• Wasiliana nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Kilimanjaro Region
Kilimanjaro Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Kilimanjaro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhamira
    • Historia ya Mkoa
    • Viongozi wa Mkoa
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Sekretariati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimaliwatu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
      • Trade and Investment
      • Administration and Human Resource Department
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Teknologia ya Habari na Mawasiliano
      • Kitengo cha Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ukaguzi wa Ndani
    • Miongozo
  • Wilaya
    • Hai
    • Moshi
    • Mwanga
    • Same
    • Rombo
    • Siha
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Wilaya ya Hai
    • Halmashauri ya Wilaya ya Moshi
    • Halmashauri ya Manispaa ya Moshi
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga
    • Halmashauri ya Wilaya ya Same
    • Halmashauri ya Wilaya ya Siha
    • Halmashauri ya Wilaya ya Rombo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Viwanda
    • Uvuvi
  • Huduma Zetu
  • Machapisho
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Matangazo
    • Albam
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Wamiliki wa Hoteli Wapewa Somo la Corona

Posted on: March 24th, 2020

Serikali mkoani Kilimanjaro imewataka wafanyabiashara ya  wa hoteli kuhakikisha wanashirikiana na serikali katika kuhakikisha kuwa janga la korona linadhibitiwa ili lisiingie katika mkoa wa Kilimanjaro na hatimaye nchi ya Tanzania isipate madhara makubwa kutokana na ugonjwa wa Korona.

Akiongea wakati wa kufungua mafunzo maalum ya kujikinga na kuenea kwa ugonjwa wa korona kwa wamiliki na viongozi wa hoteli katika wilaya ya  Moshi, Kaimu Mkuu Mkoa wa Kilimanjaro Mhe.Kippi Warioba  amezitaka menejimenti za  hoteli wilayani Moshi kuyafanyia kazi  mafunzo yaliyotolewa na wataalam wa afya mkoani ili wawe na uelewa sahihi juu maambukizi na dalili za ugonjwa wa korona.

Mhe Waariba ameleza kuwa Serikali mkoani Kilimanjaro inatekeleza agizo la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe magufuli  kwa kuhakikisha kuwa wageni wote wanaoingia nchini  watawekwa chini ya uangalizi maalum kwa muda wa siku kumi na nne kabla ya kuruhusiwa kuchangamana na watu ndani ya nchi ili kuendelea na shughuli zao.

Aidha Mhe. Warioba amewaambia wafanyabiashara hao kuwa wageni watafikia katika hoteli na watakuwa chini ya usimamizi wa wataalam wa afya pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama  na kuwataka wasiwe na hofu baadala yake wazingatie taratibu za kuchukua tahadhari kama zinavyotolewa na wataala wa afya na serikali ."Tusifanye mambo kwa woga na tuwe na tafsiri sahihi ili mtu asiye mgonjwa akaitwa au kuhudumiwa kama mgonjwa" alifafanua Mhe. Warioba.

Kuhusu  tahadhari ya ugonjwa wa korona ndani ya hifadhi ya taifa ya Mlima Kilimanjaro,  Mhe. Warioba amewotoa hofu wafanyabiashara hao na wadau wote wa utallii na kuwahaikishia  kuwa uongozi wa  Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA)  wamejipanga kuhakikisha kuwa watu wote wako salama na endapo itatokea mgeni, muongoza wageni, mpagazi au mtumishi yeyote ataonesha dalili za ugonjwa atapata huduma na wengine kulindwa ili wasiambukizwe.

Mhe. Warioba amewataka wananchi wote kuhakikisha wananawa  mikono kwa maji na sabuni mara kwa mara kwani inasaidia kwa kiasi kikubwa kuzuia mtu asiambukizwe majonwa ukiwemo korona.

ili kuhakikisha kuwa kila mdau anakuwa tayari katika kupambana na kuenea kwa ugonjwa wa korona Mhe. Warioba amewaagiza wafanyabiashara ya hoteli kuhakikisha wanachukua namba za simu za mkononi za wataalam wa afya ili ziwasadie kutoa taarifa endapo watapata mgeni ambaye ataonesha kuwa na dalili za ugonjwa wa korona na hatimaye serikali iweze kuchukua hatua za kunusuru maisha ya mgeni huyo na kuwalinda wananchi wengine wasiambukizwe.




Matangazo

  • Kwa Huduma Bora ya Ukumbi wa kisasa wa Mikutano, Tafadhali fika Ofisini au wasiliana nasi kwa S.L. P 3070, Moshi. au Piga simu namba 027 2758248/027 2751 February 03, 2020
  • ZOEZI LA KUBORESHA TAARIFA KWENYE DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA KUANZA MEI 16 HADI MEI 22 2025 KILIMANJARO May 15, 2025
  • MRADI WA BOOST April 01, 2023
  • Angalia Zote

Habari

  • VIJANA NA WANAWAKE MSIKOPE BILA MALENGO

    May 15, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaongoza wananchi kumsindikiza aliyekuwa Makamu wa kwanza wa Rais na Waziri Mkuu mstaafu, Hayati Cleopa David Msuya katika safari yake ya mwisho.

    May 13, 2025
  • Mwili wa Hayati Cleopa D. Msuya waagwa katika viwanja vya CD Msuya wilayani Mwanga

    May 12, 2025
  • SERIKALI KUTENGA BILIONI 7 KUTEKELEZA UJENZI WA BARABARA YA MABOGINI - KAHE

    May 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

Kujisajili kwenye mfumo wa NeST - Hatua ya Awali
Video

Kiunganishi cha Haraka

  • Webmail
  • Malalamiko
  • Watumishi Portal

Tovuti zinazohusiana nasi

  • Ikulu
  • Tamisemi
  • Utumishi
  • Mfumo wa kuomba vibali vya kusafiri nje ya nchi (LIVE)
  • Mfumo wa Usambazaji Mafaili kwa njia ya Ki-Eletroniki (E-Office)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na Kufuatilia malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani

Wasiliana nasi

    17 Barabara ya Florida

    Anuani ya Posta: P. O. Box 3070, Moshi

    Simu: +255 (027) 2754236/7

    Mobile:

    Anuani pepe: ras@kilimanjaro.go.tz / ras.kilimanjaro@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani

Hakiimiliki©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.Haki zote zimehifadhiwa