• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

KONGAMANO LA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO KILIMANJARO

Posted on: August 26th, 2025

WAFANYABISHARA Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kushirikiana kwa karibu na serikali katika kuboresha mazingira ya biashara ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wote wa mkoa huo

Wito huo umetolewa  Jana  katika kongamano la wafanyabiashara ndogondogo lililofanyika katika soko la Mbuyuni, mjini  Moshi  likiwa na lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya sekta binafsi na serikali.

Akizungumza katika kongamano hilo, Mkuu wa Wilaya ya Moshi,  Godfrey Mnzava alisema serikali iko tayari kushirikiana na sekta binafsi kutatua matatizo  yanayowakumba wafanyabiashara wadogo, huku akisisitiza kuwa mafanikio ya sekta hiyo yanachangia kwa kiasi kikubwa ustawi wa jamii.



"Serikali ni chombo chenu mnachotakiwa shirikiana nacho ili kutatua matatizo yanayowakabili , pia mikopo ipo kwenye halimashauri zetu mjinge kwenye vikundi  mpate mikopo hiyo iwasaidie KATIKA kukuza biashara zenu,

Hii itawasaidia kutoka kwenye biashara ndogo ndogo kwenda kwenye biashara kubwa. muweze kulipa Kodi, kutoka ajira kwa vijana na kubadilisha mfumo wa maisha yetu na familia zetu,"alisema Mzava

Awali akimkaribisha mkuu huyo, katibu tawala  ya Moshi, Shabani Mchomvu, alisema  serikali imepiga hatua kubwa katika kuwawezesha wafanyabiashara wadogo kwa kutumia mifumo ya kidijitali, ambayo imeongeza uwazi, usimamizi na urahisi wa huduma.




 Alisema   jumla ya wafanyabiashara 3,000 wamesajiliwa kupitia mfumo wa Wezesha Portal, kati yao wanaume ni 1,070 na wanawake 1,930, ikiwa ni hatua muhimu katika kutambua na kurasimisha biashara ndogondogo.

"Zaidi ya milioni 317 zimetolewa kama mikopo kwa wafanyabiashara 145 kupitia Benki ya NMB, fedha ambazo zimeelekezwa kwenye kukuza mitaji na upanuzi wa biashara. Mikopo hiyo isiyo na riba imekuwa chachu ya mabadiliko kwa wengi, hasa wanawake na vijana waliokuwa na tatizo  ya mitaji"

Alisema pia Serikali pia imefanikiwa kujenga, kukarabati na kurasimisha maeneo 41 ya biashara katika wilaya mbalimbali za mkoa, hatua iliyopunguza kwa kiasi kikubwa tatizo  la uhaba  wa maeneo rasmi ya kufanyia biashara kwa wafanyabiashara wadogowadogo.




Naye mwakilishi kutoka Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu,  Juliana Mtolela, alisema kuwa serikali  imekuwa mstari wa mbele katika kuwezesha makundi maalum kwa kuwapatia mitaji, mafunzo na fursa za kiuchumi.


“Kupitia programu na mikakati mbalimbali ya kitaifa, serikali imefanikiwa kuwafikia maelfu ya wafanyabiashara wadogo nchini kwa kuwapatia mitaji, mafunzo ya ujasiriamali, pamoja na kuwaunganisha na taasisi za kifedha,” alisema  Mtolela,



Wafanyabiashara walioshiriki kongamano hilo walieleza kufurahishwa na hatua zinazochukuliwa na serikali, huku wakisisitiza umuhimu wa kupatiwa elimu ya masoko na usimamizi wa fedha ili kuongeza ufanisi katika biashara zao.


Baadhi ya wafanyabiashara waliopatiwa mikopo walieleza kuwa mitaji hiyo imewasaidia kuongeza bidhaa, kuboresha huduma na kuongeza ajira kwa vijana wa maeneo yao. Walisema mafanikio hayo yameanza kuleta mabadiliko chanya kwenye maisha yao na ya jamii inayowazunguka.

Viongozi wa vikundi vya wafanyabiashara walipongeza serikali kwa kujenga miundombinu rafiki ya biashara kama vile vibanda vya kisasa, mabanda ya masoko na miundombinu ya maji na umeme, ambayo imeboresha mazingira ya kazi na kuvutia wateja zaidi.

Serikali imesisitiza kuwa itaendelea kushirikiana kwa karibu na wadau wa sekta binafsi kuhakikisha kuwa biashara ndogondogo zinakua na kuwa endelevu, huku ikiwahimiza wafanyabiashara kujiunga na vikundi vya kuweka na kukopa ili kuimarisha mitaji yao.


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KONGAMANO LA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO KILIMANJARO

    August 26, 2025
  • RC ATOA SIKU 14 MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI KIJIJI CHA RUVU MARWA SAME

    August 21, 2025
  • WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII YAFUATILIA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KILIMANJARO.

    August 21, 2025
  • WADAU WA TASNIA YA NGOZI WAPATIWA MAFUNZO YA KUBORESHA UZALISHAJI NA THAMANI YA ZAO LA NGOZI

    August 13, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa