• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

UZINDUZI WA WIKI YA MAJI

Posted on: March 16th, 2022

Zaidi ya wananchi 324,797 katika vijiji 179 mkoani Kilimanjaro wanaenda kunufaika na huduma ya maji safi baada ya serikali kutenga kiasi cha Tshs. Bilioni 12.3 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 katika utekelezwaji wa miradi ya maji 27.

Aidha, Serikali imetoa kiasi cha Tshs. Bilioni 3.5 kutoka kwenye fedha za mpango wa ustawi wa Taifa na mpambano dhidi ya UVIKO-19 zitakazotumika kutekeleza miradi ya maji 7 katika wilaya zote sita za mkoa wa Kilimanjaro.

Ameyasema hayo Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.  Stephen Kagaigai wakati wa uzinduzi wa wiki ya maji Machi 16,2022 mkoani hapa na kuwaelekeza RUWASA kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa wakati na kutosita kuwachukulia hatua wanaoshindwa kufanya kazi kwa utaratibu uliowekwa.

Mhe. Kagaigai amesema Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Moshi (MUWSA) imetengewa kiasi cha Tshs. Bilioni 16 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji kwa mwaka wa fedha 2021/22. Amesema mamlaka hiyo imefanya usanifu wa kuboresha huduma ya maji katika maeneo mapya ya huduma ya Kata 12 katika halmashauri ya Moshi na thamani ya utekelezaji wa miradi hiyo ni Tshs. Bilioni 11.3 na kufikia hadi sasa mamlaka imetekeleza miradi hiyo kwa asilimia 31.68 kwa thamani ya Tshs. Bilioni 2.7.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa bonde la maji mto pangani Segule Segule amesema pamoja na kutunza vyanzo vya maji wameendelea kuweka mipaka ili kuepuka uharibifu wa mazingira.

Mkuu wa kitengo cha mipango na biashara wa MUWSA, Tumaini Marandu amesema Mamlaka imepanga kutekeleza miradi minne kwa kuongeza kiwango cha maji kufikia mita za ujazo 23,067. Amesema vyanzo vinavyoongezwa ni chemchemu ya Karanga mita za ujzo 2,592, Miwaleni mita za ujazo 2,592, Mkolowonyi mita za ujazo 1,296 na Njoro ya Dhobi mita za ujazo 16,587.


Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • BASATA YAWANOA MAAFISA UTAMADUNI NA BIASHARA KILIMANJARO

    May 22, 2025
  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa