• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Jamii Yafaidi Maboresho ya Miundombinu: RC Babu Atoa Wito wa Utunzaji

Posted on: August 7th, 2025

Wananchi wa maeneo ya Kileo wilayani Mwanga na Hedaru wilayani Same, mkoani Kilimanjaro, wameanza kunufaika na maboresho makubwa ya miundombinu ya barabara na daraja, yanayotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS).

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Babu, ametoa wito kwa wananchi kuhakikisha wanatunza miundombinu hiyo kwa kuwa ni matokeo ya uwekezaji mkubwa unaolenga kuboresha maisha ya watu na kuzuia madhara yanayosababishwa na mvua za mara kwa mara.

Akizungumza Agosti 7, 2025, katika ziara yake ya siku moja eneo la Kileo, Babu alisema serikali inatekeleza ujenzi wa boxcalvert saba pamoja na kunyanyua tuta la barabara kufikia urefu wa mita 1.5, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kutatua kero za muda mrefu za usafiri nyakati za mvua.

"Kileo ilikuwa korofi sana hasa wakati wa mvua. Serikali kupitia TANROADS imejenga boxcalvati 7 na mradi huu umefikia asilimia 31 ya utekelezaji. Tunatarajia kutumia zaidi ya shilingi bilioni 6 kukamilisha kazi hii," alisema Babu.

Akiwa katika eneo la Hedaru wilayani Same, RC Babu alitembelea ujenzi wa daraja jipya litakalogharimu shilingi bilioni 1.5, likilenga kuzuia madhara ya maji yanayotiririka kutoka milimani, ambayo yamesababisha athari kubwa kwa wananchi.

"Katika mvua za El Niño 2023/2024 tulipata adha kubwa sana. Wapo wananchi waliopoteza maisha. Mheshimiwa Rais ametoa fedha ili kukamilisha daraja hili kwa haraka. Tayari kazi imefikia asilimia 50 na tunatarajia kukamilika ifikapo Septemba 4 mwaka huu," aliongeza.

Mkuu huyo wa Mkoa alisisitiza kuwa mafanikio haya ni ya wananchi wote na akawataka kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hiyo kwa manufaa ya sasa na vizazi vijavyo.


"Tuwe maaskari wa miundombinu yetu. Tukubali kubadilika na kuitunza kwa sababu changamoto zilikuwa zikitutesa kwa muda mrefu," alisema.

Akitoa taarifa kwa mkuu wa mkoa, Meneja wa TANROADS mkoa wa Kilimanjaro, Mhandisi Motta Kyando, alisema mkoa umepokea ufadhili wa shilingi bilioni 16.2 kwa ajili ya ujenzi wa madaraja, njia za maingiliano, na usimamizi wa miradi mbalimbali ya barabara.

Ameeleza kuwa fedha hizo ni sehemu ya mpango wa serikali wa kuhakikisha maeneo hatarishi yanapata ufumbuzi wa kudumu kupitia miradi ya kimkakati inayolenga kuboresha miundombinu ya usafirishaji.

Naye   Msimamizi wa Mradi wa Kileo kutoka kampuni ya King Builders, Mhandisi Paul Mwanawima, alisema mradi unaendelea vizuri licha ya changamoto ya maji mengi kwenye eneo hilo.

"Maji yalikuwa mengi sana wakati tunaanza kazi, hali iliyoathiri hata mashine zetu. Lakini tumekabiliana na hali hiyo na tunaendelea vizuri. Tunatarajia kukamilisha kazi mwanzoni mwa Septemba," alisema Mhandisi Mwanawima.


Wananchi wa maeneo husika wameanza kuona manufaa ya miradi hiyo huku wengi wakisema kuwa usafiri umeimarika na wana imani kuwa baada ya kukamilika, matatizo ya mafuriko na mazao kuozea barabarani yatabaki kuwa historia.

Kwa ujumla, maboresho ya miundombinu katika mkoa wa Kilimanjaro yanaendelea kuwa chachu ya maendeleo na kiashiria cha dhamira ya dhati ya serikali kuboresha maisha ya wananchi kwa vitendo.

Mwisho

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • WADAU WA TASNIA YA NGOZI WAPATIWA MAFUNZO YA KUBORESHA UZALISHAJI NA THAMANI YA ZAO LA NGOZI

    August 13, 2025
  • KILIMANJARO YAPIGA HATUA KATIKA LISHE

    August 13, 2025
  • Jamii Yafaidi Maboresho ya Miundombinu: RC Babu Atoa Wito wa Utunzaji

    August 07, 2025
  • KISHINDO CHA MWENGE WA UHURU 2025

    July 16, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa