wananchi wa Moshi kuwa walinzi wa rasilimali zinazoletwa katika mradi huo wakati wa utekelezaji

"Kuna baadhi ya watu sio waaminifu, wanatabia ya kuchukua  na kuuza vifaa vya ujenzi hvyo kila Mmoja wetu awe mlinzi wa mwenzake na kutoka taarifa katika vvyombo vya usalama.


Aidha, Nzowa amemtaka Mkandarasi na TIMU yake kuhakikisha mradi unakamilika Kwa wakati na Kwa viwango bora ili uanze kutoa huduma Kwa muda uliopangwa.


Naye  Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mhe. Godfrey Mnzava amesema halmashauri imekua kwenye mikakati mbalimbali ya kujenga vyanzo vipya vya mapato lengo ni kuweza kuongeza ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Kwa upande Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi Mwajuma Nasombe amesema ujenzi WA awamu ya Kwanza ambao umefikia asilimia 51 ya utekelezaji wake  unagharimu kiasi cha shilingi 19,834,027,619,08  huku ukihusisha ujenzi WA jengo la abiria lenye gorofa mbili ambalo litakua na maduka,sehemu za kukatia tiketi,migahawa,maeneo ya kusubiria wakati wa kupakia au kushusha abiria eneo la kuhifadhia mizigo,vyumba vya Ofisi,vyumba vya idara ya uhamiaji,kituo cha polis,eneo la kupakia magari na tank la ujazo WA Lita 476,000 .



 Aidha, amesema halmashauri imepokea shilingi bilioni 7,485,504,635.70 kutoka serikali kuu huku halmashauri ikichangia shilingi bilioni 1,248,746,423.54  na kufanya jumla ya fedha kuwa Shilingi 8,734,251,059.24.

Mwajuma amesema katika awamu ya pili ujenzi utahusisha jengo la hoteli lenye gorofa nne ambalo litakua na vyumba 48 vya kulala, mgahawa, supermarket,maduka, eneo la benki na sakafu ya chini ya kupakia magari madogo na daraja ambalo litaunganisha jengo la abiria na hotel ambalo chini mabasi yatapita na juu kutakua na maduka huku vikigharimu kiasi cha shilingi 9,030,621,703.77 hadi kukamilika.

Mradi huu ulianza rasmi tarehe 28/1/2019 na ulipaswa kukamilika tarehe 28/1/2021 kutokana na changamoto mbalimbali mkandarasi aliongozewa muda WA utekelezaji na kutarajiwa kukamilika rasmi APRILI,2026.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • MAJALIWA ATAKA MIKAKATI ZAIDI MATUMIZI YA NISHATI SAFI KWENYE MAGEREZA.

    August 30, 2025
  • STENDI YA NGANGAMFUMUNI KUANZA KAZI APRILI, 2026

    August 28, 2025
  • KONGAMANO LA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO KILIMANJARO

    August 26, 2025
  • RC ATOA SIKU 14 MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI KIJIJI CHA RUVU MARWA SAME

    August 21, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa