• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UZINDUZI SHULE YA MSINGI DARAJANI

Posted on: April 6th, 2024


Mwenge wa Uhuru umezindua Shule mpya ya Awali na Msingi Darajani iliyopo Kitongoji cha Faru kata ya Njiapanda kwenye Mamlaka ya Mji Mdogo wa Himo Wilayani Moshi  Aprili 6, 2024.

Akizindua mradi huo Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ameelekeza halmashauri kufanya maboresho madogo katika majengo ya awali ikiwemo Vyoo kwa kupandisha tofali mbili katika kuta zinazotenganisha choo kimoja na kingine vile vile eneo la nje lenye shimo ambalo  amelekezeka lizibwe kwa lengo la kuepusha madhara yanayoweza kutokea kwa wanafunzi lakini kwa kushauri na kupata kibali maalumu kutoka Ofisi ya Rais -  TAMISEMI.

Ndg. Mnzava amemuelekeza Mkurugenzi wa Hlamshauri ya Moshi Vijijini Shadrack M. Mhagama pamoja na Mwenyekiti Mhe. Morris Makoi  kuhakikisha gata za maji zinawekwa katika majengo ya shule hiyo hata kama ziliondolewa katika maelekezo kwani itawanufaisha na uvunaji wa maji pamoja na utunzaji wa majengo hayo lakini ni vyema kutosubiri kila jambo zuri la maenendeleo kufanyiwa na Serikali.

Aidha, Ndg. Godfrey Mnzava ameendelea kusisitiza kuhusu matumizi ya Mfumo wa Manunuzi  na kuhakikisha vifaa vyote vya miradi pamoja na mahitaji mengine yapitie kwenye mfumo pamoja na  kuwapatia mafunzo watumishi wote waliopo chini yake kwa lengo la kukuza uelewa wa Mfumo huo.

Katika kutekeleza mradi huo, Halmashauri ilipokea fedha kiasi cha Shilingi 348,500,000.00 kutoka Serikali Kuu  kwa ajili ya kutekeleza mradi huo wenye vyumba 7 vya madarasa, jengo la Utawala, matundu 16 ya vyoo, kichomea taka, vyumba 2 vya madarasa ya awali na ununuzi wa madawati 135 na samani za ofisi.

Hata hivyo, hadi kukamilika mradi huo umetumia kiasi cha Shilingi milioni 337,771,110.98 kati ya Shilingi 348,500,000.00. Fedha zilizobaki ni Shilingi 10,728,889.02 ambazo ni fedha za matazamio.

Pia, shule hiyo  imesajiliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ikipewa namba ya EM. 30205  ikiwa na idadi ya wanafunzi 377 wakiwemo wavulana 202 na wasichana 175.

Uwepo wa shule mpya hii imesaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika darasa moja kwa kuongeza nafasi 377 za usajili wa wanafunzi, Kupunguza umbali mrefu kilomita 3 kwa wanafunzi waliokuwa wanalazimika kusoma kwenye shule zilizo mbali na makazi yao ambazo kama Shule ya Awali na Msingi Dr. Shein, Njiapanda, Himo na Korona.

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa