• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MPANGO KABAMBE

Posted on: April 11th, 2017

Serikali mkoani Kilimanjaro imewataka viongozi wa kisiasa na wananchi  kutotanguliza maslahi binafsi ya kisiasa na vyama vya siasa  na kushiriki ipasavyo katika mpango kabambe (Master Plan) wa Mji wa Moshi.

Akizungumza katika  hafla ya uzinduzi wa utayarishaji wa mpango huo uliowakutanisha  madiwani na watendaji wa  serikali katika ngazi mbalimbali,Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Sadiki M.Sadiki amesema ni vyema viongozi wakatathimini fursa mbalimbali za maendeleo zitakazowafikia wananchi wa mji wa Moshi na Mkoa wa Kilimanjaro na kuachana kutanguliza maslahi binafsi ya wanasiasa na vyama vya sisiasa  ambazo   zitawachelewesha wananchi kufikia maendeleo.

Sadiki amesema kwa sasa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi iko kwenye maandalizi ya mpango mpya wa mwaka 2017-2037 ikiwa na ukubwa wa kilomita za mraba 142, kwa mujibu wa Gazeti la Serikali  Namba 219 la Tarehe 15 Julai 2016.

Ameongeza kuwa mpango huo unahusisha kuongeza eneo la mji wa Moshi kwa  kuongeza kilomita za mraba 68 kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Moshi na kilomita za mraba 16  kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Hai.

Akifafanua zaidi Sadiki amesema kutokana na mpango huo kutakua na athari za mabadiliko katika wilaya ya Moshi na Hai  kutokana na upanuzi wa mipaka kisheria na kuhusisha baadhi ya  kata zilizopo katika wilaya hizo kuingia katika mji wa Moshi.

Sadiki ameongeza kuwa kufuatia upanuzi huo kutakuwa na mabadiliko ya kiutawala hivyo basi viongozi wa kisiasa wasiwe na hofu juu ya hatima zao kisiasa. “Kuna baadhi ya watu wafikiria juu ya hatima za udiwani wao endapo kata zao zitaingia ndani ya mji. ” alisema Mhe. Sadiki.

Aidha Mhe. Sadiki aliwataka wajumbe wote kuwapa ushirikiano wataalamu wa mipangomiji watakapowasilisha mpango huo na kutokuwa na hofu ya kukosa fursa za uongozi kwani kama kiongozi atahitajika na wananchi wataendelea kumchagua.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO ASISITIZA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANANCHI WILAYANI HAI

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA SIHA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI BORA WA MAPATO

    June 17, 2025
  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa