• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mkuu wa Mkoa Awataka Wananchi Kuithamini KINAPA

Posted on: February 7th, 2020

Wananchi wa Mkoa wa Kiilimanjaro hasa wanaoishi kwenye vijiji vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro KINAPA wametakiwa kuthamini mchango wahifadhi hiyo katika  kujitoa  kwenye kuchangia maendeleo ya elimu ndani ya mkoa wa Kilimanjaro.

Akiongea baada ya kupokea mradi wa madarasa mawili, ofisi ya mwalimu,madawati  pamoja na  samani za ofisi  zilizotolewa na KINAPA kwa shule ya msingi Mweka wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Dkt. Anna Mghwira, amesema kuchangia miradi ya maendeleo ikiwemo elimu ni jukumu la jamii nzima hivyo KINAPA wanaonesha mfano wa kuigwa katika kuchangia maendeleo.

Kuhusu ubora wa vyumba vya madara pamoja na ofisi ya mwalimu Mhe. Dkt. Mghwira amesma ameridhishwa na ubora wa majengo hayo kwani ubora wa mradi unaendana na thamani."Haya ndiyo madarasa yanayotakiwa katika kutoa elimu, hata ofisi ya mwalimu ndivyo inavyotakiwa iwe pamoja na samani za ndani ya ofisi".Alisema Mhe.Dkt. Mghwira.

Akitoa taarifa ya utekelezaji wa Miradi ya Ujirani Mwema Kamishna Mwanadamizi wa TANAPA Kanda ya Kaskazini, Herrman Batiho amesma mradi wa vyumba vitatu vya madarasa, ofisi ya mwalimu, madawati 72  pamoja na samani za ofisi  ambazo ni meza saba, viti vinane   na makabati matano, katika shule ya msingi Mweka umetekelezwa kwa ushirikiano kati ya Shirika la hifadhi za taifa TanzaniaTANAPA kupitia hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro KINAPA,wananchi na Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.

Aidha  Kamishna Batiho amefafanua kuwa mradi huo wenye thamani ya shilingi za kitanzania  milioni  123,370,760 umetekelezwa kwa  TANAPA kuchangia asilimia 70 ambayo ni shilingi za kitanzania milioni   120,490,760 na mchango wa jamii  ni shilingi za kitanzania 2,880,000 sawa na aslimia 30.

Kamishna Batiho ameongeza kuwa wananchi wamechangiakwa kutoa nguvu kazi, malighafi pamoja na ufundi huku Halmashauri ya wilaya Moshi ikichangia ramani ya mradi, maandalizi ya gharama halisi za mradi yaani BOQ na kutoa ushauri wa kitaalam.

Akisoma risala ya shukrani kwa serikali na Shirika la Hifadhi za Taifa TANAPA,  mtendaji wa kijiji cha Mweka, Sophia Sanga amesema wanakijiji wanatambua na kuthamini uwepo wa hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro kama jirani yao mwema anayewajili.

Katika wilaya  ya Moshi KINAPA inatekeleza miradi ya mbalimbali ya maendeleo kwenye vijiji kumi kwa lengo la kutekeleza nia ya hifadhi ya kutoa sehemu ya mapato yake kwa jamii ili jamii inufaike na mapato yanayotokana na shughuli za uhifadhi ili na wao washiriki kuunga mkono juhudi za serikali katika kushriki kikamilifu katik ashughuli za uhidafadhi.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa