• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MWENGE WA UHURU KURIDHIA MIRADI YOTE 45 KILIMANJARO

Posted on: June 27th, 2023

Jumla ya miradi yote 45 yenye thamani ya Tshs. Bilioni 30.35 iliyopititiwa na Mwenge wa Uhuru imefunguliwa,kuzinduliwa,kuwekewa mawe ya msingi na kukaguliwa.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Abdalla Shaib Kaim amepongeza Uongozi wote wa Mkoa wa Kilimanjaro na Halmashauri kwa ujumla kwa usimamizi mzuri wa miradi iliyokidhi vigezo na viwango vinavyotakiwa na kwa upangaji mzuri wa nyaraka na wataalamu kutoa ushirikiano katika ukaguzi wa miradi.

Ametoa pongezi hizo wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Kilimanjaro kwenda Mkoa wa Arusha katika viwanja vya Tingatinga Wilayani Longido.

Abdalla amesema miradi yote 45 iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru hakuna uliokataliwa hii ni ishara nzuri ya ushirikiano uliopo kati ya viongozi wa ngazi tofauti tofauti katika kuleta maendeleo ya nchi.

Akiwasilisha taarifa ya makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru Kutoka Mkoa wa Kilimanjaro kwenda Mkoa wa Arusha, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amesema mwaka huu Mkoa umezingatia vigezo vyote vilivyobainishwa kwenye muongozo hii ndio sababu ya kupata matokeo mazuri katika miradi yote iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru.

Mhe. Babu amesema, Mwenge wa Uhuru ulitembelea miradi ya elimu 9, afya  miradi 9, maji maji 7, utunzaji wa mazingira miradi 7, barabara miradi 6, maendeleo ya vijana miradi 5 na miradi mengineyo 2 na  ulipata fursa ya kuona na kutembelea miradi mbalimbali ya makundi mbalimbali ya vijana wenye ulemavu na wanawake ambao wamedhamiria kuzalisha mali na kujiendeleza kiuchumi. Vile vile umezindua klabu za kupambana na Rushwa, Madawa ya Kulevya, Malaria,Uhifadhi na uendedlezaji wa mazingira.

Ameendelea kusema katika kipindi cha mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoani hapa katika kutekeleza kauli mbiu ya Mwenge 2023 “Tunza Mazingira, okoa vyanzo vya Maji kwa Ustawi wa Viumbe Hai kwa Uchumi wa Taifa”  Mkoa ulijiwekea lengo la kuhakikisha miradi yote itakayopitiwa na mbio za Mwenge wa Uhuru 2023 kabla na wakati wa mbio hizo miti inapandwa na hivyo kupelekea jumla ya miti 7,857 kupandwa. Aidha, Serikali na Wananchi wamedhamiria kurudisha uoto wa asili wa Mkoa wa Kilimanjaro hivyo wamepanda jumla ya miti 6,765,328 katika maeneo ya taasisi mbalimbali, vyanzo vya maji na maeneo ya wazi kabla ya Mwenge kupita kwa kuzingatia Sera, kanuni na Taratibu za uhifadhi wa mazingira.




Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa