• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

TPC Waanza Msimu Mpya wa Uzalishaji

Posted on: June 11th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Dkt Anna Mgwhira ameupongeza uwongozi wa kiwanda cha Sukari TPC kwa kuanza uzalishaji wa Sukari katika msimu wa 2020/2021ambapo wanatarajia kuzalisha takribani tani elfu 93 za sukari licha ya kukabiliwa na changamoto ya mafuriko ambayo imeathiri uzalishaji wa miwa katika mashamba kiwanda hicho


Akizungumza katika ghafla ya uzinduzi wa msimu huo Dkt. Mgwhira amesema hatua hiyo itasaidia kuwaondolea adha walaji kulanguliwa  kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kuagiza sukari  kutoka nje ya nchi na kuiuza kwa wananchi kwa bei ghali.


Aidha Dkt.Mgwhira amewataka wafanyabiashara kuwa waadilifu kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazotolewa na bodi ya Sukari ikiwemo ukomo wa bei elekezi ifikapo juni 30/ 2020 kwani kuanzia kipindi hizo sukari itakayozalishwa ndani ya nchi itatosha kukidhi mahitaji ya wananchi.


Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Utawala wa kiwanda cha TPC Bw. Jaffary Ally amesema uzalishaji wa sukari umeshaanza rasmi ambapo wanatarajia kuzalisha  kwa ziada ikilinganishwa na msimu uliopita kwa kuzalisha takribani tani 93,000 kutoka tani 89,000 walizozalisha msimu uliopita ili kutatua changamoto ya uhaba  wa sukari hapa nchini.



Bw. Ally amesebainisha changamoto kubwa waliyonayo kwa Sasa ni mafuriko yaliyosababishwa na mvua za masika ambapo maji yamefurika mashambani na kuharibu miwa iliyokuwa shamabani pamoja na miundombinu  ikiwemo na barabara na reli zinazotumika kusafirisha miwa kutoka mashambani hadi kiwandani .


Aidha Bw. Ally amewataka wasambazaji wa Sukari kufuata taratibu za usajili zinazotolewa na Serikali kupitia Bodi ya Sukari  ikiwemo kutofungasha sukari kwenye mifuko yenye ujazo wowote ambayo haina nembo ya mzalishaji kwani ni kinyume cha sheria na kunahatarisha afya za walaji.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa