• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

Posted on: May 12th, 2025

Maelfu ya waombolezaji  kutoka maeneo mbalimbali  nchini Tanzania,  wamejitokeza katika uwanja wa C.D Msuya  uliopo wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro  kwa lengo la kuaga mwili wa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri mkuu (Mstaafu) Hayati Cleopa David Msuya(94).

Pamoja na hilo, walikuwepo viongozi waandamizi wa  serikali ya awamu ya sita akiwemo  Waziri wa Nchi,  Ofsi ya Waziri Mkuu , Sera Bunge na Uratibu Mhe. William Lukuvi  pamoja  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais, Sera  Uratibu  na   baraza  la wawakilishi Serikali  ya Mapinduzi ya Zanzibar  Mhe. Hamza Hassan  Juma.

Mwili wa Hayati Msuya, uliwasili mkoani Kilimanjaro  Mei 12 majira ya saa mbili asubui  kwa ndege maalumu  ukitoke jijini  Dar es Salaam  na kulakiwa na maelefu ya watu wakiwemo viongozi wa Serikali wa ngazi mbalimbali pamoja na viongozi wa vyama vya siasa.

Ulitembezwa  kwa mwendo wa pole na gari maalumu liloongozwa  na jeshi  la wananchi wa Tanzania  na kupitia barabara Kuu ya Arusha -Moshi hadi katika viwanja vya C.D MSUYA vilivyopo wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro  na kulakiwa na maelfu  ya watu wakiwemo viongozi wa dini.

Akitoa mahubiri katika    ibada  iliyoongozwa katika viwanja  vya C.D Msuya  wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro  Askofu  mteule  wa kanisa  la Kiinjili Kilutheri Tanzania KKKT Dayosisi  ya Mwanga,  Dk. Daniel  Meno aliwataka wananchi  kujitambua  na kuwaepuka viongozi watakaokuja kwa ajili ya kuwalaghai hasa kipindi  tunapoelekea Uchaguzi mkuu 2025.

Alisema kwa sasa wapo viongozi wengi wenye tabia za  kuja kununua kura ili kujipatia madaraka na kujifufaisha wenyewe kwa maslai yao na kuwataka wananchi kuona thamani  ya kura yao.

"Tuwe makini, baba yetu Msuya  ametufundisha uwajibikaji, uadilifu na  ukweli  na alikuwa kiongozi wa kweli mwenye kuleta mageuzi.Kwa sasa kuna viongozi wa aina mbili, moja ni wale wanaouliza watapata nini na wale wanaowaza wataacha nini,  ni wajibu wetu tunapoelekea kwenye uchaguzi mkuu 2025 kupima  na kuchagua viongozi wenye tija.

"Wanamwanga  tuendelee  kushikamana, tusikubali kubaguana  kwa sababu yoyote ile ikiwemo   kabila zetu na dini zetu,vyeo, elimu zao,"alisema

Naye Waziri  Mkuu Mstaafu Mhe.  Mizengo Pinda alisema kitu pekee  ambacho anaweza kukizungumza kwa uwakika ni kuwa Msuya alikuwa akisema ukweli  hata kwenye mazingira yasiyofaa.

"Nimefanya nae kazi  kwa muda mrefu zaidi, nimechota hekima zake kidogo, alikuwa ni jasiri na mtu ambaye anasema ukweli hata kwenye  mazingira magumu ila alikuwa na  maono ya mbali  katika kuisimamia Amani, uadilifu na uchapaka kazi,

"Niongezee kidogo alichosema  askofu  Mono,  pale kwa uuzaji wa kura, hili ni kwa watanzania wote na sio kwa wanamwanga tu,  mtu yoyote anayetaka madaraka  au aliopo madarakani apimwe kwa kazi aliyofanya na sio vinginevyo,"alisema  Pinda.

Alisema  watanzania wasikubali kuwa watumwa wa wataka madaraka na badala yake kujione mwenyewe kiongozi huyo ameacha alama gani au analeta tija gani na sio  ametupa kiasi gani.

Akitoa salama za Rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu  aliishukuru  kamati ya maandalizi ya kitaifa kwa jitiada zao za kuhakisha mwili umefika salama katika mkoa wa Kilimanjaro na kuomba ushirikiano zaidi hadi kumpumzisha mzee Msuya.

"Maisha ya mzee wetu ni kitabu ambacho kimewafundisha wengi, matokeo ya kitabu hichi ni kujipima katika utekelezaji na kuitumikia jamii husika," alisema


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • RC KILIMANJARO ATAKA WATUMISHI WA UMMA KUTII SHERIA NA KANUNI ZA KAZI ILI KUONGEZA KAZINI

    May 01, 2025
  • Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Kiseo Nzowa, akihutubia wananchi na viongozi mbalimbali katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani.

    May 01, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa