• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC ATOA SIKU 14 MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI KIJIJI CHA RUVU MARWA SAME

Posted on: August 21st, 2025

Katika juhudi za kudhibiti na kutatua mgogoro wa muda mrefu wa ardhi baina ya Wakulima na Wafugaji katika kijiji cha Ruvu Marwa, wilayani Same, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu ametoa siku 14 kwa wakulima na Wafugaji wa kijiji hicho  wanaofanyakazi zao za kilimo na ufugaji katika eneo la ekari 2787 kupisha wataalamu kutoka ofisi za ardhi mkoa na wilaya kwa kushirikiana na pande zote mbili kupata suluhu ya matumizi bora ya ardhi.


Akizungumza na wakazi wa kijiji hicho Agosti 20, 2025 Mhe.  Babu alieleza kuwa mgogoro huo hauwezi kuachwa uendelee na kwamba Serikali imejipanga kuhakikisha haki inapatikana kwa wote bila upendeleo.


"Katika eneo hili la hekari 2,787, Wafugaji wasiendelee kulitumia na Wakulima nao wasifanye shughuli yoyote hadi ndani ya siku 14 suluhu ipatikane. Tunahitaji suluhisho la pamoja, si mivutano ya kila mwaka," alisema Mkuu huyo wa Mkoa.


Akiwa ameambatana na viongozi wa wilaya, wataalamu wa ardhi na kilimo, Babu aliagiza shughuli zote zilizokuwa zikiendelea kwenye eneo hilo kusitishwa mara moja ili kutoa nafasi kwa majadiliano ya kina.


Katika hatua nyingine, aliahidi kupeleka wataalam kutoka ofisi yake kwenda kutathmini maeneo ya wakulima yanayoathiriwa na mafuriko kila mwaka, ili kuwezesha upatikanaji wa vifaa na miundombinu ya kudhibiti maji kuingia mashambani.



Serikali imetoa wito kwa wakazi wa Ruvu Marwa Wakulima na Wafugaji kudumisha amani, mshikamano na utulivu bila kuangalia tofauti za kikabila, kidini wala maisha ya mtu.



"Ninyi ni Watanzania, rudisheni mahusiano yenu. Amani ndiyo msingi wa maendeleo. Hatutaki kila siku tuwe tunaleta polisi. Na kuhusu Mwenyekiti wa kijiji, hiyo ni kazi yangu na chama tutachukua hatua stahiki," aliongeza Babu.


Katika risala yao kwa Mkuu wa Mkoa, wakulima kupitia kwa msemaji wao Penueli Mkomwa, walieleza kuwa wamekuwa wakikumbwa na mafuriko ya mara kwa mara katika bonde la Ruvu, hali inayowasababishia hasara kubwa.


Mkomwa alieleza kuwa lipo eneo la wazi ambalo halijaathiriwa na mafuriko na linaweza kutumika kwa muda, lakini eneo hilo ni sehemu ya pori tengefu, hivyo kuhitaji uamuzi wa Serikali kuhusu matumizi yake

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • RC ATOA SIKU 14 MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI KIJIJI CHA RUVU MARWA SAME

    August 21, 2025
  • WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII YAFUATILIA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KILIMANJARO.

    August 21, 2025
  • WADAU WA TASNIA YA NGOZI WAPATIWA MAFUNZO YA KUBORESHA UZALISHAJI NA THAMANI YA ZAO LA NGOZI

    August 13, 2025
  • KILIMANJARO YAPIGA HATUA KATIKA LISHE

    August 13, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa