• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UVUVI HARAMU MARUFUKU

Posted on: July 11th, 2017

Serikali za mikoa ya Kilimanjaro na Manyara zimetangaza kuwa  vita dhidi ya uvuvi haramu itaendelea kuwa endelevu ili  kuhakikisha fursa zote zinazotokana na rasilimali zinatumika na kizazi cha sasa na kijacho.

Msimamo huo umetangazwa na Mkuu wa Mkoa wa Dkt. Joel Bendela  katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nyumba ya Mungu wilayani Simanjiro mkoani Manyara uliokuwa na lengo la kuwatangazia wananchi kufunguliwa rasmi kwa uvuvi katika bwawa la Nyumba ya Mungu..

Aidha Mhe. Bendela ambaye alifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira pamaoja na Wajumbe wa Kamati za Uinzi na Usalama za Mikoa hiyo amesema kuwa hatua hiyo ni matokeo makubaliano ya pamoja ya serikali katika mikoa hiyo miwili.

Mhe. Bendera amesisitiza kuwa kufungukiwa kwa shughuli za  uvuvi katika bwawa hilo nkunalenga kuwawezesha wananchi kushughulika na uvuvi halali na kupiga marufuku  watu wasio waaminifu kutumia ruhusa hiyo kwa kufanya shughuli za uvuvi haramu.

Mhe. Bendela amesema mbali na ruhusa ya kufanya shughuli za uvuvi halali, wavuvi ni lazima wafuate sherea,kanuni, taratibu pamoja na masharti kadhaa yaliyowekwa na serikali ili kuhakikisha kuwa uvuvi wa samaki  katika bwawa hilo unakuwa endelevu na kuleta tija kwa wananchi.

Miongoni mwa masharti ya shughuli za uvuvi ni pamoja na kuendesha shughuli zao kwa muda wa miezisita kuanzia mwezi juni hadi julai mwakani ambapo bwawa hilo litafungwa tena kwa muda wa miezi sita.

Sharti lingine ni kuhakikisha kuwa samaki watakaovuliwa wasipungue ukubwa wa nyanda tatu kwani ndiyo ukubwa sahihi unaokubalika kitaalam ili kuhakikisha kuwa samaki wachanga wanaendelea kukuwa ili watumike wakati mwingine.

Mbali na hilo wavuvu wote wametakiwa wauze samaki wao katika mialo inayokubalika na kuainishwa na serikali ili kuepuka uuzwaji wa samaki kiholela jambo ambalo litaikosesha serikali na takwimu sahihi za uvuvu na uuzaji wa samaki katika bwawa hilo.

Kuhusu usafirishaji wa samaki kutoka bwawanii kuelekea masokoni  Mhe. Bendela amewataka wananchi kutumia magari yenye mabodi yenye muundo wa boksi ambayo yatakuwa na hali ya ubaridi kwa ndani inayokubaliana na uhifadhi na usafirishaji wa samaki.

Aidha  serikaliza mikoa hiyo  imetoa onyoatumishi wa umma na mtu yeyote atakayebainika kujihusisha na dhuluma au  maonyanyaso kwa wananchi wanaojisisha na shughuli za uvuvi bila kukiuka sheria na taratibu zilizowekwa.

 Shughuli za uvuvi ktika bwawa la Nyumba ya Mungu zilizuiwa kuanzia Jula 1,2016 hadi Juni 30,2017 ili kuruhusu samaki kukua na kuzaliana zaidi baada ya wavuvi kuvua samaki wachanga.



Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO ASISITIZA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANANCHI WILAYANI HAI

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA SIHA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI BORA WA MAPATO

    June 17, 2025
  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa