• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

MWENGE WAKABIDHI HUNDI YA ML.3 KWA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUMU

Posted on: April 8th, 2024

Mwenge wa Uhuru umekabidhi hundi ya Tshs. 3 kwa kituo cha watoto wenye mahitaji maalumu Mama Kevina ikiwa ni sehemu ya michango ya fedha za Mwenge katika halmshauri ya Same.

Akikabidhi hundi hiyo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Ndg. Godfrey Mnzava wakati alipotembelea kituo hicho ametoa wito kwa wazazi wanaopelekea watoto kwenye vituo vya kulelea watoto wenye mahitaji maalumu kuwatembelea kila wakati ili kujua maendeleo yao na wanapopata nafuu wanaweza kuwarudisha nyumbani kuendelea na maisha ya kawaida.

Hata hivyo, Mnzava amewataka wananchi wote nchi nzima kutowaficha watoto wenye mahitaji maalumu na kuacha tabia wa kuwanyanyapaa na kuwatenga kwani na wao ni binadamu kama watoto wengine.

Akisoma taarifa ya kituo hicho Maria Kijangwa Raymomd amesema kituo hicho kilianzishwa na shirika la kidini Jimbo Katoliki Same chini ya Dada wadogo wa Mt. Fransisko wa Assis mwaka 2008 kwa lengo la kutoa huduma mbili ikiwa ni uchunguzi ambapo hufanywa na watumishi wa kituo hicho kwa kushirikiana na watumishi wa Halmashauri kwa kutembea kwenye makazi ya wananchi ili kuwabaini watoto wenye mahitaji maalumu na kuwapa elimu wazazi na walezi ya viashiria vya ulemavu. Huduma ya pili ni matibabu ya watoto hao ambayo yanahusisha mazoezi ya viungo ambapo wazazi na walezi huelekezwa namna ya kuwasaidia watoto hao.

Vile vile Maria amesema takribani watoto walemavu 600 wameweza kufikiwa majumbani kupatiwa huduma huku 44 wakiwa kituoni kwa ajili ya kupatiwa elimu, malezi na uangalizi maaalumu.

Ameendelea kusema watoto 12 wamesaidiwa kupata elimu katika shule ya Sekondari na 33 elimua ya Msingi.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Kasilda Mgeni amesema kituo hicho kimekua mkombozi kwa wananchi wa halmashauri ya Same kwa  kuwasaidia wazazi na walezi kujengewa uelewa wa namna ya kuwajali watoto wenye mahitaji maalumu kama vile watoto wenye ulemavu, kuongea na wenye utindio wa ubongo.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa