• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MWENGE WA UHURU UMEHITIMISHA MBIO ZAKE MKOANI KILIMANJARO

Posted on: April 9th, 2024


 

Mbio za Mwenge wa Uhuru zimehitimishwa Mkoani Kilimanjaro Aprili 8,2024 baada ya kukimbizwa katika halmashauri zote saba za Mkoa na kupitia miradi 47 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 29.34

Ikumbukwe kuwa mbio hizo zilizinduliwa rasmi Kitaifa Mkoani Kilimanjaro Aprili 2,2024 katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb) na kuanza kukimbizwa katika Manispaa ya Moshi na kuhitimishwa katika halmashauri ya Wilaya ya Same Aprili 8,2024.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amesema jumla ya miradi 47 yenye jumla ya thamani ya Shilingi Bilioni 29.34 imetembelewa na Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri zote za Mkoa ambapo miradi hiyo 12 imewekewa Mawe ya Msingi, miradi 16 imezinduliwa na miradi 19 imetembelewa ikiwemo sekta ya Afya miradi 7, Barabara na madaraja miradi 6, Elimu miradi 7, Maji miradi 7, Utunzaji wa  mazingira miradi 7, Vijana Miradi 7 na miradi mengineyo 6.

 

Mhe. Babu amesema hayo Wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru kutoka Mkoa wa Kilimanjaro kwenda Mkoa wa Tanga leo Aprili 9, 2024 katika viwanja vya Mazinde Mkoani Tanga.

 

Aidha, Mhe. Babu amesema Mwenge wa uhuru umepata fursa ya kutembelea  miradi mbalimbali ya makundi ya vijana wakiwemo wenye ulemavu na wanawake ambao wamedhamiria kuzalisha mali na kujiendeleza kiuchumi. Vilevile Mwenge wa uhuru umezindua klabu za kupambana na Rushwa, Madawa ya kulevya, Malaria, uhifadhi na uendelezaji wa mazingira.

Hata hivyo, Mhe. Babu amesema kuwa  miradi yote iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 imechangiwa na Wananchi, Serikali na wadau mbalimbali wa maendeleo ndani na nje ya Mkoa wa Kilimanjaro ikiwa na dhamira ya kuendeleza falsafa ya kujitegemea.

 

Ameendelea kusema  mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2024 zimejikita katika kukuza na kusimamia kwa karibu mabadiliko ya tabia nchi, hifadhi ya mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji kwa kukuza ushirikishwaji wa wadau wote kwa kuakisi kauli mbiu isemayo: - “Tunza mazingira, na Shiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa ujenzi wa Taifa Endelevu’’. 

Hivyo, Mkoa umeweza kuratibu zoezi la upandaji wa miti kutoka miti 7,857 mwaka 2022/2023 na hadi kufikia Februari, 2024 miti 8,709,200 imepandwa. Serikali na wananchi wa Mkoa wa Kilimanjaro wamedhamiria kwa pamoja kurudisha uoto wa asili wa mkoa wa Kilimanjaro na mlima Kilimanjaro kwa kuzingatia Sera, sheria, kanuni na Taratibu za uhifadhi wa mazingira hivyo jumla ya miti 2,487,095 ikiwemo miti ya matunda imepandwa katika kipindi hiki cha mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 mkoani Kilimanjaro.

Mkoa umeendelea kuwahimiza wananchi juu ya umuhimu wa kushiriki katika mapambano ya UKIMWI hivyo basi kiwango cha maambukizi ya VVU  kwa Mkoa wa Kilimanjaro kimeendelea kushuka kutoka asilimia 3.9 mwaka 2011/12 hadi asilimia 2.6 mwaka 2016/17 kwa watu wa umri wa miaka 15 hadi 64. Takwimu hizi ni kwa mujibu wa tafiti 4 za kitaifa zilizokwishafanyika hadi sasa.  

Aidha, katika mikesha ya Mwenge wa Uhuru, jumla ya wananchi 2331 (Me 1443 na Ke 888) walijitokeza kupima maambukizi ya VVU na UKIMWI na waliokutwa na maambukizi ni wananchi 13 (Me 5 na Ke 8).

 

Hata hivyo Mhe. Nurdin Babu amewapongeza na kuwashukuru Wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa kwa mwaka 2024 wakiongozwa na Ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava pamoja na wataalam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kazi kubwa waliyoifanya katika Mkoa wa Kilimanjaro.

 

 

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa