• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

KILELE CHA MAADHIMISHO YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

Posted on: April 26th, 2023



Tarehe 26 Aprili mwaka 1964 Tanganyika na Zanzibar ziliungana kuwa Taifa moja la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Maadhimisho haya yamefanyika Kimkoa kwa kuandaa Kongamano la Mafanikio ya miaka 59 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo mada mbalimbali zimewasilishwa na watoa mada mbalimbali.


Hata hivyo, Muungano huu umejengeka kutokana na historia ya uhusiano wa undugu wa damu ya wananchi wa Tanganyika na Zanzibar, harakati za pamoja za kupigania haki na ustawi wa wananchi wa nchi zote mbili kupitia ushirikiano wa vyama vya ukombozi vya Tanganyika African National Union (TANU) na Afro Shirazi Party (ASP) katika kupigania uhuru. Mahusiano hayo yaliyowezeshwa na kudumishwa na waasisi wa Taifa letu, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Sheikh Abeid Amani Karume ndiyo yaliyorasimisha Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.


Mkuu wa Mkoa wa Kiliamnjrao Mhe. Nurdin Babu amesema muungano huo umesadia kujenga na kuturithisha misingi ya undugu, uzalendo, amani, upendo, mshikamano na utulivu ambavyo vimekuwa nguzo kuu ya Muungano wetu.

Mhe. Babu amesema Muungano huu umedumu kutokana na mizizi yake kujikita kwa wadau wakuu wa Muungano ambao ni wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pia umakini mkubwa na usikivu wa hali ya juu wa viongozi wetu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kutekeleza sera endelevu za Muungano na kufuatilia kwa karibu changamoto zinazojitokeza na kuzipatia ufumbuzi umekuwa chachu katika kudumu kwa Muungano wetu.


Aidha,Mhe. Babu amesema kutokana na kuimarika kwa amani, utulivu na usalama katika nchi yetu mambo muhimu yameimarika kama uchumi na ustawi wa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika sekta za elimu, afya, siasa, utamaduni na kijamii. Kuimarika huko kunatokana na uwepo wa mazingira wezeshi na mahusiano mazuri ya kibiashara kati ya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.


Aidha, Kuongezeka kwa miundombinu ya kutolea huduma ya Afya kwa kuongeza vituo vya kutolea huduma za afya ndani ya Mkoa ambavyo kwa sasa Mkoa una vituo vya kutolea huduma za afya 427 ambapo kati ya hivyo Hospitali 21, vituo vya afya 51 na Zahanati 344.


Kusambaza na kukarabati miundombinu ya umeme na kufanya vijiji na Mitaa 569 kati ya vijiji na Mitaa 579 iliyopo katika Mkoa kufikiwa na huduma ya umemepia Serikali kwa kushirikiana na wadau wa elimu imejenga jumla ya Shule za awali na Msingi 1978, Sekondari 352, Vyuo vikuu na kati 75 ambayo imerahisisha upatikanaji wa huduma ya elimu karibu na wananchi.


Kwa upande Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Tixon Nzunda katika maadhimisho hayo amesema Tanzania ni Nchi imara isiyoweza kuyumbishwa na mtu yoyote kutokana na misingi imara iliyojengwa na Viogozi wetu.

Aidha, Nzunda amesema kuongamano hilo linawaleta pamoja wadau wa Mkoa wa Kilimanjaro lengo hasa ni kuendeleza taaluma, utafiti na ushauri katika kudumisha na kuendeleza Muungano wa Taifa letu na kujenga maarifa kwa watu nchini na Duniani kote.

Vile vile linalenga kuafakari kwa pamoja na kwa kina juu na namna bora zaidi ya kuimarisha utu, umoja,mshikamano,udugu kama Msingi imara wa Muungano wetu kwa maslahi mapana ya Taifa la Tanzania, Africa na Dunia kwa ujumla.


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa