• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MWENGE WA UHURU WAZINDUA ZAHANATI YA MASANDARE WILAYANI SAME

Posted on: June 30th, 2025

WAKINAMAMA Wajawazito katika kata ya Stesheni wilayani Same mkoani Kilimanjaro waliokuwa wakitembea umbali wa kilomita 10 kufuata huduma za afya hospitali ya wilaya wameondokana na adha hiyo baada ya Serikali kuikarabati zahanati ya Masandare.

Akizungumza Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2025, Ismail Ali Ussi mara baada ya Mwenge kufika kuzindua zahanati hiyo alisema kuwa hapo awali ilikuwa inafanya kazi japo baadhi ya huduma zilikuwa hazitolewi katika zahanati hiyo.


Alisema kuwa, wananchi wa kitongoji cha Masandare walikuwa wakikabiliana na changamoto za miundombinu ya sekta ya Afya jambo ambalo lilikuwa likipelekea baadhi ya huduma kuzikosa katika eneo hilo lakini serikali iliona haja ya kwenda kuiboresha zahanati hiyo.

"Mwenge wa Uhuru umepata heshima kubwa ya kufika katika eneo hili ili kuonyesha matumaini, upendo kwa wananchi hivyo wananchi watakuwa na uhakika wa kupata huduma iliyo bora za Afya" Alisema Ussi.


Kiongozi huyo aliongeza  "tunahitaji kupeana pongezi za hali ya juu kutokana na ukarabati wa zahanati hii ukiingia ndani unaona huduma ya mama na mtoto kwa hali ya ubora tunatambua wakinamama wetu hawa wanapokosa huduma ya kujifungulia katika eneo hili inakuwa ni changamoto kubwa".

Alisema kuwa, wakinamama hao Wajawazito walikuwa wakilazimika kutembea umbali wa kilomita 7-10 kufuata huduma katika hospita ya Same ambapo ni changamoto jambo ambalo linaweza likapelekea vifo vya kina mama na watoto.

Alitumia nafasi hiyo kuwaasa wananchi kuitunza zahanati hiyo kwani Serikali imeshatimiza wajibu wake wa kuikarabati upya na kuweka mazingira safi na madaktari wataendelea kutoa huduma iliyo bora.

Awali akisoma taarifa za ukarabati wa zahanati hiyo, Mganga Mfawidhi wa zahanati hiyo, Ally Said alisema kuwa ukarabati wake umegharimu milioni 50.

Alisema kuwa, toka kukamilika kwa zahanati hiyo jumla ya wamama 231 wamejifungua salama, watoto 711 wamepata chanjo, wajawazito 1050 wamehudhuria kliniki na wagonjwa wa nje 1750 wametibiwa.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • MWENGE WA UHURU WAZINDUA ZAHANATI YA MASANDARE WILAYANI SAME

    June 30, 2025
  • MRADI WA MAJI WA MROYO - KIZANGAZE KULETA MATUMAINI MAPYA KWA WANACHI WA KATA YA MAORE.

    June 30, 2025
  • VIJANA CHANGAMKIENI FURSA ZA MKOPO WA SERIKALI

    June 29, 2025
  • WEKEZENI KWENYE MIRADI KUONGEZA AJIRA

    June 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa