• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

RC KAGAIGAI ASHAURI WATENDAJI WA HAI

Posted on: June 23rd, 2021

Halmashauri ya Wilaya ya Hai imetakiwa kutekeleza ushauri na maelekezo yaliyotolewa na Baraza la Madiwani wa Halmashauri juu ya hoja za Mkaguzi ambazo hazijafungwa.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Stephen Kagaigai katika Baraza Maalumu la Madiwani la kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2019/2020 Wilayani Hai.


Aidha amemuelekeza Katibu Tawala Mkoa kufuatilia baadhi ya hoja ambazo zinajirudia katika kila halmashauri. Akitoa mfano wa hoja ya dawa ambazo zimeisha muda wake wa matumizi Mhe. Kagaigai amesema hoja hii inapaswa kufungwa kwa kufuata taratibu zilizopo na kuziteketeza.


Kuhusu ukusanyaji wa mapato Mhe. Kagaigai amesema  Halmashauri zingine ziko hatua nzuri za ukusanyaji wa mapato ukilinganisha na Halmashauri ya Hai iliyokusanya asilimia 74% ya mapato, amesema hii  inatokana na kutokufanya ufuatiliaji wa ukusanyaji wa mapato kwa baadhi ya maeneo. Hata hivyo amewaelekeza Watendaji wa Halmashauri hiyo kufuatilia vyanzo vya ukusanyaji wa mapato hayo napia kujitahidi kubuni vyanzo vipya ambavyo vinaweza kuwaingizia mapato.


Katibu Tawala Mkoa Dkt. Seif Shekalaghe pamoja na kupokea maelekezo ya Mhe. Mkuu wa mkoa ametoa ushauri kwa Halmashauri hiyo kwa kuwapa njia ambazo zitasaidia kutojirudia kwa hoja. Amesema kila mtu akiwajibika kwa nafasi yake  itasaidia kupunguza tatizo hilo, kufanya kazi kama timu, kuchukua hatua kwa wakati, kubadilika kwa kuwa wazalendo na kufuata taratibu zinazohusika.


Mweka hazina wa Halmashauri hiyo Juma Kasoga akiwasilisha taarifa ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali ameshauri Baraza  la halmashauri hiyo kufuata sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2013 ili kutojitokeza kwa mapungufu madogomadogo wakati wa ukaguzi.




Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa