• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC ASISITIZA USHIRIKIANO

Posted on: June 17th, 2021

Serikali Mkoani Kilimanjaro imewataka Watendaji  pamoja na Madiwani  kuendelea kushirikiana  katika utekelezaji  wa majukumu ili kukuza uchumi wa Wilaya, Mkoa na Taifa kwa ujumla.


Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Stephen Kagaigai katika Baraza Maalumu la Madiwani la kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Wilayani Siha.


Mhe. Kagaigai alisema ushirikiano miongoni mwa Watendaji  na Madiwani utasaidia kuongeza ukusanyaji wa mapato na kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.


"Mkurugenzi ninakupongeze licha ya kuwa umekaa hapa kwa muda mfupi lakini umezichambua hoja  kwa umakini na kwa kiwango kikubwa, madiwani endelezeni ushirikiano   na simamieni  mapato na matumizi, wakati huo huo mbuni vyanzo vipya vya mapato, " alisema Mkuu wa Mkoa


Aidha Mhe. Kagaigai alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Bw. Ndaki Mhuli, kuhakikisha anaongeza umakini kwa kuboresha  Kitengo cha Ukaguzi wa ndani ili  kimsaidie kujitathimini kwa kina wakati changamoto zinapotokea.


Kwa upande wake Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro. Dkt. Seif Shekalaghe amempongeza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kwa maandalizi mazuri ya kikao ikiwa ni pamoja na taarifa kuwa na hoja ambazo hazijafungwa na kutoa sababu za kutojibiwa kwa hoja hizo hadi sasa, jambo ambalo limerahisisha mjadala kwenye kikao.


Awali akisoma taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Bw. Mhuli alisema    tayari amekijulisha kikao kuwa Halmashauri imeshatatua changamoto zilizokuwepo hususani kwenye

 kuongeza  mapato pamoja na kufunga hoja zilizoainishwa na CAG.




Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa