• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

DC Warioba Ataka Usimamizi Mzuri wa KINAPA kwa Manufaa ya Vizazi Vyote

Posted on: February 8th, 2020

Wanachi wa wilaya Moshi wametakiwa kuendelea kutunza mazingira ya  Hifadhi ya Taifa ya Mlima  Kilimanajaro KINAPAili iendelee kunufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.

Akiongea na wanachi wa vijiji vya Kitowo na Kiraracha Kata ya Marangu Magharibi wilayani Moshi baada ya kukabidhiwa mradi  wa zahanati katika kijiji cha Kitowo uliojengwa na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania TANAPA kupitia hifadhi ya Taifa ya Mlima na Kilimajaro KINAPA katika kijiji cha Kitole Mkuu wa wilaya ya Moshi Mhe. Kippi Warioba amewataka wananchi kutokuwa wabinafsi kwa kutumia rasilimali zilizopo katika hali ya kuziharibu na kuziangamiza jambo ambalo si sahihi hata mbele za mungu.

Mhe. Warioba amesema  si fikra sahihi kwamba binadamu wulio karibu na rasilimali hizi kwa sasa wana haki ya kutumia hovyo bila utaratibu, hivyo basi rasilimali zote za hifadhi zitumike vizuri na wakati huohuo zitunzwe na ziongezwe ili ziwe endelevu. "Matumizi lazima yawe endelevu, watoto wetu hawa wana haki ya kunufaika na rasilimali hizi, hivyo basi tusidhani kwamba tunaruhusiwa kuvuna miti na wanyama wote ndani ya hifadhi hapana" Alisema Mhe. warioba.

Mbali na hilo Mhe Warioba amewakumbusha wananchi hao kuwa  maji safi yanayotiririka kutoka kwenye hifadhi ya KINAPA yananufaisha wananchi wengi katika  mikoa mitano kwa matumizi ya moja kwa moja ya majumbani na kiasi kingine cha maji kinaingia kwenye bwawa la Nyumba ya Mungu linalozalisha umeme.

Aidha Mhe. Warioba amewataka wananchi kuwa makini na wanasiasa hususan katika mwaka huu wa uchaguzi ili wasije kulaghaiwa kwa kuombwa kura kwa kuahidiwa kuwa wataruhusiwa kuingia ndani ya hifadhi bila kufuata sheria na tararibu.

Mhe Warioba amewataka wananchi wawe tayari kutoa taarifa sahihi na kwa wakati kuhusu waharibifu wa mazingira na majangiri ili hatua za kudhibiti zichukuliwe mara moaja.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Dkt.Alex Kazula ameishukuru KINAPA  kwani mradi huo unaongeza idadi ya vituo vya na kufanya vifikie 96  katika wilaya ya Moshi.

Dkt. Kazula ameongeza kuwa mradi huo unatarajiwa kuanza kutoa huduma tarehe moja mwezi machi mwaka hu,  kwani hadi sasa tayari halmashauri imeshapokea jengo na  samani, vinasubiriwa sasa ni vifaa tiba

Aidha Dkt. Kazula ameshukuru wizara ya Afya kwa kutoa kubali cha kuendesha kituo hicho hali kadhalika ameishukuru  Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kutoa  ruhusa ya kufungua akaunti ya kituo ili huduma zianze kutolewa.

Mradi huo ambao ni kutuo pekee cha serikali unatarajia kunufaisha  zaidi ya wananchi 15,000 kutoka kwenye  vijiji 6 vilivyomo katika kata ya Marangu Magharibi.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Kamishna Mwanadamizi wa TANAPA kanda ya Kaskazini,Hernman Batiho amesema mradi huo umechangiwa na  KINAPA, wananchi, halmashauri.

Kamishna Batiho amefafanua kuwa gharama za mradi ni jumla shilingili milioni 238, 994 ,540. ambapomMchango wa TANAPA  ni  214 994 540 na thamani ya mchango wa wananchi ni  24,000,000/=. Gharama hizo zinajumuisha ujenzi pamoja na ununzi wa samani na vifaa tiba.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO ASISITIZA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANANCHI WILAYANI HAI

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA SIHA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI BORA WA MAPATO

    June 17, 2025
  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa