• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UZINDUZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU MKOANI KILIMANJARO 2024

Posted on: April 2nd, 2024

   

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), amezindua rasmi mbio za Mwenge wa Uhuru leo Aprili 2,2024 katika uwanja wa chuo kikuu cha Ushirikia Moshi.

Wakati wa hafla ya uzinduzi wa mbio hizo amewataka wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa  kulitendea haki taifa kwa kufanya kazi waliyoaminiwa na kuhakikisha wananchi wanaondoka na ujumbe uliokusudiwa wa kuhamasisha tunu za taifa ambazo ni amani, uzalendo, umoja na mshikamano ndani ya Taifa na pia kuchochea shughuli za maendeleo.

Aidha, Mhe. Majaliwa amesema kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 umebeba ujumbe wa uchaguzi na utunzaji mazingira  hivyo amewasisitiza wananchi kwamba uchaguzi  ni haki ya kila mtanzania  kuchagua na kuchaguliwa na hivyo anawakumbusha kuhakiki jina katika daftari kabla ya zoezi la upigaji kura pamoja na kutunza mazingira katika maeneo yote kwa kupanda miti kwenye makazi yao na kutunza vyanzo vya maji.

Vilevile Mhe. Majaliwa amesisitiza wananchi juu ya kuzingatia lishe bora, kujikinga dhidi ya maambukizi ya VVU na UKIMWI,kujikinga na ugonjwa wa malaria, mapambano dhidi ya rushwa pamoja na dawa za kulevya..

Waziri wa Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Mhe. Tabia Mwita amesema baada ya uzinduzi wa mbio za Mwenge wa Uhuru utakimbizwa kwa siku 195 katika mikoa 31 na halmashauri 195.  Amesema vijana 6 ambao ni wakimbiza Mwenge kitaifa wataenda kuwakumbusha wananchi juu ya historia na uzalendo wa nchi yao.

Naye, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amesema Mwenge wa Uhuru wa Mwaka huu ni maalumu hii ni kutokana na kubeba 60 tatu ambazo 60 ya kwanza ya Mbio za Mwenge wa Uhuru, 60 ya pili Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na 60 ya tatu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Amesema Mwenge wa Uhuru huleta huduma kwa wananchi karibu za kiuchumi na kijamii, kuimarisha uzalendo, kuondoa ukabila na kuunganisha taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Nurdin Babu amesema jumla ya miradi 47 yenye thamani ya Tshs. Bilioni 29,340,412,701.88 itatembelewa, kuwekewa mawe ya msingi na kukaguliwa na Mwenge wa Uhuru, kati ya miradi hiyo 12 ni yakuwekewa mawe ya msingi, 16 yakuzinduliwa na 19 ni ya kutembelewa.

Aidha, Mhe. Babu amesema katika kipindi cha miaka 3 ya Uongozi wa awamu  ya Sita mkoa wa umepokea jumla ya Tshs. Bilioni 828.75 fedha ambazo zimetekeleza miradi 1,190 ya maendeleo katika sekta ya afya,elimu, miundombinu ya barabara, maji, kilimo, mifugo, usafirishaji na uchukuzi, mipingo miji, utalii na uwezeshaji wa wananchi kiuchumi

Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • KATIBU TAWALA MKOA WA KILIMANJARO ASISITIZA UTOAJI WA MIKOPO YA ASILIMIA 10 KWA VIKUNDI VYA WANANCHI WILAYANI HAI

    June 18, 2025
  • HALMASHAURI YA SIHA YAPONGEZWA KWA UKUSANYAJI BORA WA MAPATO

    June 17, 2025
  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa